Dec 29, 2010

Soko la filamu Tanzania linakua? (3)

 Jengo la Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

 Aliyekuwa Naibu Wizara wa Habari Utamaduni na Michezo, 
Joel Nkaya Bendera akisisitiza jambo

*Watazamaji wa kazi za Kiswahili walihamasika zaidi baada ya ITV kurusha mchezo wa Tausi
*Serikali imekusanya sh. Bilioni 2 kwa mwaka 2005 hadi Mei 2009.

BURUDANI nchini Tanzania imepitia mabadiliko makubwa hadi kufika hapa ilipo. Kipindi kile, enzi za kina Black Moses, Maneno Ngedere, Bob Tiger na wengine wengi burudani ya disko ndiyo iliyoshika hatamu. Kipindi hicho ndipo hata zile sinema za kwenye majumba ya sinema (Avalon, Drive Inn Cinema, Empire, Starlight na kadhalika) zilikuwa zimeshika hatamu.

Dec 24, 2010

Vita ya wakoloni dhidi ya utamaduni wetu

Ramani ya bara la Afrika
 Moja ya sanaa za Kiafrika

HISTORIA ya ukoloni katika Bara la Afrika, inaonyesha jinsi walivyojitahidi kuua utamaduni wa Waafrika na kuwajenga katika misingi ya utamaduni wa kizungu. Katika baadhi ya makoloni, ubora wa Mwafrika ulipimwa kwa kiasi ambacho alikuwa amejengeka katika utamaduni huo.

Baadhi ya Waafrika waliweza hata kupewa uraia wa nchi za wakoloni kutokana na vile walivyokuwa wamejiimarisha katika  ‘ustaarabu’ wa wakoloni. Mchakato wa elimu haukuwa na maana tu ya kuwapatia Waafrika maarifa na ujuzi, bali pia ilikuwa ni fursa ya kuwaondoa katika utamaduni wao na kuwajenga katika utamaduni wa kizungu.

Sanaa na utamaduni wa Tanzania vithaminiwe

Rais Jakaya Kikwete akipiga ngoma ya kisukuma, 
moja ya tamadauni za Kitanzania 

 Kingo, moja ya majarida ya Kitanzania. 
Hapa alikuwa akitafuta Miss Tanzania wa ukweli

KADRI miaka inavyozidi kusonga mbele, ndivyo mabadiliko ya sayansi na teknolojia yanavyoongezeka nchini Tanzania, pia ndivyo jamii inavyosahau utamaduni wao kwa kuiga utamaduni wa kigeni ambao ingawa una faida, lakini matatizo ni makubwa zaidi. 
 
Tangu utandawazi ulipoanza kushamiri katika miaka ya 2000, ndivyo uigaji wa utamaduni kutoka mataifa mengine ya nje, nao uliingia kwa kasi nchini Tanzania, ambapo wananchi wengi nchini Tanzania waliacha utamaduni wao na kuiga wa nje.

Dec 21, 2010

Soko la filamu Tanzania linakua? (2)

Kava la filamu ya Aunt Suzzy, moja ya kazi za Kitanzania

Msanii wa filamu za Kibongo maaruf kama Kishoka

MWAKA 1945, baada ya Vita Kuu ya Pili, uoneshaji na usambazaji wa sinema ulibadilika kidogo kwenye baadhi ya sinema. Sinema kama “Mister English at Home” na “An African in London” zilitengenezwa kutufundisha mambo na tamaduni za Kiingereza. Hata sinema zilizoanza kutengenezwa nchini baadaye zilizingatia mambo kadha wa kadha kama; faida ya dawa (tiba) za Kimagharibi dhidi ya tiba za Kiafrika.

Waafrika katika filamu za Wazungu walifanywa waonekane (na bado wanaonekana) washenzi, watu wa chini, wafungwa, nk. Wakati mwingine walifanywa waonekane wakatili sana na wanaoamini mambo ya kishirikina.

