Dec 4, 2009

Tanzania Film Federation & Baraza la Sanaa la Taifa

Mkurugenzi wa TAFF Haji Adam akisisitiza jambo

Katibu Mkuu, Bishop Hiluka, akiwa na mjumbe wa TAFF, Issa Mussa (Cloud) 
na Naibu Katibu, Simon Mwakifwamba (Jaspa) nje ya ukumbi wa Basata

Jumanne ya tarehe 1/12/2009 kulikuwa na mkutano kati ya Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) na Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), kikao hicho kiliitishwa na Basata kufuatia wadau hao wa TAFF kuliandikia barua Baraza kutaka kujua hatma ya usajiri wa shirikisho kufuatia mizengwe ambayo imejitokeza.

Katika kikao hicho mambo mengi yalijadiliwa na kisha kuundwa timu ya watu kumi kutoka TAFF na Shirikisho la Picha Jongefu ili kuangalia kwa undani mchakato mzima wa uundwaji wa shirikisho imara litakalokuwa chombo cha wadau hawa huku Basata wakilazimika kuridhia.
Katibu Mtendaji wa Basata, Ghonche Materego, akieleza jambo kwa viongozi wa TAFF na Picha Jongefu. Pembeni yake ni Mwalimu Masimbi

Mwakilishi wa Basata akieleza jambo

Wajumbe wa Shirikisho la Picha Jongefu, Agnes Lukanga (kulia), 
Richard Ndunguru (katikati) na Denis Sweya

Mjumbe wa TAFF, Issa Mussa (Cloud) akieleza jambo

Viongozi wa TAFF wakiwa nje ya ukumbi, kutoka kushoto: Steven Kanumba, 
Bishop Hiluka, Issa Mussa (Cloud) na Simon Mwakifwamba (Jaspa)

Katibu Mkuu wa TAFF, Bishop J. Hiluka, akiandika majina matano ya wajumbe 
watakaowakilisha katika mchakato wa usajiri wa shirikisho

Wajumbe wa Basata wakisikiliza kwa makini

Mjumbe wa TAFF, Mike Sangu, akizungumza. Pembeni yake ni Steven Kanumba

Mzee Mayanga akisikiliza huku akinukuu mambo muhimu

No comments: