IMEANDIKWA, “Kila siri iliyo moyoni kwa mwandishi, kila
aina ya maisha aliyoyapitia, au kipimo cha akili ya mwandishi vimeainishwa kwa
kiasi kikubwa katika maandishi yake...” hii inamaanisha kuwa kazi za kimaandishi
za waandishi huwaonesha wao ni kina nani, wametokea mazingira gani, wana uwezo
gani wa kufikiri na wanataka kuwa nani.
Kupitia kujielewa wenyewe na kuridhika katika uasili
wetu, mchakato wa kuandika huwa unakuwa wa hiari zaidi na hauzuiliki.
Tunapoelewa kuwa tuna talanta (kipaji) ya kipekee ya uandishi tuliyotunukiwa na
Mungu, inatusaidia zaidi katika kuandaa makala au hadithi nzuri.