Sep 4, 2018

Je, unajua kuwa kila msanii ni wa kipekee?



KAMA wewe ni msanii, iwe wa uimbaji, uigizaji, uchoraji, uchezaji muziki, uchekeshaji, uandishi n.k., amini usiamini hakuna mtu ambaye ana kila kitu ulicho nacho wewe.

Hata kama binadamu ni wawili wawili, basi anaweza akatokea mtu mmoja tu kati ya watu maelfu ndiyo akakufanana kwa vitu vingi: sura, rangi, uzungumzaji, uwezo wa sanaa, mvuto n.k.

Kitu ambacho pengine hukijui ni kwamba mamilioni ya watu duniani wametafuta msanii kama wewe, mwenye sifa kama zako ili wamtumie kwenye matangazo, kwenye video za muziki, kwenye filamu, kwenye mfululizo wa sinema au michezo ya kuigiza maarufu kama series n.k.

Huu ni ulimwengu wa taarifa kuelekea burudani



ULIMWENGU wa sasa unakwenda kwa spidi kubwa sana na magurudumu yake ni teknolojia ya mitandao.

Dunia ya sasa imepita kwenye ulimwengu wa maarifa, sasa ipo kwenye ulimwengu wa taarifa ikikimbia kwa spidi kubwa kwenye ulimwengu wa burudani. Watu hupenda kuburudishwa zaidi ya kuelimika.

Burudani ni muhimu kwa kuwa inawaleta watu pamoja na ni njia nzuri ya familia nzima kujumuika pamoja. Inawatoa watu kutoka kufikiria changamoto za maisha na kuwaburudisha huku ikiwaondolea msongo wa mawazo unaotokana na ugumu wa maisha.

Kwa kawaida, burudani ni kufurahi, kuchangamka na kufurahisha. Burudani inaweza kuwa muziki, matamasha, simulizi, filamu, michezo, ngoma na maonesho ya jadi.

Mwandishi wa Marekani ambaye pia ni mjasiriamali, na mwalimu, Tony Robbins anabainisha kuwa, “Hatupo katika kizazi cha taarifa na maarifa. Tupo katika kizazi cha burudani na starehe.”

Sep 1, 2018

Sanaa hustawisha fikra



SANAA ni hazina muhimu sana inayohifadhi kazi ya uumbaji, ina lugha pana ambayo hakuna lugha yoyote nyingine yenye upana kama huo.

Hii si lugha ya sayansi, wala lugha ya kawaida, wala lugha ya mawaidha yenye upana kama wa lugha ya sanaa. Inapaswa ipewe umuhimu na pafanyike juhudi za kuhakikisha muundo wa kujivunia wa sanaa unatumiwa.

Bila ya kuwepo sanaa, matamshi ya kawaida hayawezi kupata nafasi yake katika akili ya mtu yeyote yule. Sanaa ni ala na nyenzo nzuri sana ya kufikisha na kupanua fikra sahihi.