Dec 28, 2011

ILI KUDUMISHA MAADILI: Kanuni za sheria ya filamu sawa, lakini ada zinatia shaka! KULIKONI DESEMBA 30, 2011

Mwenyekiti wa Bodi ya Ukaguzi wa Filamu
na Michezo ya Kuigiza, Rose Sayore

Katibu Mtendaji wa Bodi, Joyce Fisso

MIAKA ya karibuni tasnia ya filamu imekuwa ndiyo kimbilio kubwa, chanzo cha ajira na njia ya kujikwamua kiuchumi kwa wasiojiweza au walioshindwa katika fani zingine. Jambo hili limesababisha kuwa na watendaji wasio na uwezo wala taaluma na hatimaye kuzalishwa filamu mbovu zisizokidhi viwango.

Kama mdau na mwanaharakati wa sanaa, mara nyingi nimekuwa nikishauri kuwa tuboreshe kazi zetu na kubadili mtazamo/ dhana iliyojengeka miongoni mwetu kuwa sanaa ya filamu ni kimbilio la wasiojiweza kiuchumi. Na kutambua kuwa sanaa hii ni kazi kama kazi nyingine ambayo inahitaji ubunifu, akili, maarifa na

Dec 27, 2011

Hatimaye Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) lapata viongozi kidemokrasia

Rais mteule, Simon Mwakifwamba

Makamu wa Rais, Suleiman Ling'ande

Viongozi wapya na wajumbe wa Bodi ya TAFF katika
picha ya pamoja, muda mfupi baada ya kuchaguliwa

Baada ya kuwepo kwa uongozi wa mpito, hatimaye siku ya Alhamisi Desemba 22, 2011, Shirikisho lilipata viongozi wapya kwa njia ya kidemokrasia watakaoongoza kwa kipindi cha miaka mitatu hadi 2014.



Simon Mwakifwamba aliyekuwa rais wa mpito ndiye aliyechaguliwa kuwa Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania baada ya kupita kwa kishindo kwa kupata kura zote 18 za wajumbe waliopiga kura baada ya kuwa mgombea pekee mwenye sifa za kugombea nafasi hiyo kwa mujibu wa katiba ya shirikisho.

Dec 21, 2011

TAFIDA: Viongozi waliochaguliwa wana kazi ngumu kupigania weledi

Mwenyekiti wa Tafida, Paul Mtendah

Makamu Mwenyekiti wa Tafida, John Lister Manyara

Viongozi wapya wa Tafida katika picha ya pamoja na
wanachama wa Chama cha Waongozaji Filamu Tanzania,
picha hii ilipigwa muda mfupi baada ya kumalizika uchaguzi

MWISHONI mwa wiki iliyopita, Jumapili ya tarehe 18 Desemba, 2011 kulikuwa na uchaguzi wa viongozi wa kitaifa wa Chama cha Waongozaji wa Filamu Tanzania (Tanzania Film Director’s Association “TAFIDA”), ambapo uongozi mpya uliochaguliwa siku hiyo uliashiria mwanzo mpya wa kuchipua tasnia ya filamu hasa kwa waongozaji wa filamu katika tasnia yetu. Nasema ni mwanzo mpya kwa kuwa nina imani na viongozi wapya waliochaguliwa ambao kwa kiasi kikubwa ninawafahamu kwa uchapakazi wao na kujituma.



Mwanzoni Chama cha Waongozaji wa Filamu Tanzania kilipoanzishwa na kupewa usajiri wa kudumu na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata),

Dec 20, 2011

Viongozi wapya wa Chama cha Waandishi wa Script Tanzania (Tanzania Scriptwriters Association)

Kimela Billa, Makamu Mwenyekiti 

Ramadhani Kingaru, Mjumbe 

Christian Kauzeni, Mjumbe

Hawa ndiyo viongozi waliochaguliwa kuongoza taasisi ya waandishi wa miswaada andishi ya filamu (script) kwenye uchaguzi ngazi ya taifa (Tanzania Scriptwriters Association - TASA) uliofanyika jana Jumatatu tarehe 19/12/2011 pale Vijana Social Hall - Kinondoni:

