Sep 4, 2018

Je, unajua kuwa kila msanii ni wa kipekee?



KAMA wewe ni msanii, iwe wa uimbaji, uigizaji, uchoraji, uchezaji muziki, uchekeshaji, uandishi n.k., amini usiamini hakuna mtu ambaye ana kila kitu ulicho nacho wewe.

Hata kama binadamu ni wawili wawili, basi anaweza akatokea mtu mmoja tu kati ya watu maelfu ndiyo akakufanana kwa vitu vingi: sura, rangi, uzungumzaji, uwezo wa sanaa, mvuto n.k.

Kitu ambacho pengine hukijui ni kwamba mamilioni ya watu duniani wametafuta msanii kama wewe, mwenye sifa kama zako ili wamtumie kwenye matangazo, kwenye video za muziki, kwenye filamu, kwenye mfululizo wa sinema au michezo ya kuigiza maarufu kama series n.k.

Huu ni ulimwengu wa taarifa kuelekea burudani



ULIMWENGU wa sasa unakwenda kwa spidi kubwa sana na magurudumu yake ni teknolojia ya mitandao.

Dunia ya sasa imepita kwenye ulimwengu wa maarifa, sasa ipo kwenye ulimwengu wa taarifa ikikimbia kwa spidi kubwa kwenye ulimwengu wa burudani. Watu hupenda kuburudishwa zaidi ya kuelimika.

Burudani ni muhimu kwa kuwa inawaleta watu pamoja na ni njia nzuri ya familia nzima kujumuika pamoja. Inawatoa watu kutoka kufikiria changamoto za maisha na kuwaburudisha huku ikiwaondolea msongo wa mawazo unaotokana na ugumu wa maisha.

Kwa kawaida, burudani ni kufurahi, kuchangamka na kufurahisha. Burudani inaweza kuwa muziki, matamasha, simulizi, filamu, michezo, ngoma na maonesho ya jadi.

Mwandishi wa Marekani ambaye pia ni mjasiriamali, na mwalimu, Tony Robbins anabainisha kuwa, “Hatupo katika kizazi cha taarifa na maarifa. Tupo katika kizazi cha burudani na starehe.”

Sep 1, 2018

Sanaa hustawisha fikra



SANAA ni hazina muhimu sana inayohifadhi kazi ya uumbaji, ina lugha pana ambayo hakuna lugha yoyote nyingine yenye upana kama huo.

Hii si lugha ya sayansi, wala lugha ya kawaida, wala lugha ya mawaidha yenye upana kama wa lugha ya sanaa. Inapaswa ipewe umuhimu na pafanyike juhudi za kuhakikisha muundo wa kujivunia wa sanaa unatumiwa.

Bila ya kuwepo sanaa, matamshi ya kawaida hayawezi kupata nafasi yake katika akili ya mtu yeyote yule. Sanaa ni ala na nyenzo nzuri sana ya kufikisha na kupanua fikra sahihi.

Aug 17, 2018

Tuviendeleze vipaji ili viitangaze nchi kimataifa



KILA mtu aliyezaliwa na mwanamke anacho kitu cha pekee alichojaaliwa kuwa nacho. Kitu hiki si umbile lake, elimu yake, umaarufu wake, usomi wake, cheo chake katika jamii, au utajiri wake wa vitu na fedha; la hasha, bali ni kipaji chake.

Kipaji ni uwezo wa kiasili ulio ndani ya mtu katika maumbile, nafsi na roho yake. Kipaji kinatoka ndani yake. Ni tunu au zawadi toka kwa Mungu ambayo hakuna anayeweza kutunyang’anya au kutuibia mpaka tutakapokufa.

Fedha na magari vyaweza kuibiwa, nyumba inaweza kuanguka, kubomoka, kubomolewa au hata kuungua, lakini vipaji hubakia kuwa nasi daima.

Kipaji ni karama. Ni zawadi anayokirimiwa mtu kutoka kwa Mungu. Kipaji hiki hukua katika ufanisi na matumizi ikiwa kitakuzwa na kuendelezwa na kimenuiwa kutumika kwa niaba ya vingine, si kwa ajili ya ubinafsi bali kwa faida ya wengine na si yake wenyewe.

