Oct 27, 2010

FILAMU ZA KITANZANIA: Ni kweli tuna wakosoaji wa filamu? (4)

Mwandishi wa makala haya, Bishop J. Hiluka

SIKU nilipopigiwa simu na mhariri wa gazeti hili akinitaka tuonane sikufikiria kabisa kama angenikabidhi jukumu la kuandika makala kwenye gazeti lake. Sikufikiria kwa sababu sikudhani kama angeweza kunifikiria mimi niandike badala ya wachambuzi wengi maarufu na wa muda mrefu waliopo ambao tayari wameshajijengea heshima kubwa katika uandishi.

Nilisita sana kukubali kwa kuwa sikudhani kama ningeweza kukidhi kiu ya wasomaji, lakini nilipokumbuka uzalendo wangu na kiu yangu ya kutaka tasnia ya filamu hapa Tanzania ikue nikakubali mara moja.

FILAMU ZA KITANZANIA: Ni kweli tuna wakosoaji wa filamu? (3)

 Darasa la ufundishaji wa mafunzo ya filamu (workshop in filmmaking)

NI Ijumaa nyingine, naamka asubuhi na mapema, nawahi usafiri wa kuelekea Posta, kisha naelekea Upanga ambako kipo kituo cha utamaduni cha Ujerumani (Goethe Institut) kunakofanyika mafunzo ya utengenezaji wa filamu (workshop in filmmaking). Mafunzo yaliyoanza wiki mbili zilizopita na yanahitimishwa leo. Mimi ni mmoja wa vijana waliochaguliwa kuhudhuria mafunzo hayo ya nadharia na vitendo yanayoendeshwa na wataalamu waliobobea katika tasnia ya filamu kutoka Ujerumani na Ufaransa kwa ushirikiano wa balozi za Ujerumani na Ufaransa, na kuratibiwa na Goethe Institut na Alliance Francaise.

FILAMU ZA KITANZANIA: Ni kweli tuna wakosoaji wa filamu?

 Florian Lawrence Mtaremwa, mmoja wa watengeneza filamu wa Kitanzania

TASNIA ya filamu ni sekta muhimu sana kwa maendeleo ya taifa lolote. Ni muhimu kwa sababu kubwa tatu; filamu na maigizo hutumika kama mwasilisha taarifa mkubwa katika kuifundisha ama kuionya jamii.

Kisiasa, sekta hii hutumika kama baraza la midahalo na majadiliano kwenye jamii. Na kiuchumi, sekta hii huchangia pato kubwa la mabilioni ya pesa na pia ni chanzo cha mamilioni ya ajira duniani.

Uchambuzi wa John Kitime



Mwanamuziki mkongwe na mchambuzi wa sanaa, John Kitime

Kufuatia viwango duni vinavyooneshwa na wasanii wa Kitanzania katika nyanja nyingi,  John Kitime ametoa makala kupitia mtandao wa "Wahapahapa" BOFYA HAPA wenye kichwa cha habari: 2010 Ukungu Bado Mwingi. Makala hii nimeiweka hapa kwa kuwa nadhani ni muhimu ikaendelea kusomwa kupitia vyanzo mbalimbali.

Tunaanza mwaka, kuna wanaofurahi kuna wanaowaza itakuwaje mwaka huu. Kuna wanaoona mwaka huu kuwa wa uhakika katika mafanikio, kuna wanaoogopa hata kuanza mwaka. Katika sanaa naona ukungu bado mzito.