- Abdul Maisala                     Mwenyekiti
- Kimela Billa                         Makamu Mwenyekiti
- Samwel Kitang’ala             Katibu
- Subira O.Nassor Chuu       Mweka Hazina
- Mike Sangu                         Mjumbe
- Dimo Debwe                       Mjumbe

Dec 14, 2011

Kwa hili, Tanga wamedhihirisha kuongoza jahazi la filamu nchini

Mwl. Kassim El-Siagi akizungumza na wananchi
waliohudhuria tamasha hilo muda mfupi kabla
tamasha halijaanza

Nikiwa katika picha na wadau wa filamu jijini Tanga, 
katikati ni Amri Bawji (mwenye baragashia) na kulia ni
Nassib Ndambwe, mmoja wa waandishi wa script nchini

WIKI iliyopita nilitembelea jiji la Tanga wakati wa tamasha la filamu za Kiswahili zilizotengenezwa mkoani Tanga. Tamasha hilo liliandaliwa na kampuni ya El-Siagi Movies na kudhaminiwa na StarMedia kampuni ya ving'amuzi vya StarTimes, na Nyumbani Hotels & Resorts kupitia vinywaji vyake vya Bavaria. Jiji la Tanga ndilo wanaloishi watu ninaopenda kuwaita “magwiji wa filamu nchini”, kama ambavyo nimewahi kuandika katika makala zangu kadhaa zilizopita.


Kwa nini nawaita watu hawa magwiji wa filamu? Kwa sababu ndiyo watu pekee waliothubutu kuandaa filamu za kibiashara katika miaka ya 1990 japo mazingira yalikuwa magumu sana; wakati huo hakukuwa na mahala pa kuuzia filamu, hata uoneshaji sinema kwenye majumba ya sinema ulikuwa ukisuasua kutokana na kuingia kwa vituo vya televisheni, na sinema zilizotawala nchini zilikuwa za Kihindi.


Ni filamu ya “Shamba Kubwa” (1995) iliyotungwa na kuongozwa na Mwl. Kassim El-Siagi wa Tanga ndiyo iliyofungua milango ya filamu za kibiashara nchini. Kwa walio wengi pengine watanishangaa kwa kuwa hawajahi kuiona filamu hii kwa kuwa wakati ule ilioneshwa kwenye majumba ya sinema; Majestic Cinema – Tanga, Emipre Cinema – Dar es Saalaam, Metropole Cinema – Arusha, na kadhalika.


‘Shamba Kubwa’ ndiyo filamu iliyowaibua wasanii ambao baadaye wamekuwa mahiri katika ulimwengu wa filamu, kama Hassan Master, Jimmy Master, Kaini na Amina Mwinyi, ni filamu hii iliyoteka wengi kwa wakati ule japo teknolojia ilikuwa bado ndogo sana ukilinganisha na hivi sasa.


Filamu hii na nyingine zilizofuata kama ‘Love Story Tanganyika na Unguja (1998)' ya Amri Bawji, ‘Kifo Haramu’ ya Jimmy Master, ‘Dunia Hadaa (2000)' ya Mwl. Kassim El-Siagi, na ‘Augua (2002)' ya Amri Bawji, zote zikitengenezwa na magwiji kutoka Tanga zilitengenezwa katika mfumo wa VHS (analogy), na hata uhariri wake ulitumia akili zaidi kutokana na teknolojia ya wakati huo kuwa ya kiwango kidogo, lakini zilivutia sana kutokana na maudhui na msuko mzuri wa hadithi.


Tanga pia ndiyo mkoa wa kwanza kuanzisha chama ili kukabiliana na changamoto za tasnia ya filamu. Walianzisha Chama cha Watengeneza Filamu wa Tanga (Tanga Film-Makers Association “TAFMA”), wakati huo hata ile filamu ya Girlfriend inayojulikana kwa wengi ilikuwa haijatungwa.

