Dec 31, 2017

Mwaka 2017 umekwisha, dira ya wasanii ni ipi?

Wasanii mbalimbali wakifuatilia mjadala kwenye ukumbi wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA)

Msanii akipiga tarumbeta

HEBU fikiria, unaamka asubuhi na mapema, unajiandaa na kubeba begi lako kisha unaelekea kituo cha basi, unalikuta gari na kupanda, lakini hujui unaelekea wapi!

Au mpo katika kituo cha mabasi, mara basi linakuja, kila mmoja analikimbilia na kupanda, tena mnafikia hatua ya kugombea siti, na safari inapoanza ndipo mnagundua kuwa gari haliendi kule mnakokwenda. Mnataharuki na kuanza kumpigia kelele dereva kumtaka asimamishe gari!

Dereva anawashangaa na analiegesha gari pembeni, kisha anawauliza kwani ninyi mnaelekea wapi? Hapo ndipo mnapojigundua kuwa kila mmoja anaelekea sehemu tofauti kabisa na linakokwenda gari!

Oct 23, 2017

Wasanii vunjeni ukuta wa fikra

Peter Tosh
Filamu ya Off Side
“EVERYBODY want to go to heaven, but nobody want to die…” hii ni nukuu kutoka kwenye wimbo wa Equal Rights wa aliyekuwa mwanamuziki mahiri wa reggae duniani, Peter Tosh. Maneno hayo ambayo tafsiri yake kwa lugha ya Kiswahili ni “Kila mtu anataka kwenda peponi, lakini hakuna anayetaka kufa…”

Sikuwa shabiki wa muziki wa reggae, ila nilipolazimika kusikiliza reggae nilipenda nyimbo za Lucky Dube na Peter Tosh. Wanamuziki wote wawili kwa sasa ni marehemu.

Ukiusikiliza kwa makini ujumbe ndani ya wimbo wa Equal Rights, utagundua kuwa ni chemsha bongo ya aina fulani. Maneno ya Peter Tosh katika wimbo huu yanaakisi hali halisi ilivyo katika shughuli za sanaa Tanzania, hasa muziki na filamu.

Muziki wa Singeli: ni mapinduzi mapya au kifo cha muziki?

Mwanamuziki Msaga Sumu

Mwanamuziki Sholo Mwamba
MUZIKI wa Tanzania unabadilika sana, wasanii wengi wamekuwa wakibuni mitindo ya aina mbalimbali ili kuzifanya kazi zao ziende mbali na kuvuta mashabiki wa muziki nchini na duniani kwa ujumla.

Miaka ya nyuma muziki wa dansi ndiyo ulikuwa ulishika hatamu, muziki huu ulioanza kama klabu ambapo watu walialikana kucheza aina mbalimbali za muziki wa kizungu mtindo maarufu uliojulikana kama ballroom dancing. Kisha taratibu ukaumbika ukifuata muziki wa soukous kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (rumba ya Kikongo) na tokea hapo ikawa inaitwa ‘rumba ya Tanzania’.

Oct 14, 2017

Miaka 18 baada ya kifo cha Mwalimu Julius K. Nyerere: Je, tunalinda utamaduni wetu kama alivyoamini?


LEO tunaadhimisha kumbukumbu ya miaka 18 tangu Baba wa Taifa na muasisi wa taifa hili, Rais wa kwanza wa Tanzania, Hayati Mwalimu Julius Nyerere aliyefariki dunia Oktoba 14, 1999 jijini London, Uingereza na kuzikwa Butiama, kijiji alichozaliwa.

Mwalimu Nyerere alikuwa kati ya viongozi wachache wa Afrika walioacha mwangwi katika utamaduni wa nchi zao.

Nyerere alikuwa mwalimu. Ni sahihi kusema silika ya ualimu iliathiri siasa na matendo ya Mwalimu Nyerere kama kiongozi wa Tanganyika na baadaye Tanzania. Aliiona nchi yake kama darasa na daima alikuwa akiwafundisha watu.

Sep 8, 2017

Madhara Yanayosababishwa na Ponografia



MAPOKEO ya kazi za sanaa katika jamii yoyote hufuata utaratibu wa kurithisha mfumo, mtindo, muundo, maudhui na hivyo hubaki kuelezea juhudi, matatizo au mafanikio ya jamii husika.

Kama sanaa zenu haziakisi maisha yenu, basi mjue kuwa vizazi vyenu vitarithi mambo yasiyokuwa yenu. Sanaa kama nguzo mojawapo muhimu ya Utamaduni hukua na pia hufa.
Unaweza kujiuliza; Je, filamu zetu zilivyo leo zinaweka kumbukumbu nzuri itakayorithiwa na vizazi vijavyo? Au kizazi chetu kinaweka kumbukumbu potofu ya filamu na sanaa zetu na utamaduni kwa vizazi vijavyo?

