![]() |
Waandishi mahiri wa script Tanzania, Dk.Vicensia Shule na Bishop Hiluka, katika moja ya mikutano ya Bodi ya Filamu |
Ikiwa una matumaini kuwa
siku moja utakuja kufanya kazi ya uandishi wa script kwa ajili ya filamu au
televisheni, basi unahitaji kuwa na ufahamu wa jinsi ya kuandika “spec” script. Spec Script
ni kifupi cha Speculative script, huu ni
uandishi wa filamu wa kubahatisha
(speculation),
ambao kama mwandishi unaandika script yako ukiwa hujui nani atakuja kutumia
script hiyo – hii humaanisha kuwa unaandika
script bure (pasipo kulipwa au kuajiriwa na mtu). Kwa maana
nyingine ni kwamba hakuna mtu aliyekuajiri au anayekulipa kuandika script hiyo.
Unaandika
ukiwa na matumaini ya kuja kuuza kwa mnunuzi yeyote atakayevutiwa
na kisa chako au kuajiriwa kwa ajili ya
kuandika script kwa sababu ya hiyo, lakini ili kuwa na nafasi au uwezekano,
huna uchaguzi bali kuandika spec script.