Sep 13, 2014

Unachokiandika kinakutafsiri ulivyo


 
IMEANDIKWA, “Kila siri iliyo moyoni kwa mwandishi, kila aina ya maisha aliyoyapitia, au kipimo cha akili ya mwandishi vimeainishwa kwa kiasi kikubwa katika maandishi yake...” hii inamaanisha kuwa kazi za kimaandishi za waandishi huwaonesha wao ni kina nani, wametokea mazingira gani, wana uwezo gani wa kufikiri na wanataka kuwa nani.

Kupitia kujielewa wenyewe na kuridhika katika uasili wetu, mchakato wa kuandika huwa unakuwa wa hiari zaidi na hauzuiliki. Tunapoelewa kuwa tuna talanta (kipaji) ya kipekee ya uandishi tuliyotunukiwa na Mungu, inatusaidia zaidi katika kuandaa makala au hadithi nzuri.