Jul 27, 2017

Hakuna shaka Tanga ndio kitovu cha burudani Tanzania



NAUKUBALI sana mkoa wa Tanga, una historia nzuri katika burudani na unaaminika kuwa ndio kitovu cha burudani katika nchi hii, kuanzia kabumbu, muziki, sinema na kadhalika. Tanga ni jiji lililo ufukoni mwa Bahari ya Hindi.

Jina la mji wa Tanga linaaminiwa kutokana na neno “tanga” yaani kitambaa kikubwa kinachokingamishwa kwenye mlingoti wa jahazi, ilipewa jina hilo kwa sababu kisiwa cha Toten ilipo hori ya Tanga kina umbo linalofanana na kitambaa cha aina hii.

Jul 18, 2017

SRIDEVI KAPOOR: Supastaa wa kwanza mwanamke Bollywood

Sridevi Kapoor
TASNIA ya filamu ya India maarufu kwa jina la ‘Bollywood’ hadi sasa imekwisha tengeneza mastaa wengi wakubwa waliojulikana duniani, wakatengeneza pesa nyingi na kupata heshima kubwa ndani ya India na hadi nje ya mipaka ya India. Kwa mpenzi yeyote wa sinema, iwe ni sinema za Hollywood (tasnia ya sinema ya Marekani), au Nollywood (tasnia ya sinema ya Nigeria) bado atakuwa amekwishaziona filamu za India.

Nollywood mara nyingi wamekuwa wakiiga kutoka Bollywood, tasnia ambayo imewatengeneza waigizaji maarufu duniani kama Amitabh Bachchan, Shahrukh Khan, Aamir Khan, Salman Khan, Dilip Kumar, Raj Kapoor, Dharmendra, Hrithik Roshan, Rish Kapoor na wengine wengi kwa upande wa wanaume.

Forrest Gump: Sinema pekee yenye kuonesha Marekani wameshindwa Vietnam

Forrest Gump

NILIPOITAZAMA sinema ya Forest Gump kwa mara ya kwanza haikunivutia, nadhani ni kwa sababu wakati huo sikuwa makini kama sasa. Nilipoiangalia tena nikagundua kuwa ni ‘bonge la sinema’. Sinema hii inafundisha mengi kuhusu maisha na maana ya maisha. Kwamba maisha si mabaya kama ambavyo watu wengi wanataka yaonekane. Kwamba kijana asiye na hatia anaweza kufanikisha maisha ya wengi kwa hali yake.

Na kama hujawahi kuiona au unadhani hujaipenda nakushauri uitazame tena. Inastaajabisha kwelikweli… ni moja ya sinema bomba sana, na kwa kweli ilistahili kuzoa tuzo.

Tasnia ya filamu Tanzania ni sawa na soka bila refa!

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akiongoza maandamano ya Wasanii wa Filamu

HADI leo sijajua ni ‘impact’ gani iliachwa na maandamano ya mwezi Aprili mwaka huu ya wasanii wa filamu walioandamana kushinikiza kusitishwa kwa uuzwaji wa filamu kutoka nje ya nchi kwa madai zinaharibu soko la ndani!
Athari pekee niliyoishuhudia ni ufa uliojitokeza kati ya wasanii waliounga mkono maandamano na waliopinga, kiasi cha kuibua mihemko iliyosababisha kutishiana maisha na kutukanana matusi ya nguoni.

Kwa sasa Sekta ya filamu Tanzania ipo ‘Babeli’ ingawa ilifikia hatua ya kutingisha Afrika. Sidhani kama kuna mtu atabisha kuwa filamu za kibongo ‘hazikutesa’ Afrika Mashariki na nchi za Maziwa Makuu. Filamu hizi zilisaidia kwa kiwango fulani kuitangaza Tanzania na kuwatangaza wasanii wa nchi hii. Sinema hizi ziliuzwa kwa wingi mitaani, watu walizichangamkia; wanawake na vijana ndio wakiwa wateja wakubwa wa sinema hizi.

Sonam Kapoor: Kufanya kazi nyuma ya Kamera kumenisaidia

Mwigizaji maarufu wa Bollywood, Sonam Kapoor

FILAMU zimepitia hatua kwa hatua zikianzia kwenye mawazo hadi kuwa nyenzo muhimu ya burudani na mwasilisha taarifa muhimu wa karne hii. Kutengeneza sinema nzuri inahitaji gharama kubwa. Na kufanikiwa kwake kunategemea watazamaji ambao huwezi kutabiri watapendezwa na nini. Huwezi kujua ni lini jambo fulani litawavutia au kuwasisimua.

Mara nyingi, matayarisho yanayofanywa kabla ya upigaji picha ndiyo sehemu muhimu zaidi ambayo huchukua muda mrefu katika utengenezaji wa sinema. Kama tu ilivyo kwa mradi wowote mkubwa, mafanikio yake hutegemea sana matayarisho.