Dec 12, 2011

Filamu za bajeti ndogo

Unataka kuandaa filamu, lakini huna pesa ya kutosha… 

Watengeneza filamu na waandishi wakiwa kwenye semina
iliyoandaliwa na MFDI - Tanzania

TASNIA ya filamu nchini inakua kwa kasi na kuwa kimbilio la vijana wengi, lakini bado tasnia hii imekuwa ikikumbana na changamoto kubwa katika kufikia ubora unaokubalika kimataifa kwenye filamu zetu. Hata wakosoaji wa filamu wamekuwa wakijaribu kukosoa kwa kuilinganisha tasnia hii na tasnia nyingine zilizoendelea kama Hollywood, Bollywood, tasnia ya filamu ya Afrika Kusini na nyinginezo lakini wakasahau kuwa bado tuna mambo makubwa tunayotofautiana.

Katika tasnia za filamu zilizoendelea, mara nyingi huwa zimegawanyika katika mikondo mikuu miwili; mainstream film ambayo pia hujulikana kama major movies studio, na independent film au huitwa kwa kifupi Indies.

Nov 30, 2011

SWAHILIWOOD: Wenzetu wameweza, kwa nini tushindwe?

* MFDI-Tanzania wameanza rasmi mkakati wa mafunzo

Waziri wa Habari, Utamaduni Michezo na Vijana, 
Emmanuel John Nchimbi
 
WIKI iliyopita, kuanzia Jumanne ya tarehe 22 Novemba hadi Jumamosi ya tarehe 26 Novemba, kulikuwa na warsha ya siku tano ambayo ni ya kwanza katika mkakati maalum uliowekwa na taasisi ya Media for Development International – Tanzania (MFDI-Tanzania), kuhakikisha kuwa tasnia ya filamu nchini “Swahiliwood” kama ambavyo wanapenda ijulikane, inafikia kile ambacho tasnia zingine duniani zimeweza, kwa kuandaa warsha iliyohudhuriwa na washiriki 25, wakiwemo watayarishaji wa filamu maarufu na waandishi maarufu wa script.

Warsha hii iliyoandaliwa na MFDI-Tanzania, ambayo mimi nilikuwa mmoja kati ya washiriki waliohudhuria mafunzo maalum ya jinsi ya utafiti na uandishi wa miswada andishi.

Nov 28, 2011

Ili kuboresha filamu zetu tuanze kwanza na script

John Riber

Moja ya semina zilizoandaliwa na MFDI

“MWANAHARAKATI, nimekuwa nafuatili sana makala zako, kuna makala moja ilinigusa sana, hasa pale uliposisitiza kuwa uzuri wa stori yoyote unatokana na msuko mzuri wa matukio, msuko unaohitaji creativity na inspiration. Pia ukasisitiza kwamba unapotunga stori yoyote inayohitaji msuko mzuri wa matukio unahitaji sana 'meditation' na kufanya utafiti wa kina wa kile unachokiandikia...



Kwa kifupi, makala yako imenifanya kuelewa kwa kiasi fulani kuhusu msuko mzuri wa matukio katika stori kwamba ndiyo utakaomfanya mtazamaji wa filamu au msomaji wa hadithi apate hamu ya kuendelea mbele zaidi ili kujua kitakachotokea.

Nov 16, 2011

Hadhi ya Tasnia ya Filamu nchini

 Upigaji picha za filamu Hollywood

Filamu ya Harusi ya Mariam iliyotengenezwa nchini

KUMEKUWEPO mjadala mkubwa kuhusu ukuaji wa soko la filamu hapa nchini na nini kifanyike ili tuweze kutoa filamu nzuri zaidi zenye ubora. Mimi nimekuwa nikitamani kwanza sekta hii ya filamu iwe rasmi kabla ya mambo yote kwa kuwa naamini mitaji, vifaa na rasilimali zipo kila mahali, ila bila kuwa rasmi yote haya tunayoyatarijia hayatawezekana.

Leo nimeamua kuandika mada hii hasa kufuatia mada niliyoandika wiki mbili zilizopita ambapo nilieleza jinsi tasnia yetu ya filamu ilivyopiga hatua katika uzalishaji wa filamu na kuwa ya tatu Barani Afrika (kwa kutoa filamu nyingi bila kujali ubora), ikizifuatia Nigeria inayoongoza na Ghana. Lakini bahati mbaya tuliyonayo ni kwamba mafanikio haya ya kuwa wa tatu katika Afrika hayaendani kabisa na uhalisia wake.

