Moja ya mafunzo ya filamu yaliyotolewa hapa nchini.
Hapa washiriki wakibadilishana mawazo nje ya
Kituo cha Utamaduni cha Ujerumani (Goethe Institut).
Kulia ni mwandishi wa makala hii, Bishop Hiluka
Hapa washiriki wakibadilishana mawazo nje ya
Kituo cha Utamaduni cha Ujerumani (Goethe Institut).
Kulia ni mwandishi wa makala hii, Bishop Hiluka
MWISHONI mwa wiki iliyopita Tamasha la Filamu za Nchi za Majahazi (ZIFF 2010), lilihitimishwa huku kukiwa na mambo kadhaa yanayozidi kuitia doa tasnia ya filamu nchini. Katika tamasha hilo filamu zaidi ya 100 zilioneshwa sambamba na wasanii mbalimbali kutoka nchini Tanzania, Afrika na nje ya Afrika kuonesha burudani ndani ya Visiwa vya Zanzibar.
Tamasha hilo la filamu la Zanzibar lililoanza Juni 18 ndani ya Ngome Kongwe Zanzibar, likiwa linafanyika kwa mara ya 14 tokea lilipoanzishwa, limekuwa na mchango mzuri sana katika tasnia ya filamu na linapaswa kuchukuliwa kama somo muhimu sana na waigizaji, waandaaji, waongozaji na watunzi wa filamu wa Tanzania.