Dec 15, 2010

Changamoto yatolewa kwa wasanii kuthamini kazi zao

Vincent Kigosi (Ray)

Emmanuel Myamba maaruf kama Pastor Myamba
 Jalida la Baab Kubwa linalopamba 
kichwa cha habari kuhusu wasanii matajiri

Wasanii nchini wameshauriwa kuthamini na kuheshimu kazi zao za sanaa ili ziweze kuwakomboa kiuchumi na kutokuwa tegemezi. Kauli hii imetolewa na Ofisa Utamaduni wa jiji la Mwanza, Rosemary Makenke alipokuwa akiwasilisha mada iitwayo "Sanaa ni Ajira, Tuithamini" kwenye Kikao cha Nane cha Sekta ya Utamaduni kilichofanyika jijini Mwanza.

Ofia Utamaduni huyo alisema kuwa wasanii sharti wajiheshimu wao na kazi zao za sanaa wanazozifanya katika jamii kwa kuwa kazi ya sanaa kwa sasa ni ajira. Pia alisema kuwa sheria ya hakimiliki bado haisimamiwi kikamilifu na kwamba jasho na kazi za wasanii zinaendelea kuporwa na wajanja wachache kila siku.
katika kikao hicho pia kilihudhuriwa na wasanii maaruf, Jacob Stephen maaruf kama JB na Mrisho Mpoto "Mjomba" ambao walikuwa kivutio kwenye mkutano huo.

BASATA yasema kuwa usajiri wa wasanii ndiyo mwanzo wa heshima katika sanaa

Sehemu ya jiji la Mwanza kilipofanyika Kikao cha nane cha Sekta ya Utamaduni

 
Mtendaji Mkuu wa Basata, Ghonche Materego
 
Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), Ghonche Materego amesema kwamba zoezi la usajili wa wadau wa sanaa linaloendelea nchini kote ni mwanzo wa kujenga heshima ya tasnia ya sanaa ambayo kwa miaka mingi imekuwa ikionekana kama ridhaa, isiyo na mchango wowote katika uchumi wa nchi na zaidi ya burudani tu.

Aliyasema hayo alipokuwa akizungumza kwenye Kikao cha nane cha Sekta ya Utamaduni kilichofanyika jijini Mwanza. Materego alisema kwamba, ni vema wasanii, wamiliki wa kumbi za sanaa na utamaduni na wadau wote wanaojihusisha na sekta ya sanaa

Kikao cha Nane cha Sekta ya Utamaduni kimefanyika Mkoani Mwanza

Jengo la PPF ndani ya ROCK CITY

Prof. Hermans Mwansoko na Gonche Materego
Kikao cha nane cha sekta ya Utamaduni kilifanyika jijini Mwanza hivi karibuni kikiwashirikisha wakurugenzi wa idara, maafisa utamaduni wote nchini na wadau mbalimbali wa utamaduni na kuja na mikakati mbalimbali ya uboreshaji.

Mkurugenzi wa Idara ya Utamaduni, Profesa Hermans Mwansoko alisema kikao hicho kilichobeba kaulimbiu ya Sanaa ni Ajira Tuithamini, kikajikita kwenye uwasilishaji wa mada na machapisho mbalimbali kuhusu sekta ya utamaduni ambapo wajumbe walipata fursa ya kujadili, kuja na changamoto mbalimbali na baadaye kupata majibu na dira ya changamoto hizo.

Soko la filamu Tanzania linakua?

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitafakari

TASNIA ya filamu hapa Tanzania kwa miaka ya karibuni imeonekana kupata mwamko mkubwa sana, lakini kwa bahati mbaya (au kwa makusudi) mara nyingi kumekuwa hakuna takwimu au taarifa sahihi kuhusu mwamko na maendeleo ya tasnia hii ya filamu hapa Tanzania.

Miaka michache iliyopita asilimia kubwa ya Watanzania walipendelea kutazama filamu zilizotoka nje ya nchi, hususan sinema za Nigeria na India, lakini hivi sasa hali imekuwa tofauti kidogo. Tofauti hiyo imesababishwa na ujio wa hizi filamu za Kibongo za kizazi kipya (new generation films), kutoka kwa wasanii na waandaaji wa Kitanzania ambao mpaka sasa wamechangia kwa kiasi kikubwa kuitambulisha tasnia ya filamu Tanzania ndani na nje ya mipaka ya nchi.

Dec 7, 2010

HISTORIA YA FILAMU (4): Kukua kwa biashara ya Sinema Duniani

Edwin S. Porter - The Great Train Robbery (1903)

George Melies

KAMA nilivyoanza kuelezea issue iliyopita, biashara ya sinema ilianza kujikita rasmi na kuwa ajira kamili iliyowawezesha watu kujipatia kipato halali kutokana na kazi hiyo.