Tunapomuomboleza King Majuto tusisahau somo alilotuachia

Wachekeshaji mahiri nchini ambao kwa sasa ni marehemu, King Majuto na Sharo Milionea

WIKI iliyopita tasnia ya vichekesho na wapenda burudani tulipata pigo kwa msiba uliogusa na kuwashtua watu wengi sana, wafuatiliaji na wasio wafuatiliaji wa sanaa ya vichekesho, kutokana na kifo cha King Majuto.

King Majuto ambaye jina lake halisi aliitwa Amri Athuman alikuwa msanii mkongwe na maarufu nchini Tanzania na Afrika Mashariki, na gwiji wa vichekesho ambaye umahiri wake ulikuwa wa aina yake.

Majuto alifariki dunia wakati akipokea matibabu kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam, majira ya saa 2 usiku wa Jumatano Agosti 8, 2018 akiwa amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi.

Baada tu ya kifo chake watu maarufu ndani na nje ya Tanzania walituma salamu za rambirambi kwa familia yake kupitia mitandao ya kijamii, miongoni mwao akiwa Rais wa Tanzania, John Magufuli.

Tumeitupa misingi ya michezo kwa binadamu



MICHEZO si tu kwamba ina faida kubwa sana kwa mwanadamu na nchi, pia ni chombo cha kuwasilisha tunu msingi katika kuboresha ubinadamu na katika ujenzi wa jamii ya amani na ya kindugu.

Kwa kauli hiyo yatari tunapata wazo kuu juu ya michezo kwa ujumla ya kwamba michezo imekuwa na lengo kuu msingi tangu zamani za kale la kujenga undugu na amani.

Kama mchezo ni chombo cha kuwasilisha tunu ya binadamu mwenyewe, kujieleza mwenyewe, kukubalika mwenyewe na kujikubali, inamaana kwamba nchi yoyote haiwezi kutambulikana na utaifa wake bila kuwa na utamaduni wao, na mojawapo ya viungo vya utamaduni huo vinavyounganisha katika dunia hii ni michezo.

Aretha Franklin: Malkia wa Soul aliyeishi maisha ya ‘mateso ya kimyakimya’



MUZIKI ni chombo ambacho kimewavutia wanadamu. Katika kutumia nyimbo, waimbaji wameweza kuhifadhi historia na utamaduni wa jamii zao.

Muziki umekuwa ukitumika kama njia mojawapo ya kujifundisha utamaduni na aghalabu hutumiwa katika kumwelezea mtu, mazingira yake na jinsi anavyoweza kuyatumia na kuyatunza vilivyo.

Kama chombo ambacho hutumiwa kuelezea historia ya jamii, muziki hutumiwa kupasha ujumbe maalumu kwa wanajamii hasa kutoka kizazi kimoja hadi kingine na hutumiwa hasa kuelezea historia, imani, itikadi na kaida zajamii.

Nyimbo kama zao la mazingira ya jamii, zinaweza kufananishwa na mtoto ambaye hufinyangwa na mambo mengi katika historia ya jamii yake.
Hata hivyo, muziki ni zaidi ya taaluma kama zilivyo taaluma zingine za sheria, uhandisi, udaktari, usimamizi wa fedha, biashara na kadhalika. muziki ni kipawa ambacho mtu hutunukiwa na Mungu.

Aug 12, 2018

King Majuto atabaki kuwa nembo ya tasnia ya ucheshi nchini



WASANII wakongwe na mahiri nchini wa sanaa ya maigizo, hususan wa vichekesho wanazidi kupukutika, na kuwaacha wasanii wachanga wakiwa katika mkanganyiko.

Nawakumbuka wasanii ambao walikuwa mahiri sana katika sanaa ya maigizo na vichekesho enzi za uhai wao na sasa hatupo nao ni pamoja na Ibrahim Raha (Mzee Jongo), Fundi Said (Mzee Kipara), Rajab Kibwana Hatia (Mzee Pwagu) na Ali Said Keto (Pwaguzi).

