May 30, 2013

Vita ya bidhaa bandia ianze na maudhui






KWA siku za karibuni tumekuwa na mazungumzo ya kina kati Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Shirikisho la Wenye Viwanda Tanzania (CTI) na taasisi zingine kuhusu mpango-mkakati wa nam,naa ya kudhibiti bidhaa bandia na hafifu (counterfeit and substandard) zinazotishia uhai wa soko la kazi za Kitanzania zikiwemo kazi za sanaa (filamu na muziki).

Siku hizi imekuwa si jambo la ajabu kusikia au kushuhudia bidhaa kama nondo za ubora hafifu, betri, TV, mafeni, breki za gari, dawa nk. Jambo hili limekuwa likituumiza mno na sasa tumelishuhudia kwa kasi likivamia sekta ya sanaa kwa kiwango kikubwa na kutishia uhai wa soko la filamu na muziki, hasa kwenye bidhaa kama DVDs, CDs, Tape, Vifungashio (Packaging system) nk, ambazo zinahusiana moja kwa moja na sanaa la filamu. Inaudhi mno pale unaponunua sinema (DVD) unayotegemea kwenda kuangalia nyumbani lakini unapoiweka kwenye deki unaitazama mara moja tu, ukiirudia unagundua kuwa inakwama, na wakati mwingine hugoma hata kabla haijaangaliwa!

May 16, 2013

KILIO CHA WASANII KUIBIWA: Je, ni kweli msanii muigizaji ana hakimiliki?


Mmoja wa wasanii waigizaji nchini, Issa Mussa maaruf kwa jina la Claude

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Said Mwema

MAKALA yangu ya wiki iliyopita iliyohusu mikataba ya wasanii imezua maswali mengine kutoka kwa wasomaji wangu, hasa kutokana na maswali kadhaa niliyoyaibua kuhusu ile hoja ya kilio cha wasanii kulia kuibiwa kazi zao. maswali niliyoyaibua ni kama: Je, ni kweli wanaibiwa? Na kama wanaibiwa, huwa wanaibiwaje? Je, ni kweli uharamia (piracy) wa kazi za filamu ndiyo tatizo kubwa kwenye tasnia ya filamu nchini? Kama ni kubwa lipo kwa kiwango gani? Hivi, wasanii wanayafahamu kweli matatizo yao ya msingi?

Baadhi ya wasomaji wamenitaka niyatolee ufafanuzi maswali haya ili hata wao waelewe kwa kina kinachotokea kwani nimezidi kuwaacha gizani. Ndiyo maana wiki hii nimekuja na swali litakalosaidia kutafuta majibu ya maswali haya; je, ni msanii wa filamu ana hakimiliki?

May 9, 2013

Malalamiko ya wizi wa kazi za Sanaa: Tuwe na elimu endelevu kuhusu mikataba


Biashara ya filamu huambatana na matangazo kama inavyoonekana kwenye picha hii

MAPEMA wiki hii nilipata nafasi ya kuhudhuria warsha ya siku tatu ya wadau wa filamu iliyokuwa na lengo la kutafuta njia nzuri ya namna ya kutatua matatizo ya wasanii na wadau wa filamu badala ya tabia iliyojengeka ya kumtafuta mchawi jambo ambalo limekuwa halitusaidii.

Warsha ilitokana na kilio cha muda mrefu cha wasanii kudai kuibiwa kazi zao huku baadhi ya waliokuwa wakisukumiwa lawama wakiwa ni wamili wa maktaba za video na wenye mabanda ya kuoneshea video. Warsha hii pia ilikuwa na kusudio la kuangalia mzunguko wa biashara ya filamu nchini kuanzia inapotengenezwa hadi kumfikia mtu wa mwisho (mtazamaji). Warsha hii iliandaliwa na taasisi ya MFDI-Tanzania kwa lengo la kuangalia namna ya kutatua tatizo la usambazaji nchini.