Feb 23, 2018

Tutumie filamu na muziki kutangaza utalii

Mlima Kilimanjaro

KATIKA nchi hii kuna maeneo bora ya upigaji picha, kuanzia Tanzania Bara hadi Zanzibar, kuanzia kwenye mlima mrefu hadi kwenye maziwa yenye kina kirefu kabisa katika Bara la Afrika.Tanzania ni nchi ya maajabu na vivutio: mlima mrefu Afrika (Mlima Kilimanjaro), mbuga bora yenye wanyama wa kuvutia duniani ya Serengeti, yenye stori ya wanyama wanaohama kila mwaka na kurejea.

Bila kuzunguka, hebu tutafakari ni kwa namna gani filamu na muziki vimeweza kuitangaza Nigeria? Tuanzie filamu, tasnia yao ya filamu (Nollywood) imeweza kuwatangaza kwa kiasi gani? Tutapata jibu la haraka kwamba taifa hilo limetangazika kwa kiwango ambacho siyo cha kawaida wala cha chini.