Oct 23, 2017

Wasanii vunjeni ukuta wa fikra

Peter Tosh
Filamu ya Off Side
“EVERYBODY want to go to heaven, but nobody want to die…” hii ni nukuu kutoka kwenye wimbo wa Equal Rights wa aliyekuwa mwanamuziki mahiri wa reggae duniani, Peter Tosh. Maneno hayo ambayo tafsiri yake kwa lugha ya Kiswahili ni “Kila mtu anataka kwenda peponi, lakini hakuna anayetaka kufa…”

Sikuwa shabiki wa muziki wa reggae, ila nilipolazimika kusikiliza reggae nilipenda nyimbo za Lucky Dube na Peter Tosh. Wanamuziki wote wawili kwa sasa ni marehemu.

Ukiusikiliza kwa makini ujumbe ndani ya wimbo wa Equal Rights, utagundua kuwa ni chemsha bongo ya aina fulani. Maneno ya Peter Tosh katika wimbo huu yanaakisi hali halisi ilivyo katika shughuli za sanaa Tanzania, hasa muziki na filamu.

Muziki wa Singeli: ni mapinduzi mapya au kifo cha muziki?

Mwanamuziki Msaga Sumu

Mwanamuziki Sholo Mwamba
MUZIKI wa Tanzania unabadilika sana, wasanii wengi wamekuwa wakibuni mitindo ya aina mbalimbali ili kuzifanya kazi zao ziende mbali na kuvuta mashabiki wa muziki nchini na duniani kwa ujumla.

Miaka ya nyuma muziki wa dansi ndiyo ulikuwa ulishika hatamu, muziki huu ulioanza kama klabu ambapo watu walialikana kucheza aina mbalimbali za muziki wa kizungu mtindo maarufu uliojulikana kama ballroom dancing. Kisha taratibu ukaumbika ukifuata muziki wa soukous kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (rumba ya Kikongo) na tokea hapo ikawa inaitwa ‘rumba ya Tanzania’.

Oct 14, 2017

Miaka 18 baada ya kifo cha Mwalimu Julius K. Nyerere: Je, tunalinda utamaduni wetu kama alivyoamini?


LEO tunaadhimisha kumbukumbu ya miaka 18 tangu Baba wa Taifa na muasisi wa taifa hili, Rais wa kwanza wa Tanzania, Hayati Mwalimu Julius Nyerere aliyefariki dunia Oktoba 14, 1999 jijini London, Uingereza na kuzikwa Butiama, kijiji alichozaliwa.

Mwalimu Nyerere alikuwa kati ya viongozi wachache wa Afrika walioacha mwangwi katika utamaduni wa nchi zao.

Nyerere alikuwa mwalimu. Ni sahihi kusema silika ya ualimu iliathiri siasa na matendo ya Mwalimu Nyerere kama kiongozi wa Tanganyika na baadaye Tanzania. Aliiona nchi yake kama darasa na daima alikuwa akiwafundisha watu.