![]() |
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, akiwa katika Operesheni ya kuwasaka waharamia wanaodurufu kazi za wasanii |
SERIKALI ya Awamu ya Tano imeanza kuonesha juhudi katika
kuisaidia sekta ya sanaa nchini baada ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na
Michezo, Nape Nnauye, kuingia mtaani na kukamata DVDs zisizo na stika ya TRA
zinazoingia nchini kinyume na sheria pamoja na zile zinazokwepa kulipa kodi ili
kuinua uchumi wa nchi na wasanii.
Waziri Nape Nnauye ameahidi kuwa zoezi hilo litakuwa
endelevu nchi nzima akisisitiza kuwa hatua hii ni ya mwanzo kwa kuwaonesha kuwa
agizo la Rais John Pombe Magufuli, la kulipa kodi na kununua bidhaa halisi kwa
kutoa risiti linasimamiwa ipasavyo.