Aug 26, 2015

Je, tunaweka mipaka kwa watoto kutazama televisheni/filamu?

Watoto wanaangalia televisheni

MAJUZI jirani yangu mmoja (ambaye amenunua kisimbuzi hivi karibuni) aliniita nyumbani kwake na kuniomba nimsaidie kuweka namba za siri (password) kwenye baadhi ya chaneli za televisheni yake ili kuwadhibiti watoto wake wasiweze kuangalia sinema na vipindi visivyo na maadili. Aliamua kufanya hivyo baada ya kugundua uwepo wa chaneli zinazoonesha mambo yenye ukakasi.

Kwa sasa ni jambo la kawaida sana kwa watoto wengi kutazama filamu, televisheni, video, kucheza michezo (games) ya kompyuta, na kutumia Intaneti. Kulingana na makadirio fulani, watoto na vijana hutazama na kuvitumia vyombo vya habari kati ya mara 20 au 30 zaidi ya wakati wanaotumia kufanya mambo na familia zao. Jambo hilo huwafanya watoto wapate habari nyingi zenye kudhuru.

Aug 12, 2015

Uchaguzi 2015: Hivi Wasanii wamebeba ajenda gani?

* Waepuke kuendelea kutumiwa kisiasa
Msanii maaruf wa filamu, Jacob Steven (JB) akiwa kaongozana na
Rais Jakaya Kikwete, Katibu Mkuu wa CCM, Abrahman Kinana,
mgombea urais kupitia CCM, John Magufuli na viongozi wengine,
siku wasanii walipofanya sherehe kumuaga Rais Kikwete katika
Ukumbi wa Mlimani City

“TUMEPATA mafanikio ya kuridhisha kwa upande wa sanaa za filamu na muziki. Vijana wetu wa tasnia hizi wamekuwa wanafanya vizuri kiasi kwamba leo hii Bongo Flavor na Bongo Movie zimevuka mipaka ya Tanzania. Zinaitangaza sanaa ya Tanzania, lugha ya Kiswahili pamoja na nchi yetu. Vijana hawa wameitoa kimasomaso Tanzania na kutufutia unyonge tunaopata kwenye michezo. Tasnia hizi zimeajiri vijana wengi, wanalipa kodi na wanasaidia sana katika kuhamasisha na kufikisha ujumbe kwa mambo muhimu katika jamii.”