Apr 27, 2018

Sanaa ina mchango mkubwa katika maendeleo ya nchi


Sanaa za Tanzania
KATIKA ulimwengu wa kimaada unaodhibitiwa na fikra za kupenda dunia, thamani za utamaduni (sanaa ikiwemo ndani yake) huwa hazipewi nafasi na siku zote utajiri wote wa sanaa unapimwa kwa fedha.

Suala muhimu katika ulimwengu huo ni fedha, kwa hivyo kila kitu kinapimwa thamani yake kwa kuangalia kitaingiza kiasi gani cha fedha.

Utaona inatazamwa elimu fulani itaingiza fedha kiasi gani, inaangaliwa kazi fulani ina uwezo wa kuingiza kiasi gani cha fedha na vitu kama hivi. Lakini hali haiko hivyo katika upande wa utamaduni.

Hapana, kwani elimu ni njia ya kuwa na maisha bora, na sanaa ni chombo cha kuwa na ustawi katika maisha.

Muungano wetu na utamaduni wetu


JANA Aprili 26, Tanzania iliadhimisha miaka 54 ya Muungano tangu nchi zilizoitwa Tanganyika na Zanzibar zilipoungana na kuzaa Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania. Nchi hizi mbili yaani Tanganyika (sasa Tanzania Bara) na Zanzibar (inayojumuisha Visiwa vya Pemba na Unguja) ziliungana Aprili 26, 1964.

Jahazi linalowabeba Watanzania limeweka historia ya kung’oa nanga mara baada ya Jamhuri Muungano wa Tanzania kuzaliwa rasmi.

Hii ilitokana na ujasiri, ushupavu na nia ya dhati waliyokuwa nayo waasisi wa Muungano huu: Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (Tanganyika) na Abeid Aman Karume (Zanzibar).
Tanzania ni nchi, watu wake mmoja mmoja huitwa Mtanzania na kwa ujumla wao wanaitwa Watanzania, hivyo kuunda taifa la Tanzania.

Apr 25, 2018

Tuzuie teknolojia isikwapue haki za wasanii



Wakati Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEKNOHAMA) ikizidi kuimarika na kuchukua nafasi ya njia kongwe za mawasiliano, tasnia ya ubunifu nayo inajikuta kwenye changamoto ya kuakisi mabadiliko hayo ya wakati.

Tasnia ya ubunifu (Sanaa) ni hazina muhimu sana inayohifadhi kazi ya uumbaji; ambapo wabunifu (wasanii) wanayo dhamana ya kueneza ujumbe na elimu kwa jamii.

Tasnia hii ni mjumuiko wa hakimiliki bunifu ambazo zinapaswa kulindwa ili jamii iendelee kunufaika na kazi hizi za ubunifu, ambazo sasa zimeenea duniani kote.

Apr 18, 2018

Kusambaza video chafu, wasanii wanaelekea kubaya

Wasanii Nandy na Bill Nass katika clip ya video chafu iliyoenea mtandaoni


Hamisa Mobeto
INASHANGAZA sana! Katika kipindi ambacho Sheria za mitandaoni zimetungwa ili kudhibiti matumizi ya mitandao hiyo, ndipo mdudu mbaya sana wa video chafu kaingia katika tasnia nzima ya burudani.

Kabla ya huu mtindo mpya wa video zinazodhalilisha utu tumekuwa tukishuhudia jinsi wasanii wa kike wanavyokuwa nusu watupu kitu kinachosemwa eti ndiyo maendeleo (kupiga hatua), na pengine inabainishwa kuwa hiyo ndiyo dalili ya kuwepo kwa mafanikio katika tasnia hii.

Sakata la Diamond, Nandy:Tusipojipanga dunia itatupanga

Wanamuziki Nandy na Bill Nass katika pozi
Diamond Platnumz
KAMA mtafiti, mchambuzi, mdau wa sanaa na mwananchi wa nchi hii nimekuwa nikiitahadharisha jamii yangu kuhusu vita vinavyoendelea duniani kati ya mataifa makubwa na mataifa machanga.

Lakini hivi si vita kama vile vinavyoendelea huko Syria, wala si vita vya kupinga ugaidi n.k. la hasha! Bali ni vita vya kiutamaduni, vya kutawalana kiakili.

Vita vya utamaduni huenezwa kupitia vyombo vya habari ikiwemo mitandao, televisheni, redio, magazeti, sinema, muziki n.k. ambavyo ni jukwaa muhimu sana katika kueneza utambulisho, utamaduni na fikra za nchi husika.

Apr 13, 2018

Tuwafundishe watoto umuhimu wa michezo ya pamoja



MICHEZO ni chombo cha kuwasilisha tunu msingi katika kuboresha ubinadamu na katika ujenzi wa jamii ya amani na ya kindugu.

Michezo ina faida kubwa sana kwa mwanadamu, siyo kwa wachezaji tu bali hata kwa wanaoshabikia ambao kufurahi kwao huwa ni kinga dhidi ya maradhi, hasa inapokuwa michezo ya ushindani.

Ni wazi kuwa matatizo mengi ya kiafya kwa wanadamu yanaongezeka siku hizi kutoka na mfumo mpya wa maisha tunayoishi ukilinganisha na miaka ya nyuma. Ingawa kwa wale wanaoshiriki michezo mbalimbali mara nyingi imewasaidia kuepuka matatizo hayo.

Apr 12, 2018

Sanaa ina nafasi kubwa katika jamii

Wasanii wa kizazi kipya wanaounda kundi la Tanzania All Stars wakiwa katika sherehe za maadhimisho ya miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania Bara

UHAKIKA wa sanaa – iwe sanaa yoyote ile – ni kipaji kutoka kwa Mungu, ni hazina muhimu sana inayohifadhi kazi ya uumbaji.

Ijapokuwa kudhihiri kwa sanaa kunatokana na jinsi sanaa yenyewe itakavyobainishwa, lakini huo si uhakika wote wa sanaa. Kabla ya kubainishwa, kuna hisia na utambuzi na udiriki wa sanaa yenyewe na kwamba mambo yote yanachimbukia hapo.

Baada ya kuonekana, kutambuliwa na kubainishwa uzuri, unyofu na uhakika wa sanaa, hapo ndipo zinapoweza kuzuka maelfu na nukta ndogondogo na nyembamba sana ambazo baadhi ya wakati hawawezi kuziona nukta hizo isipokuwa wasanii wenyewe.