Nov 4, 2015

DK. JOHN MAGUFULI: Wasanii wanasubiri utekelezaji wa ahadi zako

Rais Mteule Dk. John Pombe Magufuli, akijiachia jukwaani pamoja na wasanii wa kundi la Yamoto Band kwenye uwanja wa Mashujaa mkoani Mtwara, wakati wa kampeni

KWANZA kabisa napenda nikupongeze kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Tanzania katika Awamu ya Tano, nikitumaini kuwa wananchi wamekupa ridhaa kwa kuwa wamekuona unafaa zaidi kuiongoza nchi hii baada ya Rais Jakaya Kikwete, ambaye uongozi wake unahitimishwa kesho Alhamisi.

Ingawa kuna minong’ono na wasiwasi mwingi kuwa huenda wewe huna ‘interest’ kabisa na masuala ya sanaa, na uongozi wako utajikita zaidi kwenye kujenga barabara, reli, uwekezaji, kilimo, mifugo, uchimbaji madini nk, lakini nina imani kuwa uongozi wako utawapa wasanii tumaini jipya.