Feb 22, 2011

Wasanii watakiwa kuacha kulewa sifa

Sehemu ya mji wa Morogoro

Husna Posh (Dotnata), mmoja wa wasanii wenye mafaniko makubwa

Na Ashton Balaigwa
Morogoro

Wasanii nchini wametakiwa kuacha kulewa sifa mara baada ya kupata mafanikio na badala yake watumie vipaji walivyonavyo kuelimisha kwa kutumia njia zitakazoisaidia jamii kutambua mahala tulipo na tunakoelekea.

Wito huo umetolewa na mwanasheria wa Kituo cha Wasaidizi wa Sheria kwa Wanawake na Watoto cha mjini Morogoro, Aman Mwaipaja, wakati akizungumza na wasanii chipukizi wa maigizo wa Kikundi cha Mikano Arts Group.

Mwaipaja aliwataka wasanii hao kujituma ili waweze kupata mafanikio kama wasanii wengine wakubwa na kuacha tabia ya majigambo.

Aliwataka wasanii hao kuchekesha kwa kutumia kipaji walichopewa na Mungu katika kuelimisha jamii kama walivyofanikiwa wasanii wengine wa kuchekesha. Aidha aliwataka wasanii hao kutunga maigizo yanayotoa elimu kuhusiana na gonjwa la Ukimwi kwani bado kuna baadhi yao hawana uelewa wa kutosha licha ya kuwa elimu hiyo inatolewa kaatika maeneo mengi.

SOURCE: NIPASHE

No comments: