Dec 28, 2011

ILI KUDUMISHA MAADILI: Kanuni za sheria ya filamu sawa, lakini ada zinatia shaka! KULIKONI DESEMBA 30, 2011

Mwenyekiti wa Bodi ya Ukaguzi wa Filamu
na Michezo ya Kuigiza, Rose Sayore

Katibu Mtendaji wa Bodi, Joyce Fisso

MIAKA ya karibuni tasnia ya filamu imekuwa ndiyo kimbilio kubwa, chanzo cha ajira na njia ya kujikwamua kiuchumi kwa wasiojiweza au walioshindwa katika fani zingine. Jambo hili limesababisha kuwa na watendaji wasio na uwezo wala taaluma na hatimaye kuzalishwa filamu mbovu zisizokidhi viwango.

Kama mdau na mwanaharakati wa sanaa, mara nyingi nimekuwa nikishauri kuwa tuboreshe kazi zetu na kubadili mtazamo/ dhana iliyojengeka miongoni mwetu kuwa sanaa ya filamu ni kimbilio la wasiojiweza kiuchumi. Na kutambua kuwa sanaa hii ni kazi kama kazi nyingine ambayo inahitaji ubunifu, akili, maarifa na

Dec 27, 2011

Hatimaye Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) lapata viongozi kidemokrasia

Rais mteule, Simon Mwakifwamba

Makamu wa Rais, Suleiman Ling'ande

Viongozi wapya na wajumbe wa Bodi ya TAFF katika
picha ya pamoja, muda mfupi baada ya kuchaguliwa

Baada ya kuwepo kwa uongozi wa mpito, hatimaye siku ya Alhamisi Desemba 22, 2011, Shirikisho lilipata viongozi wapya kwa njia ya kidemokrasia watakaoongoza kwa kipindi cha miaka mitatu hadi 2014.



Simon Mwakifwamba aliyekuwa rais wa mpito ndiye aliyechaguliwa kuwa Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania baada ya kupita kwa kishindo kwa kupata kura zote 18 za wajumbe waliopiga kura baada ya kuwa mgombea pekee mwenye sifa za kugombea nafasi hiyo kwa mujibu wa katiba ya shirikisho.

Dec 21, 2011

TAFIDA: Viongozi waliochaguliwa wana kazi ngumu kupigania weledi

Mwenyekiti wa Tafida, Paul Mtendah

Makamu Mwenyekiti wa Tafida, John Lister Manyara

Viongozi wapya wa Tafida katika picha ya pamoja na
wanachama wa Chama cha Waongozaji Filamu Tanzania,
picha hii ilipigwa muda mfupi baada ya kumalizika uchaguzi

MWISHONI mwa wiki iliyopita, Jumapili ya tarehe 18 Desemba, 2011 kulikuwa na uchaguzi wa viongozi wa kitaifa wa Chama cha Waongozaji wa Filamu Tanzania (Tanzania Film Director’s Association “TAFIDA”), ambapo uongozi mpya uliochaguliwa siku hiyo uliashiria mwanzo mpya wa kuchipua tasnia ya filamu hasa kwa waongozaji wa filamu katika tasnia yetu. Nasema ni mwanzo mpya kwa kuwa nina imani na viongozi wapya waliochaguliwa ambao kwa kiasi kikubwa ninawafahamu kwa uchapakazi wao na kujituma.



Mwanzoni Chama cha Waongozaji wa Filamu Tanzania kilipoanzishwa na kupewa usajiri wa kudumu na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata),

Dec 20, 2011

Viongozi wapya wa Chama cha Waandishi wa Script Tanzania (Tanzania Scriptwriters Association)

Kimela Billa, Makamu Mwenyekiti 

Ramadhani Kingaru, Mjumbe 

Christian Kauzeni, Mjumbe

Hawa ndiyo viongozi waliochaguliwa kuongoza taasisi ya waandishi wa miswaada andishi ya filamu (script) kwenye uchaguzi ngazi ya taifa (Tanzania Scriptwriters Association - TASA) uliofanyika jana Jumatatu tarehe 19/12/2011 pale Vijana Social Hall - Kinondoni:

- Abdul Maisala                     Mwenyekiti
- Kimela Billa                         Makamu Mwenyekiti
- Samwel Kitang’ala             Katibu
- Subira O.Nassor Chuu       Mweka Hazina
- Mike Sangu                         Mjumbe
- Dimo Debwe                       Mjumbe

