Sep 28, 2011

Tatizo la usambazaji filamu linasababishwa na makundi

 Kulwa Kikumba (Dude)

Jacqueline Wolper

 Issa Mussa (Claude)

IMEKUWA ni kawaida katika tasnia ya filamu kuwasikia wasanii au watayarishaji wa filamu nchini kuulalamikia mfumo wa soko la filamu uliopo, hasa katika hili sakata linaloendelea hivi sasa kati ya wale walio chini ya Shirikisho la Filamu na Msambazaji mmoja mwenyewe nguvu anayelalamikiwa kuhodhi soko la filamu, ingawa ni haki yake kujipangia mfumo anaodhani utamsaidia kuuza kazi zake kwani hakuna mtu anayefanya biashara kwa ajili ya mtu mwingine.

Jina la kampuni na msambazaji anayelalamikiwa vimekuwa vikitajwa sana kila mara wanapokusanyika wasanii na watayarishaji wengi wa filamu nchini ambao wamekuwa wakiwatupia lawama wasambazaji hao wa kazi zao kwa madai kuwa,

Sep 21, 2011

Chama cha Waongozaji wa Filamu Tanzania wameonesha njia sahihi

Mwenyekiti wa Tafida, Christian Kauzeni, 
katika moja ya majukumu yake kwa chama

Amanzi Ali Kisomi, akiwa jukwaani

INGAWA kimekuwa kikionekana kama ni chama cha watu waliokosa kazi ambao hukutana na kupiga porojo pasipo manufaa yoyote, lakini Chama cha Waongozaji wa Filamu Tanzania (Tafida) kimeonesha njia sahihi kwa kuliangalia tatizo lililopo miongoni mwa wanachama wake katika tasnia hii ya filamu na kuamua kujikosoa wenyewe kabla ya kuwakosoa wengine.

Katika kujikosoa, viongozi wa chama hiki, chini ya uongozaji wa Christian Kauzeni, wameandaa mafunzo maalumu ya siku mbili yanayohusu misingi ya uongozaji yanayofanyika katika ukumbi wa Basata, Ilala Sharif Shamba, Alhamisi na kuhitimishwa Ijumaa,

Basata yataka wasanii wote wajisajili

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili Basata, Angelo Luhala

Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) limewataka wasanii pamoja na vikundi mbalimbali vya sanaa kujisajili ili kukomesha wizi wa kazi zao. Akizungumza katika Jukwaa la Sanaa siku ya Jumatatu, ambalo hufanyika kwa kushirikiana na Chama cha Waandishi wa Habari za Sanaa na Utamaduni (CAJAtz), Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili Basata, Angelo Luhala alisema kwa mujibu wa sheria suala la kujisajili ni la lazima, hivyo akasema wasanii wote wanatakiwa kupewa vibali ili waweze kutambulika mahali popote wanapokwenda.

Luhala alisema kuwa wasanii wengi hulalamika kuibiwa kwa kazi zao, pasipo kujua aliyehusika na wizi huo, hivyo usajili ni moja ya kanuni za nchi, kwani taifa linakuwa na kumbukumbu kuhusu kazi zao na pia inamsaidia msanii mwenyewe kuwa huru na kufanya kazi yake kwa imani.

Sep 20, 2011

IJUE BODI YA FILAMU TANZANIA

 Nembo ya Tanzania

 Rose S. Sayore, Mwenyekiti wa Bodi ya Filamu

Merybeatrix Mugishagwe, Mjumbe wa Bodi

HISTORIA YA BODI YA UKAGUZI WA FILAMU TANZANIA

Historia ya bodi ya Filamu nchini Tanzania inaanzia kipindi cha utawala wa kikoloni ambapo mwaka 1930 Sheria ya Picha za Sinema ilitungwa na kuanza kutumika. Mnamo mwaka 1974 Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania lilitunga namba 4 Sheria ya Filamu na Michezo ya Kuigiza na mnamo mwaka 1976 na sheria hiyo ilisainiwa na rais wa wakati huo Mwalimu Julius K. Nyerere.Sheria ambayo ina tumiaka mpaka sasa. Majukumu ya Bodi ni kulinda Utamaduni kwa kuhakikisha kuwa sanaa ya filamu na michezo ya kuigiza inazingatia maadili ya Taifa.

