![]() |
Mlima Kilimanjaro |
KATIKA nchi hii kuna maeneo bora ya upigaji picha,
kuanzia Tanzania Bara hadi Zanzibar, kuanzia kwenye mlima mrefu hadi kwenye
maziwa yenye kina kirefu kabisa katika Bara la Afrika.Tanzania ni nchi ya maajabu na vivutio: mlima
mrefu Afrika (Mlima Kilimanjaro), mbuga bora yenye wanyama wa kuvutia duniani
ya Serengeti, yenye stori ya wanyama wanaohama kila mwaka na kurejea.
Bila kuzunguka, hebu tutafakari ni kwa namna gani
filamu na muziki vimeweza kuitangaza Nigeria? Tuanzie filamu, tasnia yao ya filamu (Nollywood)
imeweza kuwatangaza kwa kiasi gani? Tutapata jibu la haraka kwamba taifa hilo
limetangazika kwa kiwango ambacho siyo cha kawaida wala cha chini.