Mar 29, 2018

Nchi za SADC na mkakati wa sanaa kwa maendeleo

Ramani inayoonesha nchi za SADC



MAPEMA Machi mwaka huu kuliandaliwa Tamasha la Kusherehekea Wanawake wa SADC Katika Sanaa ya Maigizo na Dansi lililofanyika mjini Johannesburg.

Wanawake wa Zambia katika kikundi cha dansi walitumia michezo ya maigizo kwa ajili ya maendeleo kwa kuhamasisha wanakijiji kupanda zaidi ya miti 5,000 na kujenga majengo matatu ya madarasa kwa kipindi cha miaka mitatu katika Jimbo la Kusini mwa Zambia.

Tamasha hilo liliandaliwa na "Southern Africa Theatre Initiatives (SATI)" na lilikuwa na lengo la kuonesha jukumu la wanasanaa wanawake wa nchi za SADC kuungana na kuleta mabadiliko katika kanda.

“Wanasanaa wanawake wanapuuzwa pamoja na kazi kubwa wanayofanya kuunganisha na kuendeleza jumuiya. Wanachohitaji ni kutambua na kupatiwa msaada tu,” alisema Mpo Molepo, katibu wa SATI.

Filamu ya Gifted Hands: Inaonesha jinsi maisha yako yanavyoweza kuwa somo kwa wengine

Filamu ya Gifted Hands
KILA mmoja ana ndoto zake katika maisha yake. Wengine wana ndoto kubwa za kubadilisha ulimwengu huu, huku wengine wakiwa na ndoto za kuishi maisha ya kupata mahitaji yao ya msingi tu.

Lakini wote hawa wanahitaji kuzitimiza ndoto zao; ila katika safari ya kutimiza ndoto hizi kuna vikwazo na mambo mbalimbali ambayo huwazuia watu wasiziishi ndoto zao na kuishia kulaumu na kulalamika, hasa uzeeni.

Wewe je, una ndoto? Je, ndoto yako ni ya namna gani? Je, umewahi kujiuliza kwamba ufanye nini uweze kuitimiza ndoto yako?

Mar 24, 2018

Tuwe macho, hii ni vita ya utamaduni



MIAKA kadhaa iliyopita niliwasiliana na kampuni ya Sony Pictures yenye makao yake Los Angeles (Culver City) nchini Marekani. Hii ni kampuni kubwa Hollywood ya burudani iliyoanzishwa Agosti 7, 1991 baada ya kujitenga kutoka kampuni ya Columbia Pictures Entertainment.

Kampuni hii inafahamika kwa filamu za The Karate Kid, Ghostbusters, Spider-Man, Men in Black, Underworld, Robert Langdon, The Smurfs, Sniper na nyingine nyingi. Niliwasiliana na Sony Pictures nikiwaomba watafute njia ya kudhibiti filamu za Hollywood zinazorudufiwa kiharamia na kusambaa kila kona ya Afrika Mashariki.

Mar 16, 2018

Zi wapi zama za vikundi vya sanaa?

Kikundi cha Sanaa cha TaSUBa wakifanya vitu jukwaani


DAH! Ama kweli siku hazigandi na maisha hayarudi nyuma! Maisha yakipita yamepita, japo historia ndiyo inayoweza kuturudisha nyuma tupendavyo. Enzi za uongozi wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na baadaye Ali Hassan Mwinyi kulikuwa na vikundi vingi vya sanaa, hasa vya sarakasi, maigizo, ngoma, mazingaombwe na kadhalika.

Vikundi hivi vilitoa burudani ya aina yake katika jamii husika, na watu walikuwa wakienda kwenye kumbi mbalimbali, hasa jijini Dar es Salaam na miji mikubwa mwisho wa wiki kupata burudani ya aina yake.

Nakumbuka kulikuwa na vikundi vya sanaa vya DDC Kibisa, Muungano Culture Troup, Makutano Dancing Troup, Ujamaa Ngoma Troup, Mandela Theatre, Bima Modern Taarab, Super Fanaka, Reli Kiboko Yao, JWTZ, Tancut Almasi, UDA, Urafiki n.k.

Mar 15, 2018

The Theory of Everything na maisha ya Prof Hawking

Prof Stephen Hawking enzi za uhai wake

Filamu ya The Theory of Everything
NILIWAHI kusoma riwaya ya Dunia Uwanja wa Fujo iliyoandikwa na Profesa Euphrase Kezilahabi, inayoonesha maisha yaliyopo duniani ni sawasawa na fujo, kwani kila mtu anayekuja duniani huleta fujo zake na baadaye kutoweka.