Kukua kwa sekta ya filamu kulikoambatana na biashara hakukuanza hivi hivi tu, kulitokana na changamoto nyingi sana na kulianza kuonekana kwa Georges Mèliès wa Paris, Ufaransa aliyepiga picha na kufanya maonesho ya filamu (film exhibition) mwaka 1896. Kazi zake kama “A TRIP TO THE MOON (1902)”, kazi inayosadikiwa kuwa ndiyo iliyoanzisha vuguvugu na kutia hamasa (potray) kwa wanasayansi kuhusu safari za angani (space travel).

Dec 1, 2010

HISTORIA YA FILAMU (3): Mwanzo wa Sinema za Sauti (Sound Era)

 Humphrey Bogart, muigizaji anayeshika namba moja ya ubora katika historia

MAJARIBIO ya kuchanganya muziki kwenye sinema kwa kutumia njia mbalimbali hatimaye yalifanikiwa; kurekodi moja kwa moja au kuingizia muziki studio (play back) wakati wa uhariri, ingawa juhudi zilianza tangu kipindi chote tangu mwanzo wa sinema bubu, lakini matatizo makubwa mawili (twin problems) ya kuoanisha (synchronise) na kukuza (amplifiy) sauti katika kiwango kinachostahili yalikuwa kikwazo kikubwa (Eyman, 1997).

Mwaka 1926, studio ya Warner Bros ya Hollywood ilitambulisha mfumo mpya uliojulikana kama ‘Vitaphone’, kwa kutoa sinema fupi zilizotokana na matukio ya moja kwa moja (live entertainment acts) ya wasanii maarufu na baadaye kuongezea sauti maalum (sound effects) na muziki (orchestral scores).

Nov 30, 2010

Jukwaa la Sanaa Basata: Michuzi ahamasisha wasanii kujiunga na mtandao jamii

Muhidin Issa Michuzi akionesha namna mtandao wa youtube unavyofanya kazi

MUHIDINI Issa Michuzi, ambaye ni mwandishi wa habari mwandamizi nchini amewashauri wadau wa sanaa hasa wasanii kuingia kwenye matumizi ya teknolojia ya mtandao jamii ili kujitangaza na kuuza kazi za sanaa duniani kote.

Akizungumza kwenye Jukwaa la Sanaa jana, jukwaa ambalo hufanyika kila Jumatatu kwenye ukumbi wa Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), Ilala Shariff Shamba jijini Dar,

Nov 24, 2010

Mwalimu Nyerere Film Festival kuwakomboa wasanii wetu

Simon Mwakifwamba akihojiwa na 
mtangazaji wa Clouds TV, Zamaradi Mtetema

INAONEKANA kuwa Shirikisho la filamu Tanzania lina mikakati kabambe ya kuikomboa tasnia ya filamu nchini dhidi ya changamoto mbalimbali zinazoikabili. Baadhi ya changamoto hizo ni kuwafanya wasanii wa Tanzania kuwa na maisha bora na pia kuwawezesha kufanya kazi zenye ubora na zinazokubalika ndani na nje ya nchi.

Mikakati hiyo ni pamoja na kuhakikisha sheria ya hakimiliki na hakishiriki inaangaliwa upya, kupambana na maharamia wa kazi za sanaa, kujenga mtandao mpana wa ushirikiano baina ya wadau, kuimarisha uongozi wa vyama mbalimbali vya wadau,

Nov 23, 2010

HISTORIA YA FILAMU 2: Kuibuka kwa ukoo wa Lumiere



Ndugu wawili, Auguste na Louis Lumière

Mwaka1895, nchini Ufaransa ndugu wawili Auguste na Louis Lumière (tamka lumia) walifanikiwa kutengeneza kifaa cha kupigia picha chenye viambatanisho vitatu ndani yake: camera, printer, na projector.

Mwishoni mwa mwaka 1895 jijini Paris, Antoine Lumière ambaye ni baba wa Auguste na Louis alifanya onesho la sinema kwa malipo, huo ndiyo ukawa mwanzo wa kukua kwa sekta hii na soko la filamu (kwa mujibu wa Cook, 1990).

