Nov 30, 2010

Jukwaa la Sanaa Basata: Michuzi ahamasisha wasanii kujiunga na mtandao jamii

Muhidin Issa Michuzi akionesha namna mtandao wa youtube unavyofanya kazi

MUHIDINI Issa Michuzi, ambaye ni mwandishi wa habari mwandamizi nchini amewashauri wadau wa sanaa hasa wasanii kuingia kwenye matumizi ya teknolojia ya mtandao jamii ili kujitangaza na kuuza kazi za sanaa duniani kote.

Akizungumza kwenye Jukwaa la Sanaa jana, jukwaa ambalo hufanyika kila Jumatatu kwenye ukumbi wa Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), Ilala Shariff Shamba jijini Dar,

Nov 24, 2010

Mwalimu Nyerere Film Festival kuwakomboa wasanii wetu

Simon Mwakifwamba akihojiwa na 
mtangazaji wa Clouds TV, Zamaradi Mtetema

INAONEKANA kuwa Shirikisho la filamu Tanzania lina mikakati kabambe ya kuikomboa tasnia ya filamu nchini dhidi ya changamoto mbalimbali zinazoikabili. Baadhi ya changamoto hizo ni kuwafanya wasanii wa Tanzania kuwa na maisha bora na pia kuwawezesha kufanya kazi zenye ubora na zinazokubalika ndani na nje ya nchi.

Mikakati hiyo ni pamoja na kuhakikisha sheria ya hakimiliki na hakishiriki inaangaliwa upya, kupambana na maharamia wa kazi za sanaa, kujenga mtandao mpana wa ushirikiano baina ya wadau, kuimarisha uongozi wa vyama mbalimbali vya wadau,

Nov 23, 2010

HISTORIA YA FILAMU 2: Kuibuka kwa ukoo wa Lumiere



Ndugu wawili, Auguste na Louis Lumière

Mwaka1895, nchini Ufaransa ndugu wawili Auguste na Louis Lumière (tamka lumia) walifanikiwa kutengeneza kifaa cha kupigia picha chenye viambatanisho vitatu ndani yake: camera, printer, na projector.

Mwishoni mwa mwaka 1895 jijini Paris, Antoine Lumière ambaye ni baba wa Auguste na Louis alifanya onesho la sinema kwa malipo, huo ndiyo ukawa mwanzo wa kukua kwa sekta hii na soko la filamu (kwa mujibu wa Cook, 1990).

Serikali imeombwa kuinua vipaji

Lisa Jensen

Serikali kupitia baraza lake la sanaa (Basata) imetakiwa kuinua vipaji vya wasanii nchini kwa kuweka wawakilishi kwenye ofisi zake za kibalozi zilizoko nje. Ushauri huo ulitolewa na msanii na mwanaharakati wa sanaa, Lisa Jensen, katika mkutano unaowakutanisha wadau mbalimbali wa sanaa kila Jumatatu, safari hii walikuwa wakijadili kuhusu fursa za wasanii.

Lisa Jensen ambaye aliwahi kuwa mrembo wa Kanda ya Ziwa na mrembo namba tatu wa Tanzania alieleza kuwa tatizo linalokwamisha taaluma hiyo ni kukosa msukumo wa serikali kwani imebainika kuwa wasanii wa Tanzania wanapokuwa nje ya nchi wanakosa maslahi mengi kutokana na uwakilishi mbovu kutoka balozi zilizoko nje.

Aidha wasanii wametakiwa kuungana pamoja ili kuikuza tasnia hiyo ya ubunifu ili kutoa nguvu kwa wadau wote wa sekta hiyo na kuiomba serikali kuipa kipaumbele.