Fujo hizo zimekuwa zikitofautiana, wapo waliofanya fujo kwa jina la amani, waliofanya fujo kwa kutumia nguvu na wengine wamefanya fujo za kimaandishi, fujo ambazo hazitafutika hadi dunia inafutika…

Nimejikuta nikiikumbuka riwaya hii baada kutafakari kuhusu maisha ya Prof Stephen Hawking, mwanafizikia maarufu duniani aliyefariki dunia jana Jumatano Machi 14, 2018 akiwa na miaka 76.

Mar 12, 2018

Mapokeo ya kazi za sanaa yanavyotuathiri



INGAWA Tanzania kuna zaidi ya makabila 120 na lugha 128 zinazotumika, Watanzania tumeweza kubaki kama tulivyo, Watanzania. Popote pale Mtanzania atakapokwenda atajiita  Mtanzania, akiulizwa zaidi ya hapo, anaweza akataja kabila yake. Ila, Watanzania hupenda zaidi kuwa Watanzania. Ndiyo utamaduni wetu.

Kinachoonekana sasa ni Watanzania kutaka kugawanyika kwa misingi ya kidini, hasa kati ya Wakristo na Waislamu, japo wameishi pamoja vizuri tangu uhuru.

Pamoja na hayo, Sera ya Ujamaa na lugha ya Kiswahili zimechangia sana kutufanya kuwa wamoja. Rangi, ladha, urafiki na uchangamfu ndiyo viungo muhimu vya utamaduni wa Tanzania.

Mar 7, 2018

Filamu ya The Silent Child: Somo kubwa kwa tunaodhani ‘hawawezi’




MARA nyingi nimewashauri wasanii wa Tanzania kutengeneza filamu fupi, kwani soko lake limejengwa katika misingi imara, haliangalii majina ya watu bali misingi na weledi.

Soko kubwa la filamu hizi lipo kwenye matamasha ya filamu ya kimataifa, kwani matamasha ya filamu ni sehemu nzuri zaidi ya kutengeneza mtandao na kumfanya mtengenezaji kujulikana kimataifa.

Naam… sanaa ya filamu ni kitu cha ajabu sana. Si kila mtu anaweza kuipenda kazi yako. Ila unachotakiwa ni kusimamia ndoto yako pasipo kukata tamaa. Hasa ukiwa na script nzuri na mipango sahihi.

Mar 3, 2018

Black Panther inapowasuta wazungu kuhusu Afrika



TANGU filamu ya Black Panther itoke, kwa kweli imenifikirisha sana kwa jinsi ilivyojaribu kuiweka Afrika katika nafasi chanya, ikiionesha Wakanda (Afrika) kuwa nchi bora sana.
Kwa jinsi Wakanda ilivyoonekana, maana yake ni kuwa kama Afrika isingetawaliwa na wakoloni na kuachwa kukua yenyewe, ingekuwa mbali sana.

Ukiangalia filamu nyingi za watu weusi, mazingira ya Afrika yanaonekana kuwa ni mabaya sana na machafu, lakini tofauti katika filamu hii, nchi ya kufikirika ya Wakanda ina teknolojia za hali ya juu kuliko hata nchi kubwa za ulaya na Marekani.

Filamu ya Watu Wote ni somo kwa Bongo Movies


JUZI nilipata nafasi ya kujadili jambo na Mpigapicha mkuu wa gazeti la HabariLeo, Fadhili Akida, ambaye alionesha nia ya kutaka kutengeneza filamu fupi, ingawa hakujua soko lake likoje.

Tulijikuta tukiwa katika mazungumzo hayo baada ya mchambuzi maarufu wa filamu nchini, ambaye pia ni mhariri wa uzalishaji wa gazeti la HabariLeo, Beda Msimbe, kuibua hoja kuhusu filamu fupi.

Wakati nikiongea na Fadhili, nilijaribu kumweleza uzoefu wangu kuhusu tasnia ya filamu na kile ninachojua kuhusu sekta hii na soko la filamu fupi. Ni mara nyingi nimekuwa nikiwashauri wasanii wetu kuligeukia soko la filamu fupi, kwani soko hili limejengwa katika misingi imara, kwani haliangalii majina ya watu bali misingi na weledi.