Nov 14, 2011

Kwa nini hatutafuti watunzi wazuri wa stori katika filamu? KULIKONI, NOV 11, 2011

 Hamisi Kibari

 Hussein Tuwa

 Adam Shafi

MAJUZI nilikutana na mdau mmoja wa filamu ambaye tumefahamiana kupitia mtandao wa jamii wa facebook. Katika mazungumzo yetu yaliyochukua takriban saa mbili mdau huyo aliniambia kuwa anapenda sana kusoma makala zangu kwa kuwa anaamini kama zingekuwa zikifanyiwa kazi basi tasnia hii ingefika mbali.

Katika mazungumzo hayo, kikubwa zaidi alitaka kujua kwa nini filamu zetu nyingi zinatumia sana hadithi za kuiga kutoka Nigeria na kwingineko. Aliniambia kuwa kwa uelewa wake anadhani tatizo kubwa lililopo kwenye filamu (nyingi) za Kitanzania ni uwezo mdogo wa uandishi wa hadithi na miongozo ya filamu, kitu ambacho kinasababisha filamu zetu kuonekana hazina muelekeo.

Nov 2, 2011

BONGO MOVIE: Tasnia ya tatu Barani Afrika isiyoendana na uhalisia wake



 Upigaji picha wa filamu ya Mzimu wa Maisara

 Filamu ya Fasta Fasta

IMEKUWA ikisemwa na wadau mbalimbali kuwa Tasnia ya Filamu nchini imekua na kupiga hatua, lakini kwa bahati mbaya kati ya wote wanaosema hivyo hakuna hata mmoja ambaye anaweza kuelezea kwa vitendo zaidi ya kusema tu siku hizi filamu zinatoka kwa wingi, jambo ambalo bado si mwafaka kwa tathmini inayoweza kutumiwa kumshawishi mtu makini aliye nje sekta hii kuingia na kuwa Mwekezaji.

Na imekuwa ikiaminika kuwa sekta ya filamu imeanza kuwa biashara rasmi baada ya mwaka 2002 ambapo ni baada ya filamu ya “Girlfriend” kuingia kwa kishindo na kuwaaminisha Watanzania kuwa kuna Watanzania wanaoweza kupigana vita na filamu kutoka nje ya nchi ambazo kwa kiwango kikubwa zilikuwa zimeshika chati,

Oct 26, 2011

Tusipodhibiti sasa kazi chafu tujue kuwa tunaandaa bomu

 Kazi za utengenezaji sinema kama hizi zinahitaji nidhamu 
na maadili ya taaluma kama ilivyo kwa taaluma nyingine.

TAKRIBANI mwezi mmoja tu kuanzia sasa, nchi yetu itasherehekea miaka hamsini tangu tujipatie uhuru kutoka kwa wakoloni wa Kiingereza. Baada ya uhuru wa Tanganyika serikali katika kuthamini sanaa na utamaduni ilianzisha Wizara ya Utamaduni wa Taifa na Vijana iliyoundwa mwaka 1962, na rais wa Tanganyika na baadaye Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, alitamka wazi kuwa Utamaduni ndiyo kiini na roho ya Taifa.

Katika jitihada zake, nchi yetu ilipata kusifiwa sana kwa jitihada hizo za kushughulikia ukuzaji wa utamaduni katika duru nyingi za kimataifa. Hata hivyo, wakati tukiwa tunajiandaa kusherehekea miaka hii hamsini tangu uhuru, hali ilivyo sasa inatisha na kama hatua za dhati hazitachukuliwa, kazi iliyofanywa miaka ya nyuma, hasa mara baada ya uhuru na miaka takriban 20 iliyofuata, itapotea na tutajikuta tukiwa taifa lisilo na utamaduni wake.