Serikali imeombwa kuinua vipaji

Lisa Jensen

Serikali kupitia baraza lake la sanaa (Basata) imetakiwa kuinua vipaji vya wasanii nchini kwa kuweka wawakilishi kwenye ofisi zake za kibalozi zilizoko nje. Ushauri huo ulitolewa na msanii na mwanaharakati wa sanaa, Lisa Jensen, katika mkutano unaowakutanisha wadau mbalimbali wa sanaa kila Jumatatu, safari hii walikuwa wakijadili kuhusu fursa za wasanii.

Lisa Jensen ambaye aliwahi kuwa mrembo wa Kanda ya Ziwa na mrembo namba tatu wa Tanzania alieleza kuwa tatizo linalokwamisha taaluma hiyo ni kukosa msukumo wa serikali kwani imebainika kuwa wasanii wa Tanzania wanapokuwa nje ya nchi wanakosa maslahi mengi kutokana na uwakilishi mbovu kutoka balozi zilizoko nje.

Aidha wasanii wametakiwa kuungana pamoja ili kuikuza tasnia hiyo ya ubunifu ili kutoa nguvu kwa wadau wote wa sekta hiyo na kuiomba serikali kuipa kipaumbele.

Nov 19, 2010

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) latoa lawama kwa waandishi wa habari

 Mzee Omari Mayanga akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani)

Bango la Jukwaa la sanaa

Gonche Materego, Katibu Mtendaji wa Basata akifafanua kwenye Jukwaa la Sanaa

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limewaangushia lawama waandishi wa habari nchini kuwa wamekuwa wakisusia vikao vya Jukwaa la Sanaa vinavyofanyika kila Jumatatu katika ukumbi wa Baraza. Lawama hizo zimetolewa na mwakilishi wa baraza hilo, Mzee Omari Mayanga alipokuwa akiliwakilisha baraza hilo wakati viongozi wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) walipokuwa wakielezea mikakati yao kwa waandishi wa habari kuhusiana na tamasha la filamu la Mwalimu Nyerere.

Mwalimu Nyerere Film Festival ni Februari 2011

 Rais wa TAFF, Simon Mwakifwamba akitoa ufafanuzi,
pembeni yake ni Katibu Mkuu, Wilson Makubi
Katibu Mkuu wa TAFF, Wilson Makubi akifafanua jambo

Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) limetangaza rasmi tarehe ya tamasha la filamu la Mwalimu Nyerere. Kwa mujibu wa rais wa shirikisho hilo, Simon Mwakifwamba, shirikisho hilo litakuwa linaendesha tamasha la filamu za Tanzania kila mwaka, na litafanyika kwa mara ya kwanza mwezi februari mwakani, 2011.

Rais wa shirikisho alisema hayo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini kwenye ukumbi wa Baraza la sanaa la taifa (Basata) jana Alhamisi, tarehe 18 Nov, 2010 na kubainisha kuwa lengo lao ni kukuza soko la kazi za filamu nchini na kukuza mahusiano ya kisekta kati ya wasanii wa tanzania na wale wa nje ya nchi.

Nov 16, 2010

Historia ya Filamu duniani

Zoöpraxiscope

FILAMU (Motion picture film), au wengine hupenda kuita picha jongefu zimekuwepo kwa zaidi ya miaka mia, historia ya filamu inaanzia mwishoni mwa karne ya 19. Filamu zimepitia hatua kwa hatua hadi kufika hapa zikianzia kwenye mawazo yaliyoonekana mapya hadi kuwa nyenzo muhimu ya mawasiliano na burudani, na hata kuwa mwasilisha taarifa katika karne ya 20 na ya 21. Filamu pia zina athari kubwa (substantial impact) kwenye sanaa, teknolojia, na siasa.

Machapisho mbalimbali yamekuwa yakiwataja ndugu wawili, Auguste na Louis Lumière (tamka Lumia) wa Ufaransa kama waasisi wa filamu duniani na kumsahau William Kennedy Laurie Dickson (WKL Dickson) aliyekuwa injinia mkuu katika kampuni ya Edison Laboratories ya Marekani.

