Jan 19, 2011

Jukwaa la Sanaa lakutanisha Wadau wa filamu na Wasomi

Prof. Amandina Lihamba akiongea kwenye Jukwaa la Sanaa, 
kushoto ni Katibu Mtendaji wa Basata, Gonche Materego

Idara ya Sanaa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam 
ambapo ni chimbuko la wasomi katika sanaa

Nembo ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam 
wanapotoka wasomi wa kada mbalimbali

Amandina Lihamba na marehemu Kaduma 
kwenye sinema ya Harusi ya Mariam

Jukwaa la Sanaa la Baraza la Taifa la Sanaa la Taifa linalofanyika kila Jumatatu limekuwa kiungo muhimu kwa wadau mbalimbali wa sanaa hapa nchini, Jumatatu hii ya tarehe 17 Januari, 2011 Jukwaa hilo lilishuhudia wasomi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na waigizaji mahiri katika tasnia ya filamu Tanzania wakijadili kuhusu mustakabali wa Tasnia ya Filamu Tanzania chini ya uratibu wa Profesa Amandina Lihamba.


Monalisa akiwa kashika tuzo aliyoipata ZIFF

Single Mtambalike (Richie)

Katika Jukwaa la Sanaa siku hiyo kuliendeshwa darasa kwa pande zote mbili, wasanii waliongozwa na Yvonne Cheryl maarufu kama Monalisa na Single Mtambalike maaruf kama Rich Richie huku upande wa Chuo Kikuu ukiongozwa na Prof. Amandina Lihamba na Dk. Mona Mwakalinga.

Dk. Mwakalinga alielezea kuhusu historia ya filamu Tanzania na kubainisha kuwa ni nchi ya kwanza Kusini mwa Jangwa la Sahara ukiitoa Afrika Kusini, filamu kwanza iliyotengenezwa Tanzania ilitolewa mwaka 1935 kwa nakala 35

No comments: