Mkurugenzi wa Utamaduni wa Wizara ya Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo, Prof. Hermas Mwansoko, akiongea
jambo katika moja ya shughuli za Idara yake
BAADA ya uhuru Disemba 1961,
Serikali iliunda Wizara ya Utamaduni wa Taifa na vijana, mwaka 1962, Mwalimu
Julius Nyerere alitamka wazi kuwa Utamaduni ni kiini na roho ya Taifa, nchi
inayokosa utamaduni wake ni sawa na mkusanyiko wa watu usiokuwa na roho na
hivyo kukosa sifa ya kuitwa taifa kamili.
Lakini chakushangaza pamoja na umuhimu uliopo katika suala la utamaduni kwa maisha ya watu, bado sera ya utamaduni imepewa nafasi finyu katika serikali yetu tangu ilipoanzishwa wizara ya kushughulikia masuala ya sanaa. Katika kipindi chote tangu mwaka 1962, shughuli za sanaa zilipewa nafasi katika mfumo wa kiserikali lakini zimekuwa hazithaminiwi.
Lakini chakushangaza pamoja na umuhimu uliopo katika suala la utamaduni kwa maisha ya watu, bado sera ya utamaduni imepewa nafasi finyu katika serikali yetu tangu ilipoanzishwa wizara ya kushughulikia masuala ya sanaa. Katika kipindi chote tangu mwaka 1962, shughuli za sanaa zilipewa nafasi katika mfumo wa kiserikali lakini zimekuwa hazithaminiwi.