Nov 10, 2010

Rais Kikwete, kazi rasmi ya kuiokoa tasnia ya filamu ni sasa

Rais Jakaya M. Kikwete

KWANZA napenda kukupongeza, Rais Jakaya Kikwete kwa kuchaguliwa tena kuliongoza taifa hili kwa kipindi kingine cha miaka mitano. Pia nakushukuru angalau kwa kuonesha kuutambua mchango wa sekta ya filamu Tanzania. Katika hotuba yako ya kuvunja bunge la tisa uliyoitoa huko Dodoma tarehe 20 Julai 2010, chini ya kipengele cha “Michezo, Burudani na Utamaduni”, ulinukuliwa ukisema, pamoja na mambo mengine kwamba: “...Hivi sasa tumelipia mtaalamu mshauri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam asaidie kutengeneza njia bora ya kusambaza kazi za wasanii wa muziki na filamu ili wapate malipo halali kwa jasho lao. Mafanikio ya zoezi hili yatatufundisha namna ya kuwasaidia wasanii wa fani nyingine pia...”

Ikumbukwe kuwa kwa miaka mingi sasa, wasanii na watengenezaji wa sinema miongoni mwa wadau wengine wa sanaa wameendelea kutoa sinema hapaTanzania ili kujipatia riziki kutokana na kazi yao bila mafanikio. Ingawaje sekta ya filamu ni sekta yenye thamani ya mabilioni ya  fedha, wengi wameishi na kufa maskini.

Rais, serikali yako inapaswa ibadilishe mtazamo wake kuhusu wizi wa sanaa na nakala zisizo halali (pirated copies). Mambo haya lazima iyaone kama wizi na ipinge wizi kwa nguvu zote kama inatarajia kuona taaluma hii ikinawili na kuwaajili vijana wengi na hivyo kuchangia katika kuinua uchumi wa taifa letu. Ieleweke kuwa ni kosa la jinai kuuza au kununua kazi feki, kama ilivyo kwa nchi nyingi zilizofanikiwa katika tasnia hii.

 Cover ya sinema ya Miss Bongo

Taaluma hii haiwezi kukua kama viongozi wataishia kusema tu bila kutekeleza huku kukiwa na mambo mengi yanayoirudisha nyuma. Binafsi nimetumia miaka kadhaa kujifunza na kufanya tafiti mbalimbali kuhusu historia ya filamu, matatizo makubwa katika tasnia hii, mfumo unaofaa kutumika katika tasnia ya filamu na mambo mengine mengi, kutoka na na haya, naweza kukuhakikishia kwamba sekta ya filamu Tanzania ina thamani ya bilioni 200 ya pesa za Tanzania katika biashara, kama tu serikali yako itatilia mkazo na kutoa msaada unaohitajika.

Filamu za Kibongo zinavyoibwa nje ya nchi

Moja ya filamu za Kitanzania, Black Sunday

Filamu ya One by One iliyotengenezwa na Mahsen Awadh, "Cheni" 

Kwa inasikitisha sana kuona wasanii na watengeneza filamu wa Kitanzania wanavyohangaika kujitengenezea sinema kwa pesa za kubangaiza au pengine za mkopo wakitegemea kuuza na kupata faida itakayowawezesha kupiga hatua kimaisha lakini inatokea kwamba watuwengine wanawaibia. Tena inauma sana endapo mtu huyo anayeiba ni tajiri mkubwa.

Nov 9, 2010

Uandishi ni Sanaa adimu


 Bishop J. Hiluka


Kipaji cha uandishi huanza tangu ukiwa mtoto 
hasa kama unapenda kujisomea kama 
mtoto huyu, Magdalena J. Hiluka

IMEANDIKWA kuwa; “hapo mwanzo palikuwepo na neno,” lakini unapoongelea burudani (entertainment industry) imesemwa; “hapo mwanzo palianza na wazo.” Wazo linaweza kukujia katika njia mbalimbali, linaweza kukufikia kutoka kwa mtu yeyote, mahali popote, wakati wowote. Wazo linaweza kuanzia kwa mwandishi, mtayarishaji wa sinema; linaweza kupitia kwa muongozaji wa sinema au mwigizaji. Linaweza hata kuanzia kwa msomaji wa makala, rafiki, ndugu, jamaa au jirani yako.

