![]() |
Rais Mteule Dk. John Pombe Magufuli, akijiachia jukwaani pamoja na wasanii wa kundi la Yamoto Band kwenye uwanja wa Mashujaa mkoani Mtwara, wakati wa kampeni |
KWANZA kabisa napenda nikupongeze kwa kuchaguliwa kuwa Rais
wa Tanzania katika Awamu ya Tano, nikitumaini kuwa wananchi wamekupa ridhaa kwa
kuwa wamekuona unafaa zaidi kuiongoza nchi hii baada ya Rais Jakaya Kikwete,
ambaye uongozi wake unahitimishwa kesho Alhamisi.
Ingawa kuna minong’ono na wasiwasi mwingi kuwa huenda
wewe huna ‘interest’ kabisa na masuala ya sanaa, na uongozi wako utajikita
zaidi kwenye kujenga barabara, reli, uwekezaji, kilimo, mifugo, uchimbaji
madini nk, lakini nina imani kuwa uongozi wako utawapa wasanii tumaini jipya.