May 27, 2015

Wasanii wanapokubali kutumika kisiasa!

Bishop Hiluka, Simon Mwakifwamba na Michael Sangu
wakati wa harakati za kupigania ukombozi wa msanii
HISTORIA huwa haina haja na wale wote wenye kushindwa, labda tu kunukuu tarehe walizokutwa na umauti wao... Sekta ya filamu Tanzania ambayo ilionekana kupiga hatua siku hadi siku, siku za karibuni imeonekana kuanza kudorora. Ipo chumba cha wagonjwa mahututi (ICU).

Ni ukweli usiopingika, sekta ya filamu ipo chumba cha wagonjwa mahututi ikisubiri kupelekwa mochwari, hasa kama hatua za makusudi hazitachukuliwa kunusuru hali hii, hali ambayo kwangu ni kama mazingaombwe.

May 13, 2015

Kuna nini Sekta ya Utamaduni?

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, 
Dk. Fenella Mukangara
MUUNDO wa uendeshaji wa sekta au shughuli yoyote hutokana na azma ya kushughulikia matatizo yaliyopo. Muundo huo huwa ni nyenzo ya awali kabisa ya kutatua matatizo hayo. Kwa hiyo idara na sehemu zinazoundwa katika asasi na aina ya wataalamu wanaoajiriwa huzingatia majukumu na kazi za asasi ile katika muhula husika.

Ingawa Sekta ya Utamaduni imekuwa katika mfumo wa serikali tangu 1962, nafasi yake katika maendeleo ya taifa bado haijatambuliwa kikamilifu. Mipango ya Maendeleo imekuwa ikibuniwa na kutekelezwa bila kujali utamaduni wa wananchi, utamaduni haupewi dhima katika uamuzi na mipango ya maendeleo kwa sababu inaaminika kuwa maendeleo ni kuondokana na mambo ya kiasili pasipo kuchunguza misingi ya mambo hayo na faida zake.

May 6, 2015

SEKTA YA FILAMU: Kenya inapiga hatua wakati sisi tunasinzia

Gavana wa Kaunti ya Machakosi, Alfred Mutua
SEKTA ya Filamu nchini Kenya imetajwa kama sekta muhimu sana katika ujenzi wa uchumi wa nchi hiyo, hasa katika kuvutia watalii na kutoa nafasi za ajira kwa vijana wa Kenya. Lakini sekta hiyo kwa muda mrefu imekosa wafadhili wa kuiwezesha kufikia kiwango hicho na kuendelea kubaki nyuma huku sekta zingine kama utalii zikinawiri.

Sasa sekta hii imeanza kupiga hatua kubwa baada ya kupigwa jeki na hazina ya vijana nchini humo, ambayo ilitenga kiasi cha shilingi milioni 300, ili zitumiwe na vijana kwa njia ya mikopo katika kuijenga sekta hiyo na kuiimarisha nchini kote. Kwa miaka sasa sekta hii ya filamu nchini Kenya imekuwa iking'ang'ana kujikita, lakini isiwezekane.