Jun 25, 2014

USHINDI WA SHOESHINE FESTICAB: Kwanini hatutilii maanani filamu fupi?

 Amil Shivji


TAKRIBAN wiki mbili zilizopita nilikuwa mjini Bujumbura nchini Burundi kwa mwaliko wa Shirika la Kijerumani la GIZ, ambapo Mtandao wa Wanafilamu wa Afrika Mashariki ulikuwa ukizinduliwa rasmi, sambamba na Tuzo za filamu kwenye Tamasha la Kimataifa la Filamu la Burundi (Festicab) 2014, linalofanyika jijini Bujumbura.



Kabla ya safari yangu hii, nilipata bahati ya kupitia nchi zingine kama mbili ambapo nilipata nafasi ya kukutana na watengeneza filamu wa nchi hizo, na kwa kweli nilijifunza mengi kutoka kwao.

Jun 16, 2014

HARAKATI ZA TAFF: Serikali, sikieni kilio chetu kwa mustakabali wa Taifa



Katibu Mkuu wa TAFF, Bishop Hiluka, akitoa ufafanuzi katika warsha ya wadau wa sanaa nchini, iliyofanyika kwenye hoteli ya Chichi, Kinondoni B, jijini Dar es Salaam hivi karibuni
 
HEBU jaribu kupata picha: umelima shamba lako na kupanda mahindi ambayo umeyatunza vizuri na yako tayari kuvunwa… unaamka siku moja na kukuta kuna mtu kayavuna na ameanzisha biashara inayompatia fedha nzuri wakati wewe uliyelima huna hata fedha ya kula! Au umenunua suti nzuri akaja mtu akaivaa harusini, kesho yake anakuja kukutaarifu jinsi walivyomsifia harusini kwa kupendeza na suti yako. Hiyo ndio picha ilivyo katika shughuli za sanaa Tanzania. Na haswa katika mambo ya filamu.

Katika mifano hii midogo moja kwa moja unapata picha halisi ya kile kinachoendelea kwenye tasnia ya filamu na hata sanaa zingine hapa nchini, ambayo tunaweza kuiita kuwa ni shamba la bibi, kwani kila anayejisikia anaingia, anavuna tani yake na kufaidi mazao pasipo kulima.

Jun 11, 2014

Wasanii wanajifunza nini kwenye vifo mfululizo vya wasanii wenzao?

Marehemu Said Ngamba maaruf kwa jina la Mzee Small



KWANZA naomba nianze kwa kutoa pole kwa familia nzima ya wasanii na wadau wa filamu nchini kufuatia vifo mfululizo vya wasanii wa filamu ndani ya wiki tatu; Adam Kuambiana, Rachel Haule, George Otieno “Tyson) na Said Ngamba maarufu kama Mzee Small. Mfululizo wa vifo hivi umeambatana na uvumi au dhana potofu inayosambaa kwa kasi, eti vifo mfululizo vya wasanii vinatokana na kafara inayofanywa na baadhi ya wadau (wasanii) ndani ya tasnia ya filamu kwa lengo fulani lenye maslahi kwao.

Uvumi huu umejitokeza hasa baada ya kushuhudia kundi la watu fulani likiwa ndiyo kinara wa kukumbatia misiba ya wasanii nyota, kuunda kamati mbalimbali na kuchangisha fedha nyingi ambazo baadhi yake zimekuwa zikitumika kununulia majeneza ya bei mbaya, vyakula vya gharama (utadhani kuna sherehe) na shughuli zingine ikiwemo ukodishaji wa magari ya kusindikiza msafara wakati wa mazishi. Lakini kama hiyo haitoshi, kumeripotiwa pia kufanyika kwa ubadhirifu wa pesa.