Feb 4, 2015

Dunia na historia ya filamu

D. W. Griffith

Muongozaji wa filamu Tanzania, John Lister Manyara
SINEMA za mwanzo zilijielekeza kama vile sehemu ya jukwaa mbele ya pazia. Kamera iliwekwa katika sehemu moja na matendo yote katika tukio zima yalifanyika ndani ya fremu moja ya kamera na kwa pigo moja (one shot). Mtazamo wa watazamaji kipindi hicho haukutofautiana na watazamaji ambao leo wanakaa mbele ya jukwaa wakiangalia maigizo ya jukwaani. Ni D. W. Griffith, aliyekuwa wa kwanza kuwahamishia watazamaji katika ulingo wa sinema kwa kazi zake za “For Love of Gold (1908)”; “The Lonely Villa (1909)”; “The Lonedale Operator (1911)”; na iliyovutia zaidi, “Birth of a Nation (1915)”.