Nov 19, 2010

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) latoa lawama kwa waandishi wa habari

 Mzee Omari Mayanga akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani)

Bango la Jukwaa la sanaa

Gonche Materego, Katibu Mtendaji wa Basata akifafanua kwenye Jukwaa la Sanaa

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limewaangushia lawama waandishi wa habari nchini kuwa wamekuwa wakisusia vikao vya Jukwaa la Sanaa vinavyofanyika kila Jumatatu katika ukumbi wa Baraza. Lawama hizo zimetolewa na mwakilishi wa baraza hilo, Mzee Omari Mayanga alipokuwa akiliwakilisha baraza hilo wakati viongozi wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) walipokuwa wakielezea mikakati yao kwa waandishi wa habari kuhusiana na tamasha la filamu la Mwalimu Nyerere.

Mwalimu Nyerere Film Festival ni Februari 2011

 Rais wa TAFF, Simon Mwakifwamba akitoa ufafanuzi,
pembeni yake ni Katibu Mkuu, Wilson Makubi
Katibu Mkuu wa TAFF, Wilson Makubi akifafanua jambo

Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) limetangaza rasmi tarehe ya tamasha la filamu la Mwalimu Nyerere. Kwa mujibu wa rais wa shirikisho hilo, Simon Mwakifwamba, shirikisho hilo litakuwa linaendesha tamasha la filamu za Tanzania kila mwaka, na litafanyika kwa mara ya kwanza mwezi februari mwakani, 2011.

Rais wa shirikisho alisema hayo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini kwenye ukumbi wa Baraza la sanaa la taifa (Basata) jana Alhamisi, tarehe 18 Nov, 2010 na kubainisha kuwa lengo lao ni kukuza soko la kazi za filamu nchini na kukuza mahusiano ya kisekta kati ya wasanii wa tanzania na wale wa nje ya nchi.

Nov 16, 2010

Historia ya Filamu duniani

Zoöpraxiscope

FILAMU (Motion picture film), au wengine hupenda kuita picha jongefu zimekuwepo kwa zaidi ya miaka mia, historia ya filamu inaanzia mwishoni mwa karne ya 19. Filamu zimepitia hatua kwa hatua hadi kufika hapa zikianzia kwenye mawazo yaliyoonekana mapya hadi kuwa nyenzo muhimu ya mawasiliano na burudani, na hata kuwa mwasilisha taarifa katika karne ya 20 na ya 21. Filamu pia zina athari kubwa (substantial impact) kwenye sanaa, teknolojia, na siasa.

Machapisho mbalimbali yamekuwa yakiwataja ndugu wawili, Auguste na Louis Lumière (tamka Lumia) wa Ufaransa kama waasisi wa filamu duniani na kumsahau William Kennedy Laurie Dickson (WKL Dickson) aliyekuwa injinia mkuu katika kampuni ya Edison Laboratories ya Marekani.

Nov 10, 2010

Rais Kikwete, kazi rasmi ya kuiokoa tasnia ya filamu ni sasa

Rais Jakaya M. Kikwete

KWANZA napenda kukupongeza, Rais Jakaya Kikwete kwa kuchaguliwa tena kuliongoza taifa hili kwa kipindi kingine cha miaka mitano. Pia nakushukuru angalau kwa kuonesha kuutambua mchango wa sekta ya filamu Tanzania. Katika hotuba yako ya kuvunja bunge la tisa uliyoitoa huko Dodoma tarehe 20 Julai 2010, chini ya kipengele cha “Michezo, Burudani na Utamaduni”, ulinukuliwa ukisema, pamoja na mambo mengine kwamba: “...Hivi sasa tumelipia mtaalamu mshauri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam asaidie kutengeneza njia bora ya kusambaza kazi za wasanii wa muziki na filamu ili wapate malipo halali kwa jasho lao. Mafanikio ya zoezi hili yatatufundisha namna ya kuwasaidia wasanii wa fani nyingine pia...”

Ikumbukwe kuwa kwa miaka mingi sasa, wasanii na watengenezaji wa sinema miongoni mwa wadau wengine wa sanaa wameendelea kutoa sinema hapaTanzania ili kujipatia riziki kutokana na kazi yao bila mafanikio. Ingawaje sekta ya filamu ni sekta yenye thamani ya mabilioni ya  fedha, wengi wameishi na kufa maskini.