Wengine ni Hamis Tajiri (Janja au Meneja Mikupuo) Tunu Mrisho (Mama Haambiliki), Branco Minyugu, Bartholomew Milulu (Masawe), Said Ngamba (Mzee Small), Said Maulid Banda (Max) na wengine.

Wasanii hawa waliifanya sanaa ya maigizo, hususan ucheshi (comedy) kujizolea umaarufu mkubwa nchini na hivyo kuwafanya vijana wengi nchini kuingia kwenye sanaa ya vichekesho.

Tuitumie fursa ya burudani kukuza uchumi na kuongeza ajira

Diamond Platnumz akitumbuiza


“HATUPO katika kizazi cha taarifa na maarifa. Tupo katika kizazi cha BURUDANI na STAREHE.” Tony Robbins.

Tony Robbins ni mwandishi wa Marekani, mjasiriamali, mwalimu na anajulikana kwa matangazo yake kwenye runinga, semina na vitabu, ikiwa ni pamoja na ‘Unlimited Power’ na ‘Awaken the Giant Within’.

Burudani ni biashara inayokua kwa kasi sana barani Afrika zaidi ya kawaida. Sekta ya burudani imejaa fursa nyingi sana kupita kawaida. Yeyote atakayeamua kuichunguza sekta hii kwa makini atashangaa fursa zilizojaa.

Kila siku mamilioni ya watu duniani wanahangaika kutafuta sehemu za kustarehe, vitu vya kujistarehesha na kujiburudisha, michezo na matamasha ya kufurahisha.

Tujitafakari upya kwenye Bongo Fleva

Wanamuziki Profesa Jay (kushoto) na MwanaFA


MUZIKI kama chombo ambacho hutumiwa kuelezea historia ya jamii, hupasha ujumbe maalumu kwa wanajamii, hasa kutoka kizazi kimoja hadi kingine na hutumiwa kuelezea historia, imani, itikadi na kaida za jamii.

Kwa kawaida nyimbo ni zao la mazingira ya jamii. Zinaweza kufananishwa na mtoto ambaye hufinyangwa na mambo mengi katika historia ya jamii yake.

Hii inamaanisha kwamba muziki hauibuki katika ombwe tupu na hauwezi vilevile kujiundia mazingira yake yenyewe. Mabadiliko na maendeleo ya muziki yamekuwa yakifuatana na historia ya watu wenyewe.

Umuhimu wa muziki unadhihirika katika matumizi ya nyimbo katika wakati maalumu kama njia mojawapo ya kuanzisha mabadiliko katika tabia za jamii au mtu binafsi.

Hatuwezi kuitenganisha sekta ya sanaa na utalii


TANZANIA ni moja ya sehemu bora kabisa duniani ambazo msanii atafurahia kutengeneza filamu yake au kupigia picha za video kwa muziki wake, historia, utamaduni na wanyamapori.

Kuna hali ya hewa nzuri na watu wakarimu ambao wako tayari kumkaribisha mgeni katika mtazamo wa Kitanzania.

Imekuwa inashangaza kuona wasanii wetu wanakwenda kufanya video zao Afrika Kusini na Kenya, wakati Tanzania inashika nafasi ya pili duniani, nyuma ya Brazil, kwa kuwa na vivutio vingi vya utalii huku nchi ya Afrika ya Kusini ikishika nafasi ya 14.

Tupaze sauti dunia ijue kuhusu michoro ya Tingatinga


SANAA ya ufundi ambayo inajumuisha uchoraji, upakaji rangi picha, ufinyanzi, uchongaji na utengenezaji wa mapambo mbalimbali ya asili ni utamaduni ambao, kwa mujibu wa machapisho mbalimbali, ilianza nchini Tanzania.

Sanaa ya uchoraji ilianzia nchini Tanzania takribani miaka 5,000 iliyopita na uthibitisho halisi ni michoro iliyopo katika mapango ya Kondoa Irangi.

