Jul 18, 2012

Tasnia ya filamu Tanzania: Tumetokea wapi na tunaelekea wapi?

 Jacklin Wolper akiwa na tuzo yake

KATIKA wasanii mastaa ambao wangepaswa kuishi maisha mazuri nchini kwa sasa, ni wale wa filamu ndio wangepaswa kuwa wanashikilia chati za juu kutokana na jinsi kazi zao zinavyotengeneza fedha nyingi. Kwa mujibu wa takwimu, kazi za wasanii hao zimekuwa zikiingiza fedha nyingi katika miaka ya karibuni tofauti na ilivyokuwa awali, lakini masilahi hayo hutofautiana kwani wapo baadhi ambao hawashikiki.

Wasanii wa filamu wamejijengea majina maakubwa kwenye jamii ya wapenzi wa filamu kufikia kiwango ambacho bila wao kazi hazinunuliki madukani na baadhi ya waandaaji wa filamu hizi wamekuwa wakieleza waziwazi kuwa wengine hata kutokea sura zao tu kwenye sinema ni biashara tosha hata kama wameigiza upuuzi!

Jul 4, 2012

Tupige vita matumizi ya lugha za kigeni kwenye filamu zetu

 Sinema nyingi za Tanzania zimeingia kwenye mkumbo wa kutumia majina ya kigeni

KIPINDI fulani niliwahi kuandika kuhusu suala la mila na utamaduni wa Mtanzania ambapo kwa kiasi kikubwa lilikuwa likinitatiza sana. Nilikuwa nikifikiria sana; tunaposema utamaduni na mila za Watanzania hasa tunamaanisha nini kwa Tanzania yenye zaidi ya makabila 120 ambayo kila moja lina mila na utamaduni wake? Huu utamaduni na mila za Watanzania ni upi hasa?

Haya ni maswali yaliyonitesa kila mara nilipokuwa nikiufikiria utamaduni wa Mtanzania. Lakini baada ya kufanya utafiti niligundua kuwa, neno “utamaduni” linatumika kimsingi katika njia tatu zifuatazo:

Jul 2, 2012

Wasanii maarufu wamepamba tamasha la filamu Tanga

Umati wa watu waliohudhuria tamasha la filamu jijini Tanga

Sehemu ya wasanii nyota katika tamasha hilo

Nyota  mbalimbali wa filamu nchini, akiwemo Wema Sepetu, Jacqueline Wolper, Irene Uwoya, Jacob Steven 'JB' na Vicent Kigosi 'Ray' kwa mara ya kwanza wamepanda kwenye jukwaa moja la tamasha la filamu linalofanyika jijini Tanga lililoanza Jumamosi hadi Julai 6 mwaka huu.

Katika tamasha hilo kumekuwa na burudani mbalimbali kutoka kwa wasanii wa Tanga wanaoimba ngoma za asili kama baikoko, mdumange na msanga.