Oct 19, 2011

Filamu zetu na athari zake katika jamii

 Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo
Dk. Emmanuel John Nchimbi

TUKIWA tunaelekea kutimiza miaka 50 tangu tuwe huru, jamii ya Kitanzania imeendelea kupoteza mila na tamaduni zake kila kukicha. Baada ya uhuru wa Tanganyika mwaka 1961, Wizara ya Utamaduni wa Taifa na Vijana iliundwa mwaka 1962, rais wa wakati huo, Mwalimu Julius Nyerere, alitamka wazi kuwa Utamaduni ndiyo kiini na roho ya Taifa, na nchi inayokosa utamaduni wake ni sawa na mkusanyiko wa watu usiokuwa na roho na hivyo kukosa sifa ya kuitwa taifa kamili.

Nalazimika kusema kuwa miaka hii hamsini ya uhuru nchi yetu inashuhudia mmomonyoko mkubwa wa maadili katika jamii huku tasnia ya sanaa/utamaduni ikionekana kutelekezwa kabisa na serikali yetu bila kujali kuwa tasnia hii imesheheni utajiri mkubwa ambao kama ungetiliwa maanani ungeliingizia taifa hili pato kubwa.

Oct 12, 2011

Filamu yaweza kukufanya uishi hata baada ya kifo!

 Susan Lewis (Natasha)

 Marehemu Dalillah Kisinda (Tabia)

 Wakati wa upigaji picha ya Naomi

FILAMU (Movie au Motion pictures) maana yake ni mfululizo wa picha zinazoonesha mwendo wa watu au vitu na kuonekana mbele ya watazamaji kupitia kioo cha seti ya televisheni (screen). Ni aina ya mawasiliano yanayotumiwa kwa ajili ya kuhadithia/ kusimulia au kuwaelezea watu kuhusiana na kujifunza fikra au mitazamo mipya katika jamii.

Watu tofauti katika kila pembe ya dunia huwa wanaangalia filamu ambazo zinasimulia hadithi fulani ikiwa kama kiburudisho, mafunzo au njia mojawapo ya upenzi.

Oct 7, 2011

Ubinafsi huu wa nini kwenye biashara ya filamu?

Kazi ya kurekodi filamu ikiendelea

Anti Ezekiel, mmoja wa wasanii wanaotingisha 
katika soko la filamu nchini

WAKATI tasnia ya filamu nchini ikiendelea kukua, imefahamika kuwa thamani ya kazi za sanaa (filamu) inaendelea kushuka siku hadi siku kutokana na sababu nitakazozieleza baadaye na kusababisha zitengenezwe filamu nyingi zisizo na ubora. Pia kumekuwa hakuna tafiti zinazofanywa kwa maana ya kuweka kumbukumbu (data) zinazowekwa kutusaidia katika kutambua thamani halisi ya tasnia na soko la filamu nchini.

Wadau wengi wa filamu wamekuwa wakiilalamikia serikali kuhusu kutoitilia maanani tasnia hii ambayo ingeweza kuwa suluhisho kubwa la ajira kwa vijana wengi, chanzo cha mapato ya nchi na ambayo ingesaidia kutangaza vivutio vya nchi na hivyo kuvutia watalii wengi na kuliingizia taifa pesa nyingi kupitia utalii.

Sep 28, 2011

Tatizo la usambazaji filamu linasababishwa na makundi

 Kulwa Kikumba (Dude)

Jacqueline Wolper

 Issa Mussa (Claude)

IMEKUWA ni kawaida katika tasnia ya filamu kuwasikia wasanii au watayarishaji wa filamu nchini kuulalamikia mfumo wa soko la filamu uliopo, hasa katika hili sakata linaloendelea hivi sasa kati ya wale walio chini ya Shirikisho la Filamu na Msambazaji mmoja mwenyewe nguvu anayelalamikiwa kuhodhi soko la filamu, ingawa ni haki yake kujipangia mfumo anaodhani utamsaidia kuuza kazi zake kwani hakuna mtu anayefanya biashara kwa ajili ya mtu mwingine.