Kwa miongo kadhaa, Tanzania imejulikana kwa umahiri wa uchoraji wa picha licha ya kuwa Watanzania wenyewe wametajwa kujiona kuwa siyo walengwa husika wa sanaa hii.
Sanaa ya uchoraji ni lugha ambayo ina ulingo mpana na kila msanii ana lugha yake na wapo wasanii ambao wanafanana katika mfumo wa sanaa wanayofanya na wengine hawafanani kabisa.

Apr 27, 2018

Sanaa ina mchango mkubwa katika maendeleo ya nchi


Sanaa za Tanzania
KATIKA ulimwengu wa kimaada unaodhibitiwa na fikra za kupenda dunia, thamani za utamaduni (sanaa ikiwemo ndani yake) huwa hazipewi nafasi na siku zote utajiri wote wa sanaa unapimwa kwa fedha.

Suala muhimu katika ulimwengu huo ni fedha, kwa hivyo kila kitu kinapimwa thamani yake kwa kuangalia kitaingiza kiasi gani cha fedha.

Utaona inatazamwa elimu fulani itaingiza fedha kiasi gani, inaangaliwa kazi fulani ina uwezo wa kuingiza kiasi gani cha fedha na vitu kama hivi. Lakini hali haiko hivyo katika upande wa utamaduni.

Hapana, kwani elimu ni njia ya kuwa na maisha bora, na sanaa ni chombo cha kuwa na ustawi katika maisha.

Muungano wetu na utamaduni wetu


JANA Aprili 26, Tanzania iliadhimisha miaka 54 ya Muungano tangu nchi zilizoitwa Tanganyika na Zanzibar zilipoungana na kuzaa Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania. Nchi hizi mbili yaani Tanganyika (sasa Tanzania Bara) na Zanzibar (inayojumuisha Visiwa vya Pemba na Unguja) ziliungana Aprili 26, 1964.

Jahazi linalowabeba Watanzania limeweka historia ya kung’oa nanga mara baada ya Jamhuri Muungano wa Tanzania kuzaliwa rasmi.

Hii ilitokana na ujasiri, ushupavu na nia ya dhati waliyokuwa nayo waasisi wa Muungano huu: Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (Tanganyika) na Abeid Aman Karume (Zanzibar).
Tanzania ni nchi, watu wake mmoja mmoja huitwa Mtanzania na kwa ujumla wao wanaitwa Watanzania, hivyo kuunda taifa la Tanzania.

Apr 25, 2018

Tuzuie teknolojia isikwapue haki za wasanii



Wakati Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEKNOHAMA) ikizidi kuimarika na kuchukua nafasi ya njia kongwe za mawasiliano, tasnia ya ubunifu nayo inajikuta kwenye changamoto ya kuakisi mabadiliko hayo ya wakati.

Tasnia ya ubunifu (Sanaa) ni hazina muhimu sana inayohifadhi kazi ya uumbaji; ambapo wabunifu (wasanii) wanayo dhamana ya kueneza ujumbe na elimu kwa jamii.

Tasnia hii ni mjumuiko wa hakimiliki bunifu ambazo zinapaswa kulindwa ili jamii iendelee kunufaika na kazi hizi za ubunifu, ambazo sasa zimeenea duniani kote.

Apr 18, 2018

Kusambaza video chafu, wasanii wanaelekea kubaya

Wasanii Nandy na Bill Nass katika clip ya video chafu iliyoenea mtandaoni


Hamisa Mobeto
INASHANGAZA sana! Katika kipindi ambacho Sheria za mitandaoni zimetungwa ili kudhibiti matumizi ya mitandao hiyo, ndipo mdudu mbaya sana wa video chafu kaingia katika tasnia nzima ya burudani.

Kabla ya huu mtindo mpya wa video zinazodhalilisha utu tumekuwa tukishuhudia jinsi wasanii wa kike wanavyokuwa nusu watupu kitu kinachosemwa eti ndiyo maendeleo (kupiga hatua), na pengine inabainishwa kuwa hiyo ndiyo dalili ya kuwepo kwa mafanikio katika tasnia hii.

