Desmond Eliot, msanii wa Nollywood
HIVI karibuni Nigeria imetangazwa kuwa ndilo Taifa lenye uchumi mkubwa barani
Africa na kuipita Afrika Kusini. Pato Ghafi la Ndani (Gross
Domestic Product ‘GDP’) la Nigeria limefikia Dola Billion 509 huku lile la Afrika ya
Kusini likifikia Dola Bilioni 322.
Kwa mujibu wa Idara ya Takwimu yaNigeria , Nigeria imekuwa Taifa lenye uchumi mkubwa Afrika baada ya
wanauchumi wa nchi hiyo kuziongeza sekta za Mawasiliano na Filamu (Nollywood)
kwenye takwimu. Ni dhahiri kuwa soko la Filamu la Nigeria linatoa mchango mkubwa mno katika ukuaji wa uchumi
wa nchi hiyo. Kabla ya hapo Nigeria ilionekana kama taifa linalotegemea zaidi uuzaji wa mafuta na ilikadiriwa kuwa pato la
mafuta lilichangia asilimia 32 kwenye GDP lakini ripoti ya wanauchumi hivi
karibuni imeonesha sasa pato la mafuta huchangia Asilimia 15 tu ya pato ghafi
la ndani.
Kwa mujibu wa Idara ya Takwimu ya