Jul 29, 2015

TAMASHA LA 18 LA ZIFF: Tutumie fursa kama hizi kwa ajili ya kujitangaza na kujifunza zaidi

Mkongwe, Dorothy Masuka, akiwa jukwaani katika shoo yake usiku wa Julai 19, katika tamasha la 18, la ZIFF 2015,Ngome Kongwe upande wa Mambo Club

MATAMASHA ya filamu duniani ni sehemu nzuri zaidi kwa ajili ya kutengeneza mtandao na kumfanya mtengenezaji wa filamu au msanii kujulikana si tu katika kanda husika bali kimataifa.

Mkurugenzi wa ZIFF, Prof. Martin Mhando
Ukibahatika kuwa mmoja wa washindi wa tuzo, unakuwa kwenye nafasi nzuri zaidi ya kujitangaza na hata kupata msaada wa kipesa (funds) kwa ajili ya kutengeneza sinema bora zaidi unayohitaji siku zote kwa kuwa utaingia kwenye orodha ya watu wanaoaminiwa, na hapo ndo’ washindi hujua kuwa wapo katika mstari sahihi.

Jul 22, 2015

Kukua kwa sekta ya filamu Tanzania kutakuza utalii

Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu akiwa na muigizaji
Anti Ezekiel, siku walipotembelea Marekani kutangaza utalii

SEKTA ya Filamu nchini ikiendelezwa vizuri ni chanzo kikubwa cha ajira kwa vijana, njia madhubuti ya kukuza utalii na uchumi wa Taifa na wa wananchi kwa ujumla. Sekta ya Filamu (kwa kuzingatia kuwa ni sehemu ya habari “media”) inapotumika vizuri, hufanya kazi kama mhimili huru unaosimamia dola.

Katika nchi ambayo Bunge linakosa meno dhidi ya udhaifu wa serikali, vyombo vya habari navyo vikawa kimya, sekta hii inaweza kuwa nyenzo imara zaidi ya kuwasiliana na jamii na kuieleza jinsi mambo yasivyo sawa. Lakini pia sekta hii ina nguvu kubwa kiutamaduni, na chanzo kizuri cha kupashana taarifa.

Jul 20, 2015

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuiunga mkono ZIFF

Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kuunga mkono  juhudi zinazochukuliwa na Uongozi wa Tamasha la Kimataifa la Filamu la Nchi za Jahazi  Zanzibar (ZIFF) katika azma yake ya kuijengea nguvu tasnia ya Filamu Nchini inayoonekana kusaidia ukuaji wa uchumi kupitia sekta ya Utalii.

Kauli hiyo imetolewa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein, katika Hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi, wakati  akilizindua Tamasha la 18 la Kimataifa la Filamu la Nchi za Jahazi Zanzibar (ZIFF) hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa Hoteli ya Double Tree By Hilton Shangani Mjini Zanzibar.

Jul 18, 2015

Buhari kuipiga jeki sekta ya filamu NIgeria

Rais wa Nigeria, Muhammadu Buhari

Rais mpya wa Nigeria, Muhammadu Buhari, ameendeleza kile kilichoanzishwa na mtangulizi wake, Goodluck Jonathan, katika kusaidia sekta ya filamu kwa kuapa kuhakikisha anasaidia sekta ya filamu nchini humo kutoanguka kutokana na uharamia wa kazi.

Alisema kuwa sekta ya filamu ya Nollywood inafanya vizuri ila inaweza kuathiriwa na uharamia. Sekta hii ina thamani ya dola bilioni 5 (sawa na paundi bilioni 3), lakini watengeneza filamu bado wanasota kutengeneza faida  kwa sababu ya uharamia.

Jul 14, 2015

Benson Wanjau Karira (Mzee Ojwang Hatari) afariki dunia

Benson Wanjau Karira maarufu kama Mzee Ojwang Hatari

Muigizaji mkongwe wa vichekesho nchini Kenya, Benson Wanjau Karira maarufu kama Mzee Ojwang Hatari, amefariki dunia siku ya Jumapili usiku katika Hospitali ya Taifa ya Kenyatta alipokuwa amelazwa.

Mzee Ojwang wakati akichukuliwa vipimo vya macho

Mzee Ojwang alikuwa amelazwa katika hospitali hiyo akisumbuliwa na maradhi ya homa ya mapafu (Pneumonia). Muigizaji huyo ambaye alikuwa kinara katika vipindi vya Vitimbi, Vioja Mahakamanii, Vituko na Kinyonga, pamoja na kazi nyingine, alikuwa hajaonekana kwenye televisheni kwa muda mrefu.

Jul 7, 2015

Mabanda ya Video: Tutazame upande wa pili wa shilingi

Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Bi. Joyce Fissoo

Mjumbe wa Bodi ya Filamu, Dk. Vicensia Shule (kushoto), akizungumza katika kikao na wafanyakazi wa kampuni ya usambazaji ya Proin Promotion. Katikati ni Bishop Hiluka na kulia ni Mzee Silvester Sengerema (Kaimu Mwenyekiti Bodi ya Filamu)

INGAWA nchini Tanzania televisheni imekuwapo tangu mwaka 1973 (Zanzibar), Tanzania Bara televisheni imeanza mwanzoni mwa miaka ya 1990. Hadi 1996 kulikuwa na vituo vitatu tu vya televisheni: CTN, DTV na ITV. Kupingwa kwa televisheni Tanzania Bara na kuwapo kwa Radio moja (RTD) tokea miaka ya baada ya uhuru ulikuwa mkakati wa serikali kujenga utamaduni wa Umoja, Udugu na Utanzania.

Enzi hizo (nilikuwa bado mdogo) watu walikuwa wanakwenda kwenye majumba maalum ya sinema kuangalia sinema kwa wakati maalum na masharti maalum. Majumba haya yalikuwepo katika kila mji-makao makuu ya mkoa na baadaye katika wilaya, na idadi yake ilitegemea ukubwa wa mji.

Jul 1, 2015

Filamu zinaweza kutumika kama tiba

·         Lakini pia zinaweza kuacha athari ya kisaikolojia

Wapenzi wa sinema wakisubiri kuangalia sinema katika moja ya
maonesho ya sinema kwenye viwanja vya Tangamano, jijini Tanga
TUPENDE tusipende, nyakati hizi za karne ya 21 tunalazimika kutumia vyombo mbalimbali vya mawasiliano, kama magazeti, simu, redio, vinasa sauti, televisheni, filamu, mtandao, n.k. Vyombo hivi vimechangia kwa kiasi kikubwa sana katika kuifanya dunia yetu kuwa ndogo sana. Tunaweza kuvitumia vyombo hivi kwa ajili ya kujielimisha na kujiburudisha ingawa kwa walio wengi, maendeleo ya vyombo hivi ni kama kitendawili. Kila wakati vyombo hivi vinakuwa vya teknolojia mpya na vya rahisi kutumia.