Mmoja wa wasanii wenye mafanikio kisanii nchini Tanzania,
Yvonne Cherryl maarufu kwa jina la Monalisa
HIVI karibuni nilikuwa katika kikao cha wadau saba wa filamu waliopendekezwa kuunda kamati maalum itakayokuwa na lengo kuu la kupitia na kutoa maoni katika filamu zetu, ili kuziboresha na hatimaye kuongeza ufanisi katika uzalishaji wa filamu kwenye tasnia hii nchini. Kamati hiyo ya watu saba ilipendekezwa na wadau mbalimbali wa filamu kwa kupiga kura kupitia mtandao wa kijamii wa facebook/ Tanzania Film Critics Association.
Ukosoaji wa filamu duniani ni uchambuzi na utathmini wa filamu, iwe kwa mtu mmoja mmoja au kwa pamoja. Kwa ujumla, kazi hii ya ukosoaji wa filamu inaweza kugawanywa katika makundi mbalimbali kama vile mapitio ya filamu yanayofanywa na waandishi wa habari ambayo huonekana mara kwa mara katika magazeti,