Jina la kampuni na msambazaji anayelalamikiwa vimekuwa vikitajwa sana kila mara wanapokusanyika wasanii na watayarishaji wengi wa filamu nchini ambao wamekuwa wakiwatupia lawama wasambazaji hao wa kazi zao kwa madai kuwa,

Sep 21, 2011

Chama cha Waongozaji wa Filamu Tanzania wameonesha njia sahihi

Mwenyekiti wa Tafida, Christian Kauzeni, 
katika moja ya majukumu yake kwa chama

Amanzi Ali Kisomi, akiwa jukwaani

INGAWA kimekuwa kikionekana kama ni chama cha watu waliokosa kazi ambao hukutana na kupiga porojo pasipo manufaa yoyote, lakini Chama cha Waongozaji wa Filamu Tanzania (Tafida) kimeonesha njia sahihi kwa kuliangalia tatizo lililopo miongoni mwa wanachama wake katika tasnia hii ya filamu na kuamua kujikosoa wenyewe kabla ya kuwakosoa wengine.

Katika kujikosoa, viongozi wa chama hiki, chini ya uongozaji wa Christian Kauzeni, wameandaa mafunzo maalumu ya siku mbili yanayohusu misingi ya uongozaji yanayofanyika katika ukumbi wa Basata, Ilala Sharif Shamba, Alhamisi na kuhitimishwa Ijumaa,

Basata yataka wasanii wote wajisajili

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili Basata, Angelo Luhala

Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) limewataka wasanii pamoja na vikundi mbalimbali vya sanaa kujisajili ili kukomesha wizi wa kazi zao. Akizungumza katika Jukwaa la Sanaa siku ya Jumatatu, ambalo hufanyika kwa kushirikiana na Chama cha Waandishi wa Habari za Sanaa na Utamaduni (CAJAtz), Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili Basata, Angelo Luhala alisema kwa mujibu wa sheria suala la kujisajili ni la lazima, hivyo akasema wasanii wote wanatakiwa kupewa vibali ili waweze kutambulika mahali popote wanapokwenda.

Luhala alisema kuwa wasanii wengi hulalamika kuibiwa kwa kazi zao, pasipo kujua aliyehusika na wizi huo, hivyo usajili ni moja ya kanuni za nchi, kwani taifa linakuwa na kumbukumbu kuhusu kazi zao na pia inamsaidia msanii mwenyewe kuwa huru na kufanya kazi yake kwa imani.

Sep 20, 2011

IJUE BODI YA FILAMU TANZANIA

 Nembo ya Tanzania

 Rose S. Sayore, Mwenyekiti wa Bodi ya Filamu

Merybeatrix Mugishagwe, Mjumbe wa Bodi

HISTORIA YA BODI YA UKAGUZI WA FILAMU TANZANIA

Historia ya bodi ya Filamu nchini Tanzania inaanzia kipindi cha utawala wa kikoloni ambapo mwaka 1930 Sheria ya Picha za Sinema ilitungwa na kuanza kutumika. Mnamo mwaka 1974 Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania lilitunga namba 4 Sheria ya Filamu na Michezo ya Kuigiza na mnamo mwaka 1976 na sheria hiyo ilisainiwa na rais wa wakati huo Mwalimu Julius K. Nyerere.Sheria ambayo ina tumiaka mpaka sasa. Majukumu ya Bodi ni kulinda Utamaduni kwa kuhakikisha kuwa sanaa ya filamu na michezo ya kuigiza inazingatia maadili ya Taifa.

Sep 16, 2011

Tasnia ya filamu nchini ni kama shamba la bibi

 Mwanaharakati wa sanaa nchini, John Kitime

HUWA napata wakati mzuri sana pale ninapopata nafasi ya kukutana na kuwa katika mazungumzo na wadau muhimu wa sanaa hapa nchini na tasnia ya burudani kwa ujumla, na mmoja wao ni mwanaharakati wa sanaa na mtu aliyebobea katika masuala ya hakimiliki nchini, John Kitime, ambaye pia amekuwa akijitolea muda wake mwingi kujaribu kuelimisha wadau wengine kuhusu haki zao na mambo mbalimbali yanayoendelea katika tasnia ya sanaa, jambo ambalo ni nadra sana kufanywa na wengine.

