Jul 18, 2013

KUPUUZWA KWA UTAMADUNI: Hii ndo fursa ya wasanii kuchangia maoni yao rasimu ya Katiba mpya


Jaji Joseph Sinde Warioba

BAADA ya uhuru mwaka 1961, iliundwa Wizara ya Utamaduni wa Taifa na Vijana, mwaka 1962, Rais wa kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere alitamka wazi kuwa Utamaduni ni kiini na roho ya Taifa, nchi inayokosa utamaduni wake ni sawa na mkusanyiko wa watu usiokuwa na roho na hivyo kukosa sifa ya kuitwa taifa kamili.

Sera ya utamaduni ilizinduliwa Agosti 23 mwaka 1997 mjini Dodoma ikiwa ni hatua ya pili muhimu baada ya ile ya kuundwa kwa Wizara ya Utamaduni wa Taifa na Vijana mwaka 1962.

Jul 4, 2013

Umuhimu wa Shirikisho la Filamu Tanzania ni kwenye misiba tu?

Linathaminiwa wakati wa misiba ya wasanii tu na kutupwa katika shughuli zingine za kijamii



Sehemu ya umati wa watu katika Tamasha la Filamu jijini Mwanza

Mmoja wa wasanii wa Bongo Movie, Jacob Steven (JB), 
akigawa vyandarua jijini Mwanza

NI asubuhi tulivu ya Jumatano, siku moja tu baada ya kumalizika kwa ziara ya kiongozi mkuu wa taifa linaloongoza duniani la Marekani, Rais Barack Obama, aliyeondoka nchini baada ya ziara yake ya siku mbili. Nikiwa nimekaa sebuleni nikifuatilia kipindi cha televisheni cha ‘Tuongee Asubuhi’ kinachorushwa na moja ya vituo vya runinga hapa nchini, ambapo kulikuwa na mada iliyosema “Nafasi ya filamu katika soko la kimataifa”.

Katika mada hii, walialikwa wasanii wa jijini Mwanza, Hussein Kim, Prosper Kiri na Anita Kajumulo, na Dar es Salaam kulikuwa na Steve Mengere na Mwakilishi wa TBL wa kinywaji cha Grand Malt, Fimbo Butala. Mada hii ilijikita zaidi kulielezea Tamasha la filamu linaloendelea jijini Mwanza chini ya udhamini wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia kinywaji cha Grand Malt.