Marehemu Hammie Rajab
Marehemu Hammie Rajab akiongoza upigaji picha za filamu
ALHAMISI ya Aprili 21, 2011 saa tatu asubuhi, nilipokea ujumbe mfupi kwenye simu yangu uliotoka kwa Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Simon Mwakifwamba, akinijulisha kuhusu kifo cha mmoja wa watunzi mahiri wa vitabu na muongozaji wa filamu nchini ambaye nchi hii imepata kumshuhudia, Hammie Rajab.
Mwakifwamba alinijulisha kuhusu msiba huo ambao umeacha pigo sio tu kwa wapenzi wa riwaya bali kwa tasnia nzima ya filamu nchini.