Nov 30, 2011

SWAHILIWOOD: Wenzetu wameweza, kwa nini tushindwe?

* MFDI-Tanzania wameanza rasmi mkakati wa mafunzo

Waziri wa Habari, Utamaduni Michezo na Vijana, 
Emmanuel John Nchimbi
 
WIKI iliyopita, kuanzia Jumanne ya tarehe 22 Novemba hadi Jumamosi ya tarehe 26 Novemba, kulikuwa na warsha ya siku tano ambayo ni ya kwanza katika mkakati maalum uliowekwa na taasisi ya Media for Development International – Tanzania (MFDI-Tanzania), kuhakikisha kuwa tasnia ya filamu nchini “Swahiliwood” kama ambavyo wanapenda ijulikane, inafikia kile ambacho tasnia zingine duniani zimeweza, kwa kuandaa warsha iliyohudhuriwa na washiriki 25, wakiwemo watayarishaji wa filamu maarufu na waandishi maarufu wa script.

Warsha hii iliyoandaliwa na MFDI-Tanzania, ambayo mimi nilikuwa mmoja kati ya washiriki waliohudhuria mafunzo maalum ya jinsi ya utafiti na uandishi wa miswada andishi.

Nov 28, 2011

Ili kuboresha filamu zetu tuanze kwanza na script

John Riber

Moja ya semina zilizoandaliwa na MFDI

“MWANAHARAKATI, nimekuwa nafuatili sana makala zako, kuna makala moja ilinigusa sana, hasa pale uliposisitiza kuwa uzuri wa stori yoyote unatokana na msuko mzuri wa matukio, msuko unaohitaji creativity na inspiration. Pia ukasisitiza kwamba unapotunga stori yoyote inayohitaji msuko mzuri wa matukio unahitaji sana 'meditation' na kufanya utafiti wa kina wa kile unachokiandikia...



Kwa kifupi, makala yako imenifanya kuelewa kwa kiasi fulani kuhusu msuko mzuri wa matukio katika stori kwamba ndiyo utakaomfanya mtazamaji wa filamu au msomaji wa hadithi apate hamu ya kuendelea mbele zaidi ili kujua kitakachotokea.

Nov 16, 2011

Hadhi ya Tasnia ya Filamu nchini

 Upigaji picha za filamu Hollywood

Filamu ya Harusi ya Mariam iliyotengenezwa nchini

KUMEKUWEPO mjadala mkubwa kuhusu ukuaji wa soko la filamu hapa nchini na nini kifanyike ili tuweze kutoa filamu nzuri zaidi zenye ubora. Mimi nimekuwa nikitamani kwanza sekta hii ya filamu iwe rasmi kabla ya mambo yote kwa kuwa naamini mitaji, vifaa na rasilimali zipo kila mahali, ila bila kuwa rasmi yote haya tunayoyatarijia hayatawezekana.

Leo nimeamua kuandika mada hii hasa kufuatia mada niliyoandika wiki mbili zilizopita ambapo nilieleza jinsi tasnia yetu ya filamu ilivyopiga hatua katika uzalishaji wa filamu na kuwa ya tatu Barani Afrika (kwa kutoa filamu nyingi bila kujali ubora), ikizifuatia Nigeria inayoongoza na Ghana. Lakini bahati mbaya tuliyonayo ni kwamba mafanikio haya ya kuwa wa tatu katika Afrika hayaendani kabisa na uhalisia wake.

Nov 14, 2011

Kwa nini hatutafuti watunzi wazuri wa stori katika filamu? KULIKONI, NOV 11, 2011

 Hamisi Kibari

 Hussein Tuwa

 Adam Shafi

MAJUZI nilikutana na mdau mmoja wa filamu ambaye tumefahamiana kupitia mtandao wa jamii wa facebook. Katika mazungumzo yetu yaliyochukua takriban saa mbili mdau huyo aliniambia kuwa anapenda sana kusoma makala zangu kwa kuwa anaamini kama zingekuwa zikifanyiwa kazi basi tasnia hii ingefika mbali.

Katika mazungumzo hayo, kikubwa zaidi alitaka kujua kwa nini filamu zetu nyingi zinatumia sana hadithi za kuiga kutoka Nigeria na kwingineko. Aliniambia kuwa kwa uelewa wake anadhani tatizo kubwa lililopo kwenye filamu (nyingi) za Kitanzania ni uwezo mdogo wa uandishi wa hadithi na miongozo ya filamu, kitu ambacho kinasababisha filamu zetu kuonekana hazina muelekeo.

Nov 2, 2011

BONGO MOVIE: Tasnia ya tatu Barani Afrika isiyoendana na uhalisia wake



 Upigaji picha wa filamu ya Mzimu wa Maisara

 Filamu ya Fasta Fasta

IMEKUWA ikisemwa na wadau mbalimbali kuwa Tasnia ya Filamu nchini imekua na kupiga hatua, lakini kwa bahati mbaya kati ya wote wanaosema hivyo hakuna hata mmoja ambaye anaweza kuelezea kwa vitendo zaidi ya kusema tu siku hizi filamu zinatoka kwa wingi, jambo ambalo bado si mwafaka kwa tathmini inayoweza kutumiwa kumshawishi mtu makini aliye nje sekta hii kuingia na kuwa Mwekezaji.

Na imekuwa ikiaminika kuwa sekta ya filamu imeanza kuwa biashara rasmi baada ya mwaka 2002 ambapo ni baada ya filamu ya “Girlfriend” kuingia kwa kishindo na kuwaaminisha Watanzania kuwa kuna Watanzania wanaoweza kupigana vita na filamu kutoka nje ya nchi ambazo kwa kiwango kikubwa zilikuwa zimeshika chati,