Sakata la Diamond, Nandy:Tusipojipanga dunia itatupanga

Wanamuziki Nandy na Bill Nass katika pozi
Diamond Platnumz
KAMA mtafiti, mchambuzi, mdau wa sanaa na mwananchi wa nchi hii nimekuwa nikiitahadharisha jamii yangu kuhusu vita vinavyoendelea duniani kati ya mataifa makubwa na mataifa machanga.

Lakini hivi si vita kama vile vinavyoendelea huko Syria, wala si vita vya kupinga ugaidi n.k. la hasha! Bali ni vita vya kiutamaduni, vya kutawalana kiakili.

Vita vya utamaduni huenezwa kupitia vyombo vya habari ikiwemo mitandao, televisheni, redio, magazeti, sinema, muziki n.k. ambavyo ni jukwaa muhimu sana katika kueneza utambulisho, utamaduni na fikra za nchi husika.

Apr 13, 2018

Tuwafundishe watoto umuhimu wa michezo ya pamoja



MICHEZO ni chombo cha kuwasilisha tunu msingi katika kuboresha ubinadamu na katika ujenzi wa jamii ya amani na ya kindugu.

Michezo ina faida kubwa sana kwa mwanadamu, siyo kwa wachezaji tu bali hata kwa wanaoshabikia ambao kufurahi kwao huwa ni kinga dhidi ya maradhi, hasa inapokuwa michezo ya ushindani.

Ni wazi kuwa matatizo mengi ya kiafya kwa wanadamu yanaongezeka siku hizi kutoka na mfumo mpya wa maisha tunayoishi ukilinganisha na miaka ya nyuma. Ingawa kwa wale wanaoshiriki michezo mbalimbali mara nyingi imewasaidia kuepuka matatizo hayo.

Apr 12, 2018

Sanaa ina nafasi kubwa katika jamii

Wasanii wa kizazi kipya wanaounda kundi la Tanzania All Stars wakiwa katika sherehe za maadhimisho ya miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania Bara

UHAKIKA wa sanaa – iwe sanaa yoyote ile – ni kipaji kutoka kwa Mungu, ni hazina muhimu sana inayohifadhi kazi ya uumbaji.

Ijapokuwa kudhihiri kwa sanaa kunatokana na jinsi sanaa yenyewe itakavyobainishwa, lakini huo si uhakika wote wa sanaa. Kabla ya kubainishwa, kuna hisia na utambuzi na udiriki wa sanaa yenyewe na kwamba mambo yote yanachimbukia hapo.

Baada ya kuonekana, kutambuliwa na kubainishwa uzuri, unyofu na uhakika wa sanaa, hapo ndipo zinapoweza kuzuka maelfu na nukta ndogondogo na nyembamba sana ambazo baadhi ya wakati hawawezi kuziona nukta hizo isipokuwa wasanii wenyewe.

Mar 29, 2018

Nchi za SADC na mkakati wa sanaa kwa maendeleo

Ramani inayoonesha nchi za SADC



MAPEMA Machi mwaka huu kuliandaliwa Tamasha la Kusherehekea Wanawake wa SADC Katika Sanaa ya Maigizo na Dansi lililofanyika mjini Johannesburg.

Wanawake wa Zambia katika kikundi cha dansi walitumia michezo ya maigizo kwa ajili ya maendeleo kwa kuhamasisha wanakijiji kupanda zaidi ya miti 5,000 na kujenga majengo matatu ya madarasa kwa kipindi cha miaka mitatu katika Jimbo la Kusini mwa Zambia.

Tamasha hilo liliandaliwa na "Southern Africa Theatre Initiatives (SATI)" na lilikuwa na lengo la kuonesha jukumu la wanasanaa wanawake wa nchi za SADC kuungana na kuleta mabadiliko katika kanda.

“Wanasanaa wanawake wanapuuzwa pamoja na kazi kubwa wanayofanya kuunganisha na kuendeleza jumuiya. Wanachohitaji ni kutambua na kupatiwa msaada tu,” alisema Mpo Molepo, katibu wa SATI.