Jan 1, 2015

Mwaka 2014 umeshuhudia vifo mfululizo vya wasanii

* Wapo waliohusisha vifo hivi na kafara

Marehemu George Otieno Okumu "Tyson"

Marehemu Adam Phillip Kuambiana
 TUMEINGIA mwaka mpya 2015 tukitaraji mafanikio makubwa zaidi na tukiuaga mwaka 2014 uliokuwa wa simanzi kwa tasnia ya filamu tulipokumbwa na taharuki kufuatia vifo vilivyotokea mfululizo vya wasanii wa filamu vilivyotokea katika muda mfupi mfupi. Kufuatia vifo hivyo tetesi zilienea mitaani kwamba vifo hivyo vilitokana na kutoana kafara!