Jacklin Wolper akiwa na tuzo yake
KATIKA wasanii mastaa ambao wangepaswa kuishi maisha mazuri nchini kwa sasa, ni wale wa filamu ndio wangepaswa kuwa wanashikilia chati za juu kutokana na jinsi kazi zao zinavyotengeneza fedha nyingi. Kwa mujibu wa takwimu, kazi za wasanii hao zimekuwa zikiingiza fedha nyingi katika miaka ya karibuni tofauti na ilivyokuwa awali, lakini masilahi hayo hutofautiana kwani wapo baadhi ambao hawashikiki.
Wasanii wa filamu wamejijengea majina maakubwa kwenye jamii ya wapenzi wa filamu kufikia kiwango ambacho bila wao kazi hazinunuliki madukani na baadhi ya waandaaji wa filamu hizi wamekuwa wakieleza waziwazi kuwa wengine hata kutokea sura zao tu kwenye sinema ni biashara tosha hata kama wameigiza upuuzi!