Rais wa Shirikisho la Filamu nchini, Simon Mwakifwamba
IJUMAA iliyopita nilielezea udhaifu wa wasanii kutojitambua unaotokana na kulewa umaarufu, pia niliuliza swali kama sanaa zetu zilivyo leo zinaweka kumbukumbu nzuri itakayorithiwa na vizazi vijavyo na kuashiria historia inayolingana na mila na desturi nzuri za kizazi husika. Au kama tunaweka kumbukumbu potofu ya sanaa zetu na uasili wake kwa vizazi vijavyo?
Leo najaribu kuangalia kwa makini kuhusu mfumo wetu wa usambazaji wa kazi za sanaa (hasa filamu) kutokana na sababu kuu mbili: kwanza nimepokea meseji kadhaa za wasomaji mbalimbali zilizonisisitiza nieleze namna tunavyoweza kujikwamua katika usambazaji na namna gani tunaweza kufanikiwa kuondokana na uharamia wa kazi za sanaa.