Sep 14, 2012

Tanzania na nchi za SADC bado zina nafasi ya kufanya vizuri


Wakati wa upigaji wa sinema ya Tsotsi, nje ya jiji la Johannesburg

NCHI za kusini mwa Afrika zina nafasi kubwa ya kutoa mchango katika tasnia ya filamu na televisheni duniani. Kumekuwepo makubaliano miongoni mwa wadau na wachunguzi wa tasnia hii, kwamba, utajiri uliopo wa ubunifu miongoni mwa vijana na hadithi zilizopo katika ukanda huu vitumike vyema. Hata hivyo, pia wote wanakubaliana kwamba tasnia ya filamu katika nchi hizi bado iko chini sana na, katika hali halisi, inazidi kushuka.

Utafiti unaonesha kuwa tasnia ya filamu ya nchi za SADC ni ndogo na haijapiga hatua, ingawa inaonekana kutoa fursa nyingi katika kuendeleza miundombinu na hadithi zetu. Makampuni mengi katika sekta hii ni madogo madogo na yanayoonekana kuchangia katika ajira na ukuaji wa uchumi.