My Wife's Murder: Sinema ya Bollywood itakayokuacha mdomo wazi muda wote

Filamu ya My Wife's Murder ya India
NI kazi ngumu kufuatilia mipango ya muuaji usiyemjua, lakini muongozaji wa filamu za Bollywood, Jijy Phillip, amejaribu kufikiri nje ya boksi katika kisa cha filamu ya My Wife's Murder (Mauaji ya Mke Wangu). Filamu hii ilitengenezwa upya kufuatia filamu ya kwanza iliyoitwa ‘Madhyanam Hathya’, iliyoongozwa na Ram Gopal Varma. Hadithi ya filamu hii inaonekana kuchukua kisa cha Horace William Manton, mtuhumiwa mkuu katika kesi ya mauaji ya Luton Sack.

Lengo la sinema yoyote ni kumsisimua na kumfanya mtazamaji muda wote macho yake yasitoke kwenye runinga hadi mwisho, na filamu hii imefanikiwa. Ukianza kuiangalia utajikuta umekamatika ndani ya dakika 15 tu za mwanzo. Inspekta (Mkaguzi) wa Polisi Tejpal Randhawa (Boman Irani) anapewa jukumu la kuchunguza kesi ya mwanamke aliyekufa na mwili wake kupatikana katika bwawa.

Soko la filamu Tanzania halijafa bali mfumo ndiyo mbovu (2)

Filamu ya Chalii wa Ngarenaro

KIGEZO cha pili cha kusaidia soko la filamu ni jukwaa la uwasilishaji; watazamaji wanahitaji majukwaa ya habari. Falsafa hii ni muhimu wakati unaposhughulikia maudhui yanayowafaa watazamaji. Maudhui ya jukwaa la uwasilishaji katika dunia ya kisasa ya filamu hayaishii tu kwenye kazi ya usambazaji, yanakwenda ndani zaidi ya soko la filamu lilivyo. Jukwaa husaidia kuwasilisha mawazo kwa watu katika njia itakayojumuisha mitazamo yao. 

Jukwaa muafaka litampa urahisi mtengenezaji wa filamu kuendana na ushindani wa soko. Watoaji filamu wanatakiwa kuandaa takwimu ya watazamaji na kukutana nao katika dunia yao iliyostawi kwenye kundi la teknolojia ya digitali. 

Filamu ni bidhaa kama zilivyo bidhaa nyingine, kuzitangaza na kuzisambaza ni vitu vyenye umuhimu sawa. Lazima kuwe na mkakati wa kujitangaza kwenye mitandao ya intaneti. Hii itaongeza mipaka katika utekelezaji wa kampeni ya kuzitangaza. 

Soko la filamu Tanzania halijafa bali mfumo ndiyo mbovu (1)

Msanii Jacob Steven maarufu kama JB akipokea Tuzo kutoka kwa Msambazaji wa filamu, Dilesh Solanki wa Steps Entertainment

KATIKA sekta za filamu kwenye nchi zilizopiga hatua, biashara ya filamu huanza na Box Office (mfumo maalum unaoanzia kwenye uoneshaji sinema ndani ya majumba ya sinema 'theatres') au kutolewa katika njia ya sinema.
Baadaye hurushwa kwenye vituo vya televisheni za kulipia, baadaye kwenye vyombo vya habari saidizi (video games, mitandao maalumu ya kupakua filamu, katuni n.k.), kisha katika televisheni za umma na mwisho kutolewa kama bidhaa rasmi (DVD) kwa matumizi ya nyumbani.

Huu ni mfumo maalumu wa kimasoko katika studio kubwa za filamu, iwe ni Uingereza, Marekani, India, China, au hata Afrika Kusini na nchi zingine zilizopiga hatua. Ni mfumo unaotumika katika mkondo mkuu (main stream), ambapo studio kubwa huwekeza na kusambaza kazi zilizotegenezwa kwa bajeti kubwa.

Jun 6, 2017

Bibi Esther Mahlangu: Darasa zuri kwa wasanii wa Tanzania

Msanii wa Afrika Kusini, Bibi Esther Mahlangu

NI ukweli usiopingika kuwa sekta ya sanaa nchini ipo chumba cha wagonjwa mahututi, na hatua za makusudi zinahitajika kuchukuliwa (na wasanii wenyewe) kunusuru hali hii.

Nakumbuka miaka ya 1990 hadi 2000, wasanii wa sanaa ya uchoraji walitingisha sana kutokana na kazi zao za michoro. Enzi hizo wachoraji ndio wasanii waliokuwa maarufu (kwa majina yao), ingawa watu hawakuwafahamu kwa sura, kwa kuwa michoro yao ilitamba sana kwenye magazeti na majarida. Na waliweza hata kumiliki magari, japo hayakuwa ya kifahari.