![]() |
Msanii wa Afrika Kusini, Bibi Esther Mahlangu |
NI ukweli usiopingika kuwa sekta ya sanaa nchini
ipo chumba cha wagonjwa mahututi, na hatua za makusudi zinahitajika kuchukuliwa
(na wasanii wenyewe) kunusuru hali hii.
Nakumbuka miaka ya 1990 hadi 2000, wasanii wa
sanaa ya uchoraji walitingisha sana kutokana na kazi zao za michoro. Enzi hizo
wachoraji ndio wasanii waliokuwa maarufu (kwa majina yao), ingawa watu
hawakuwafahamu kwa sura, kwa kuwa michoro yao ilitamba sana kwenye magazeti na
majarida. Na waliweza hata kumiliki magari, japo hayakuwa ya kifahari.