NAUKUBALI sana
mkoa wa Tanga, una historia nzuri katika burudani na unaaminika kuwa ndio
kitovu cha burudani katika nchi hii, kuanzia kabumbu, muziki, sinema na
kadhalika. Tanga ni jiji lililo
ufukoni mwa Bahari ya Hindi.
Jina la mji wa Tanga
linaaminiwa kutokana na neno “tanga” yaani kitambaa kikubwa kinachokingamishwa
kwenye mlingoti wa jahazi, ilipewa jina hilo kwa sababu kisiwa cha Toten ilipo
hori ya Tanga kina umbo linalofanana na kitambaa cha aina hii.