Dec 14, 2011

Kwa hili, Tanga wamedhihirisha kuongoza jahazi la filamu nchini

Mwl. Kassim El-Siagi akizungumza na wananchi
waliohudhuria tamasha hilo muda mfupi kabla
tamasha halijaanza

Nikiwa katika picha na wadau wa filamu jijini Tanga, 
katikati ni Amri Bawji (mwenye baragashia) na kulia ni
Nassib Ndambwe, mmoja wa waandishi wa script nchini

WIKI iliyopita nilitembelea jiji la Tanga wakati wa tamasha la filamu za Kiswahili zilizotengenezwa mkoani Tanga. Tamasha hilo liliandaliwa na kampuni ya El-Siagi Movies na kudhaminiwa na StarMedia kampuni ya ving'amuzi vya StarTimes, na Nyumbani Hotels & Resorts kupitia vinywaji vyake vya Bavaria. Jiji la Tanga ndilo wanaloishi watu ninaopenda kuwaita “magwiji wa filamu nchini”, kama ambavyo nimewahi kuandika katika makala zangu kadhaa zilizopita.


Kwa nini nawaita watu hawa magwiji wa filamu? Kwa sababu ndiyo watu pekee waliothubutu kuandaa filamu za kibiashara katika miaka ya 1990 japo mazingira yalikuwa magumu sana; wakati huo hakukuwa na mahala pa kuuzia filamu, hata uoneshaji sinema kwenye majumba ya sinema ulikuwa ukisuasua kutokana na kuingia kwa vituo vya televisheni, na sinema zilizotawala nchini zilikuwa za Kihindi.


Ni filamu ya “Shamba Kubwa” (1995) iliyotungwa na kuongozwa na Mwl. Kassim El-Siagi wa Tanga ndiyo iliyofungua milango ya filamu za kibiashara nchini. Kwa walio wengi pengine watanishangaa kwa kuwa hawajahi kuiona filamu hii kwa kuwa wakati ule ilioneshwa kwenye majumba ya sinema; Majestic Cinema – Tanga, Emipre Cinema – Dar es Saalaam, Metropole Cinema – Arusha, na kadhalika.


‘Shamba Kubwa’ ndiyo filamu iliyowaibua wasanii ambao baadaye wamekuwa mahiri katika ulimwengu wa filamu, kama Hassan Master, Jimmy Master, Kaini na Amina Mwinyi, ni filamu hii iliyoteka wengi kwa wakati ule japo teknolojia ilikuwa bado ndogo sana ukilinganisha na hivi sasa.


Filamu hii na nyingine zilizofuata kama ‘Love Story Tanganyika na Unguja (1998)' ya Amri Bawji, ‘Kifo Haramu’ ya Jimmy Master, ‘Dunia Hadaa (2000)' ya Mwl. Kassim El-Siagi, na ‘Augua (2002)' ya Amri Bawji, zote zikitengenezwa na magwiji kutoka Tanga zilitengenezwa katika mfumo wa VHS (analogy), na hata uhariri wake ulitumia akili zaidi kutokana na teknolojia ya wakati huo kuwa ya kiwango kidogo, lakini zilivutia sana kutokana na maudhui na msuko mzuri wa hadithi.


Tanga pia ndiyo mkoa wa kwanza kuanzisha chama ili kukabiliana na changamoto za tasnia ya filamu. Walianzisha Chama cha Watengeneza Filamu wa Tanga (Tanga Film-Makers Association “TAFMA”), wakati huo hata ile filamu ya Girlfriend inayojulikana kwa wengi ilikuwa haijatungwa.

Dec 12, 2011

Filamu za bajeti ndogo

Unataka kuandaa filamu, lakini huna pesa ya kutosha… 

Watengeneza filamu na waandishi wakiwa kwenye semina
iliyoandaliwa na MFDI - Tanzania

TASNIA ya filamu nchini inakua kwa kasi na kuwa kimbilio la vijana wengi, lakini bado tasnia hii imekuwa ikikumbana na changamoto kubwa katika kufikia ubora unaokubalika kimataifa kwenye filamu zetu. Hata wakosoaji wa filamu wamekuwa wakijaribu kukosoa kwa kuilinganisha tasnia hii na tasnia nyingine zilizoendelea kama Hollywood, Bollywood, tasnia ya filamu ya Afrika Kusini na nyinginezo lakini wakasahau kuwa bado tuna mambo makubwa tunayotofautiana.

Katika tasnia za filamu zilizoendelea, mara nyingi huwa zimegawanyika katika mikondo mikuu miwili; mainstream film ambayo pia hujulikana kama major movies studio, na independent film au huitwa kwa kifupi Indies.