Rais, serikali yako inapaswa ibadilishe mtazamo wake kuhusu wizi wa sanaa na nakala zisizo halali (pirated copies). Mambo haya lazima iyaone kama wizi na ipinge wizi kwa nguvu zote kama inatarajia kuona taaluma hii ikinawili na kuwaajili vijana wengi na hivyo kuchangia katika kuinua uchumi wa taifa letu. Ieleweke kuwa ni kosa la jinai kuuza au kununua kazi feki, kama ilivyo kwa nchi nyingi zilizofanikiwa katika tasnia hii.

 Cover ya sinema ya Miss Bongo

Taaluma hii haiwezi kukua kama viongozi wataishia kusema tu bila kutekeleza huku kukiwa na mambo mengi yanayoirudisha nyuma. Binafsi nimetumia miaka kadhaa kujifunza na kufanya tafiti mbalimbali kuhusu historia ya filamu, matatizo makubwa katika tasnia hii, mfumo unaofaa kutumika katika tasnia ya filamu na mambo mengine mengi, kutoka na na haya, naweza kukuhakikishia kwamba sekta ya filamu Tanzania ina thamani ya bilioni 200 ya pesa za Tanzania katika biashara, kama tu serikali yako itatilia mkazo na kutoa msaada unaohitajika.

Filamu za Kibongo zinavyoibwa nje ya nchi

Moja ya filamu za Kitanzania, Black Sunday

Filamu ya One by One iliyotengenezwa na Mahsen Awadh, "Cheni" 

Kwa inasikitisha sana kuona wasanii na watengeneza filamu wa Kitanzania wanavyohangaika kujitengenezea sinema kwa pesa za kubangaiza au pengine za mkopo wakitegemea kuuza na kupata faida itakayowawezesha kupiga hatua kimaisha lakini inatokea kwamba watuwengine wanawaibia. Tena inauma sana endapo mtu huyo anayeiba ni tajiri mkubwa.

Nov 9, 2010

Uandishi ni Sanaa adimu


 Bishop J. Hiluka


Kipaji cha uandishi huanza tangu ukiwa mtoto 
hasa kama unapenda kujisomea kama 
mtoto huyu, Magdalena J. Hiluka

IMEANDIKWA kuwa; “hapo mwanzo palikuwepo na neno,” lakini unapoongelea burudani (entertainment industry) imesemwa; “hapo mwanzo palianza na wazo.” Wazo linaweza kukujia katika njia mbalimbali, linaweza kukufikia kutoka kwa mtu yeyote, mahali popote, wakati wowote. Wazo linaweza kuanzia kwa mwandishi, mtayarishaji wa sinema; linaweza kupitia kwa muongozaji wa sinema au mwigizaji. Linaweza hata kuanzia kwa msomaji wa makala, rafiki, ndugu, jamaa au jirani yako.

Wazo linaweza kumfikia yeyote hata anapokuwa akifanya kazi, akifanya mazoezi, akikimbia, akiongea au akiwa kajipumzisha nyumbani anasoma makala hii. Ni ajabu sana; eti wakia (ounce) chache katika ubongo wa mwanadamu huweza kufanya na kuleta mabadiliko au maendeleo makubwa kama tunayoyashuhudia wakati huu wa sayansi na teknolojia.

Nov 3, 2010

Tasnia ya Filamu: Tunamuenzi vipi Mzee Kawawa?

Mzee Rashid Mfaume Kawawa

NAKUBALIANA na maneno kwamba; wasanii ni watu wenye akili nyingi sana. Msanii (wa aina yoyote) ni mtu mbunifu, mwenye uwezo wa kuumba jambo likakubalika kwenye jamii, na ni mtu anayefanya tafiti za kina katika fani yake. Wasanii wanaweza kuwa viongozi wazuri wakiingia kwenye siasa; mojawapo ya waigizaji maaruf walioingia kwenye siasa na kuongoza ni pamoja na Ronald Reagan, Rais wa Marekani (1980-1988), na Arnold Schwarzenegger, gavana wa jimbo tajiri la California.