Jaji Joseph Sinde Warioba
BAADA ya uhuru mwaka 1961,
iliundwa Wizara ya Utamaduni wa Taifa na Vijana, mwaka 1962, Rais wa kwanza wa
Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere alitamka wazi kuwa Utamaduni ni kiini na roho
ya Taifa, nchi inayokosa utamaduni wake ni sawa na mkusanyiko wa watu usiokuwa
na roho na hivyo kukosa sifa ya kuitwa taifa kamili.
Sera ya utamaduni
ilizinduliwa Agosti 23 mwaka 1997 mjini Dodoma
ikiwa ni hatua ya pili muhimu baada ya ile ya kuundwa kwa Wizara ya Utamaduni
wa Taifa na Vijana mwaka 1962.