Namheshimu sana Kitime kwa mchango wake na heshima yangu si ile ya kinafiki kama ilivyo kawaida ya Watanzania wengi kutothamini mchango wa mtu anapokuwa angali hai, na husubiri pale anapoaga dunia ndipo hujidai wanamfahamu sana na kumwagia sifa kemkem japo ni haohao waliokuwa wakimponda wakati wa uhai wake.

Sep 14, 2011

Kanisa laipotezea ndoa ya Joyce Kiria



 Ndoa ya kwanza ya Joyce kiria na DJ Nelly


Ndoa ya sasa na Henry Kilewo

Mbunge wa Ubungo John Mnyika pia alikuwepo

Zikiwa zimekatika siku kadhaa toka kufungwa kwa ndoa kati ya presenter wa Kipindi cha Bongo Movies kupitia runinga ya EATV, Joyce Kiria na Katibu wa Chadema Wilaya ya Kinondoni, Henry John Kilewo, Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) kupitia mchungaji wake mmoja (jina limehifadhiwa), limesema ndoa hiyo haitambuliki.

Akizungumza na gazeti moja Jumatano iliyopita jijini Dar, mchungaji huyo alisema kuwa, ndoa ya Joyce inayotambulika ni ile iliyofungwa Desemba 16, 2008 katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheli la Kijitonyama, jijini Dar es Salaam ambako nakala ya cheti  cha ndoa yake imehifadhiwa.

Sep 8, 2011

Ujasiriamali sekta ya filamu umedhoofishwa makusudi...

Hamisi Kibari 



UJASIRIAMALI ni uwezo na nia ya mtu au watu kufikiria, kubuni na kuanzisha fursa mpya za kiuchumi/uzalishaji na kuingia kwenye soko bila kuogopa ushindani au vikwazo vilivyopo au vitakavyoweza kutokea. Mjasiriamali ni mtu mwenye moyo wa kuthubutu, mbunifu, mwerevu wa kubaini na kutumia fursa mbalimbali za kiuchumi, mpenda ufanisi na viwango bora katika kazi ya Sanaa, asiye na tabia ya kuvuruga na kuvunja taratibu za makubaliano na mikataba.

Pia mjasiriamali anasemwa kuwa ni mtu mpenda kutafuta na kupata habari mbalimbali, anayeweka malengo, mwenye kuweka mipango na kufuatilia, asiye tegemezi na anayeamini, na mwenye uwezo wa kushawishi na kuwa na mtandao.

Sep 6, 2011

Marehemu Tabia wa Kidedea afufuliwa

 Marehemu Dalillah Peter Kisinda ‘Tabia’

Pamoja na kutangulia mbele za haki mwanzoni mwa mwaka huu, Watanzania watapata fursa ya kuona vimbwanga vya aliyekuwa mwigizaji mkubwa Bongo, marehemu Dalillah Peter Kisinda ‘Tabia’ katika muvi yake ya mwisho ya Naomi inayokimbiza sokoni.

Kwa mujibu wa mtayarishaji wa filamu hiyo, Hamis Kibari, watakaoitazama muvi hiyo watagundua kwamba Tabia aliyevuma na Kundi la Kidedea alikuwa hazina kubwa ya uigizaji Bongo kwa jinsi alivyomudu vizuri nafasi yake.

Aug 29, 2011

NAOMI: Filamu ya mwisho ya marehemu Tabia

Marehemu Dalillah Peter Kisinda (Tabia)

 Kava la filamu ya Naomi (part 2)

TASNIA ya filamu nchini mwetu imezidi kukua na kuendelea kuua soko la filamu kutoka Nigeria ambazo mwanzoni mwa miaka ya 2000 zilikuwa zimeliteka soko la nchi yetu. Tofauti na ilivyokuwa miaka michache iliyopita, kwa sasa takriban, filamu mbili mpya za Kitanzania hutoka kila wiki na hali inaonesha kwamba idadi hiyo itazidi kupanda miaka michache ijayo, hasa kama watengeneza filamu wa Tanzania wataboresha zaidi kazi zao.

Moja ya filamu inayosubiriwa kwa hamu ni ya Naomi, iliyotayarishwa na mmoja wa Watunzi mahiri wa hadithi nchini na mtengeneza filamu, Hamisi Kibari.