Aug 31, 2016

Bongo Movies: Bado tuna tatizo kubwa katika uandishi wa filamu

Mwandishi wa makala haya, Bishop Hiluka, katika moja ya kazi za uandishi wa filamu

FILAMU ni chombo muhimu sana cha mawasiliano katika jamii na ustawi wa nchi yoyote, huchangia kupatikana kwa ajira kwa vijana, huchangia ukuaji wa uchumi wa nchi, husaidia kuwaambia watu wengine kuhusu hadithi za jamii husika, huchangia maendeleo ya nchi na kadhalika.

Utengenezaji wa filamu si suala la mzaha, si jambo la mtu ambaye jana usiku alilala akiwa hana kazi ya kufanya na leo asubuhi kaamka akiwa na wazo la kutengeneza filamu, bila kuwa na ujuzi, nyenzo wala mtaji wa kutosha. Utengenezaji filamu ni jambo linalohitaji gharama, ni jambo la hatari (venture) linalohitaji muda mwingi na mtengenezaji wa filamu hatakiwi kuwa mvivu wa kufikiri au kupoteza muda akipiga soga na rafiki zake au kufanya mizaha.