Wazo linaweza kumfikia yeyote hata anapokuwa akifanya kazi, akifanya mazoezi, akikimbia, akiongea au akiwa kajipumzisha nyumbani anasoma makala hii. Ni ajabu sana; eti wakia (ounce) chache katika ubongo wa mwanadamu huweza kufanya na kuleta mabadiliko au maendeleo makubwa kama tunayoyashuhudia wakati huu wa sayansi na teknolojia.

Nov 3, 2010

Tasnia ya Filamu: Tunamuenzi vipi Mzee Kawawa?

Mzee Rashid Mfaume Kawawa

NAKUBALIANA na maneno kwamba; wasanii ni watu wenye akili nyingi sana. Msanii (wa aina yoyote) ni mtu mbunifu, mwenye uwezo wa kuumba jambo likakubalika kwenye jamii, na ni mtu anayefanya tafiti za kina katika fani yake. Wasanii wanaweza kuwa viongozi wazuri wakiingia kwenye siasa; mojawapo ya waigizaji maaruf walioingia kwenye siasa na kuongoza ni pamoja na Ronald Reagan, Rais wa Marekani (1980-1988), na Arnold Schwarzenegger, gavana wa jimbo tajiri la California.

Oct 27, 2010

FILAMU ZA KITANZANIA: Ni kweli tuna wakosoaji wa filamu? (4)

Mwandishi wa makala haya, Bishop J. Hiluka

SIKU nilipopigiwa simu na mhariri wa gazeti hili akinitaka tuonane sikufikiria kabisa kama angenikabidhi jukumu la kuandika makala kwenye gazeti lake. Sikufikiria kwa sababu sikudhani kama angeweza kunifikiria mimi niandike badala ya wachambuzi wengi maarufu na wa muda mrefu waliopo ambao tayari wameshajijengea heshima kubwa katika uandishi.

Nilisita sana kukubali kwa kuwa sikudhani kama ningeweza kukidhi kiu ya wasomaji, lakini nilipokumbuka uzalendo wangu na kiu yangu ya kutaka tasnia ya filamu hapa Tanzania ikue nikakubali mara moja.

FILAMU ZA KITANZANIA: Ni kweli tuna wakosoaji wa filamu? (3)

 Darasa la ufundishaji wa mafunzo ya filamu (workshop in filmmaking)

NI Ijumaa nyingine, naamka asubuhi na mapema, nawahi usafiri wa kuelekea Posta, kisha naelekea Upanga ambako kipo kituo cha utamaduni cha Ujerumani (Goethe Institut) kunakofanyika mafunzo ya utengenezaji wa filamu (workshop in filmmaking). Mafunzo yaliyoanza wiki mbili zilizopita na yanahitimishwa leo. Mimi ni mmoja wa vijana waliochaguliwa kuhudhuria mafunzo hayo ya nadharia na vitendo yanayoendeshwa na wataalamu waliobobea katika tasnia ya filamu kutoka Ujerumani na Ufaransa kwa ushirikiano wa balozi za Ujerumani na Ufaransa, na kuratibiwa na Goethe Institut na Alliance Francaise.

FILAMU ZA KITANZANIA: Ni kweli tuna wakosoaji wa filamu?

 Florian Lawrence Mtaremwa, mmoja wa watengeneza filamu wa Kitanzania

TASNIA ya filamu ni sekta muhimu sana kwa maendeleo ya taifa lolote. Ni muhimu kwa sababu kubwa tatu; filamu na maigizo hutumika kama mwasilisha taarifa mkubwa katika kuifundisha ama kuionya jamii.

Kisiasa, sekta hii hutumika kama baraza la midahalo na majadiliano kwenye jamii. Na kiuchumi, sekta hii huchangia pato kubwa la mabilioni ya pesa na pia ni chanzo cha mamilioni ya ajira duniani.

Uchambuzi wa John Kitime



Mwanamuziki mkongwe na mchambuzi wa sanaa, John Kitime

Kufuatia viwango duni vinavyooneshwa na wasanii wa Kitanzania katika nyanja nyingi,  John Kitime ametoa makala kupitia mtandao wa "Wahapahapa" BOFYA HAPA wenye kichwa cha habari: 2010 Ukungu Bado Mwingi. Makala hii nimeiweka hapa kwa kuwa nadhani ni muhimu ikaendelea kusomwa kupitia vyanzo mbalimbali.

