Jun 22, 2016

Kipindi cha XYZ cha Kenya kumilikiwa na Trace TV


Kipindi hiki kinachohitajika sana kimekuwa kikiimarika katika bara Afrika. Mapema mwaka huu kulikuwa na uzinduzi wa Netflix katika soko la Afrika, hatua iliyofurahisha wateja wengi. Hatua hii inajiri wakati ambapo Showmax cha Afrika Kusini kinatarajiwa kuingia katika soko la Kenya. Mipango mengine ni ile ya ushirikiano wa kati ya Airtel na Ericsson kuzindua huduma kwa jina NUVU.

Jun 8, 2016

Mgogoro TAFF ni vita vya panzi, furaha kwa kunguru

Kutoka kushoto; Katibu Mtendaji wa BASATA Godfrey Mungereza, Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Joyce Fisoo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel, na Rais wa TAFF Simon Mwakifwamba. Hii ilikuwa ni siku ya uzinduzi wa Tuzo za TAFA

NIKIWA sijui hili wala lile hivi karibuni nilijikuta natumiwa ujumbe wa WhatsApp kwenye simu yangu kutoka kwa mdau mmoja wa filamu. Ujumbe ambao nilipoutazama kwa makini nikagundua kuwa haukuwa umeandikwa na mdau aliyenitumia bali ama alitumiwa au aliukopi kutoka kwa mdau mwingine.

Ujumbe huu uliandikwa hivi: “Habari? Mungu hulipa hapa hapa, tulimpakazia Bishop kila aina ya hila kulinda mambo yetu lakini tukajiona washindi bila kujua dhambi kubwa tuitendayo itatuhukumu tulipo. Kwa tatizo hili la Tanzanite film festival, Katibu tena atang’oka? Nasubiri muujiza. Hongera sana ndugu yangu Bishop, dhuluma uliyofanyiwa inawahukumu.”