Sep 16, 2011

Tasnia ya filamu nchini ni kama shamba la bibi

 Mwanaharakati wa sanaa nchini, John Kitime

HUWA napata wakati mzuri sana pale ninapopata nafasi ya kukutana na kuwa katika mazungumzo na wadau muhimu wa sanaa hapa nchini na tasnia ya burudani kwa ujumla, na mmoja wao ni mwanaharakati wa sanaa na mtu aliyebobea katika masuala ya hakimiliki nchini, John Kitime, ambaye pia amekuwa akijitolea muda wake mwingi kujaribu kuelimisha wadau wengine kuhusu haki zao na mambo mbalimbali yanayoendelea katika tasnia ya sanaa, jambo ambalo ni nadra sana kufanywa na wengine.

Namheshimu sana Kitime kwa mchango wake na heshima yangu si ile ya kinafiki kama ilivyo kawaida ya Watanzania wengi kutothamini mchango wa mtu anapokuwa angali hai, na husubiri pale anapoaga dunia ndipo hujidai wanamfahamu sana na kumwagia sifa kemkem japo ni haohao waliokuwa wakimponda wakati wa uhai wake.

Sep 14, 2011

Kanisa laipotezea ndoa ya Joyce Kiria



 Ndoa ya kwanza ya Joyce kiria na DJ Nelly


Ndoa ya sasa na Henry Kilewo

Mbunge wa Ubungo John Mnyika pia alikuwepo

Zikiwa zimekatika siku kadhaa toka kufungwa kwa ndoa kati ya presenter wa Kipindi cha Bongo Movies kupitia runinga ya EATV, Joyce Kiria na Katibu wa Chadema Wilaya ya Kinondoni, Henry John Kilewo, Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) kupitia mchungaji wake mmoja (jina limehifadhiwa), limesema ndoa hiyo haitambuliki.

Akizungumza na gazeti moja Jumatano iliyopita jijini Dar, mchungaji huyo alisema kuwa, ndoa ya Joyce inayotambulika ni ile iliyofungwa Desemba 16, 2008 katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheli la Kijitonyama, jijini Dar es Salaam ambako nakala ya cheti  cha ndoa yake imehifadhiwa.

Sep 8, 2011

Ujasiriamali sekta ya filamu umedhoofishwa makusudi...

Hamisi Kibari 



UJASIRIAMALI ni uwezo na nia ya mtu au watu kufikiria, kubuni na kuanzisha fursa mpya za kiuchumi/uzalishaji na kuingia kwenye soko bila kuogopa ushindani au vikwazo vilivyopo au vitakavyoweza kutokea. Mjasiriamali ni mtu mwenye moyo wa kuthubutu, mbunifu, mwerevu wa kubaini na kutumia fursa mbalimbali za kiuchumi, mpenda ufanisi na viwango bora katika kazi ya Sanaa, asiye na tabia ya kuvuruga na kuvunja taratibu za makubaliano na mikataba.

Pia mjasiriamali anasemwa kuwa ni mtu mpenda kutafuta na kupata habari mbalimbali, anayeweka malengo, mwenye kuweka mipango na kufuatilia, asiye tegemezi na anayeamini, na mwenye uwezo wa kushawishi na kuwa na mtandao.

Sep 6, 2011

Marehemu Tabia wa Kidedea afufuliwa

 Marehemu Dalillah Peter Kisinda ‘Tabia’

Pamoja na kutangulia mbele za haki mwanzoni mwa mwaka huu, Watanzania watapata fursa ya kuona vimbwanga vya aliyekuwa mwigizaji mkubwa Bongo, marehemu Dalillah Peter Kisinda ‘Tabia’ katika muvi yake ya mwisho ya Naomi inayokimbiza sokoni.

Kwa mujibu wa mtayarishaji wa filamu hiyo, Hamis Kibari, watakaoitazama muvi hiyo watagundua kwamba Tabia aliyevuma na Kundi la Kidedea alikuwa hazina kubwa ya uigizaji Bongo kwa jinsi alivyomudu vizuri nafasi yake.