Tunaanza mwaka, kuna wanaofurahi kuna wanaowaza itakuwaje mwaka huu. Kuna wanaoona mwaka huu kuwa wa uhakika katika mafanikio, kuna wanaoogopa hata kuanza mwaka. Katika sanaa naona ukungu bado mzito.

Sep 21, 2010

Uzinduzi wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF)

 Umati wa watu waliohudhuria uzinduzi huo

Shirikisho la Filam Tanzania (TAFF) lilizinduliwa rasmi katika viwanja vya Leaders Club siku ya Jumamosi Septemba 18, 2010 na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, wasanii wa filamu na wadau mbalimbali.

Akifungua tamasha hilo Rais wa Shirikisho, Saimon Mwakifamba maaruf kama Jaspa alianza kwa kutoa shukurani kwa serikali kwa kulitambua Shirikisho la Filamu na kazi yao ya kwanza itakuwa ni kutetea maslahi ya wasanii na wadau wote katika tasnia ya filamu kwani mapato wanayopata ni kidogo sana na hayaendani na ugumu wa kazi husika. Vile vile Jaspa alisema kuwa wao kama TAFF wamedhamiria kuanzisha tamasha la filamu litakalojulikana kama Nyerere Film Festival na litaanza mwaka huu litakapofanyika kwa mara ya kwanza hapo Disemba.


Ripoti ya warsha ya TAIPA


Yustus Mkinga, Mtendaji Mkuu wa Cosota

TAARIFA YA WARSHA KUHUSU WIZI WA KAZI ZA SANAA ILIYOFANYIKA UKUMBI WA KITUO CHA UTAMADUNI CHA UFARANSA ALHAMISI TAREHE 19 AGOSTI 2010

Chama cha Watengeneza Filamu na Vipindi vya Luninga na Radio (TAIPA)/UMOJA AUDIOVISUAL E.A. LTD/ na KITUO CHA UTAMADUNI CHA UFARANSA (ALLIANCE FRANCAISE), waliandaa warsha juu ya WIZI WA KAZI ZA SANAA “COPYRIGHT INFRINGEMENT (PIRACY)” iliyofanyika siku ya Alhamisi tarehe 19 Agosti 2010 kuanzia saa 3 asubuhi katika ukumbi wa Kituo cha Utamaduni cha Ufaransa.

Serikali ina dhima ya kuokoa sekta ya filamu-2


Msanii nyota wa kike wa filamu za Bongo, Irene Uwoya

Ninapatashida kidogo kutokana na ukweli kwamba watengenezaji wa filamu wanaoinukia na hata wengi waliopo kwenye soko hili hapa nchini kukosa mfumo mzuri wa kuwawezesha kupata msaada wa mitaji (financials pring board) kwa kazi zao. Hata hivyo, kwa mtazamo wangu, nashauri serikali ijayo kuangalia kwa makini jinsi tunavyoandaa miundo ya kihazina (funding structure) katika kampuni na kazi zetu kabla haijaamua kuelekeza nguvu zake katika kusaidia sekta hii.

Endapo ningepata nafasi ya kuwa mshauri wa Rais katika masuala yanayohusu sekta ya filamu; ningemuomba afikirie sana kuhusu serikali yake kuanzisha mpango maalum wa kutoa mikopo/ruzuku kwa watengenezaji wasinema ambao hawafikiriwi kabisa na mabenki yetu.

Serikali ina dhima ya kuokoa sekta ya filamu


Rais Jakaya Kikwete

Kwanza napenda kumshukuru Rais Jakaya Kikwete kwa angalau kuonesha kuutambua mchango wa sekta ya filamu Tanzania. Hii ni sekta ambayo bado imeonekana kupewa kisogo na hivyo kubaki mikononi mwa wajasiriamali wadogo wasio na mitaji. Haionekani kama nayo inatakiwa kupewa kipaumbele (politicalvaluable) kama sekta muhimu inayoweza kuchangia pato kubwa kwa maendeleo na ukuaji wa uchumi wataifa letu.

Sekta ya Filamu hapa Tanzania haifikiriwi sana kuwa ni taaluma adimu, ndio maana haipewi kipaumbele katika kamati za mipango serikalini. Pia  sekta hii yaweza kuwa mwangamizaji na mchochezi mkubwa katika jamii ya kidemokrasia na pengine kuwa mwasilisha taarifa potofu.