Jun 6, 2017

Bibi Esther Mahlangu: Darasa zuri kwa wasanii wa Tanzania

Msanii wa Afrika Kusini, Bibi Esther Mahlangu

NI ukweli usiopingika kuwa sekta ya sanaa nchini ipo chumba cha wagonjwa mahututi, na hatua za makusudi zinahitajika kuchukuliwa (na wasanii wenyewe) kunusuru hali hii.

Nakumbuka miaka ya 1990 hadi 2000, wasanii wa sanaa ya uchoraji walitingisha sana kutokana na kazi zao za michoro. Enzi hizo wachoraji ndio wasanii waliokuwa maarufu (kwa majina yao), ingawa watu hawakuwafahamu kwa sura, kwa kuwa michoro yao ilitamba sana kwenye magazeti na majarida. Na waliweza hata kumiliki magari, japo hayakuwa ya kifahari.