Jul 29, 2016

Waziri Nape Nnauye; Angalia pia upande wa pili wa shilingi

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, akiwa katika Operesheni ya kuwasaka waharamia wanaodurufu kazi za wasanii
SERIKALI ya Awamu ya Tano imeanza kuonesha juhudi katika kuisaidia sekta ya sanaa nchini baada ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, kuingia mtaani na kukamata DVDs zisizo na stika ya TRA zinazoingia nchini kinyume na sheria pamoja na zile zinazokwepa kulipa kodi ili kuinua uchumi wa nchi na wasanii.

Waziri Nape Nnauye ameahidi kuwa zoezi hilo litakuwa endelevu nchi nzima akisisitiza kuwa hatua hii ni ya mwanzo kwa kuwaonesha kuwa agizo la Rais John Pombe Magufuli, la kulipa kodi na kununua bidhaa halisi kwa kutoa risiti linasimamiwa ipasavyo.