Sep 4, 2018

Je, unajua kuwa kila msanii ni wa kipekee?



KAMA wewe ni msanii, iwe wa uimbaji, uigizaji, uchoraji, uchezaji muziki, uchekeshaji, uandishi n.k., amini usiamini hakuna mtu ambaye ana kila kitu ulicho nacho wewe.

Hata kama binadamu ni wawili wawili, basi anaweza akatokea mtu mmoja tu kati ya watu maelfu ndiyo akakufanana kwa vitu vingi: sura, rangi, uzungumzaji, uwezo wa sanaa, mvuto n.k.

Kitu ambacho pengine hukijui ni kwamba mamilioni ya watu duniani wametafuta msanii kama wewe, mwenye sifa kama zako ili wamtumie kwenye matangazo, kwenye video za muziki, kwenye filamu, kwenye mfululizo wa sinema au michezo ya kuigiza maarufu kama series n.k.

Huu ni ulimwengu wa taarifa kuelekea burudani



ULIMWENGU wa sasa unakwenda kwa spidi kubwa sana na magurudumu yake ni teknolojia ya mitandao.

Dunia ya sasa imepita kwenye ulimwengu wa maarifa, sasa ipo kwenye ulimwengu wa taarifa ikikimbia kwa spidi kubwa kwenye ulimwengu wa burudani. Watu hupenda kuburudishwa zaidi ya kuelimika.

Burudani ni muhimu kwa kuwa inawaleta watu pamoja na ni njia nzuri ya familia nzima kujumuika pamoja. Inawatoa watu kutoka kufikiria changamoto za maisha na kuwaburudisha huku ikiwaondolea msongo wa mawazo unaotokana na ugumu wa maisha.

Kwa kawaida, burudani ni kufurahi, kuchangamka na kufurahisha. Burudani inaweza kuwa muziki, matamasha, simulizi, filamu, michezo, ngoma na maonesho ya jadi.

Mwandishi wa Marekani ambaye pia ni mjasiriamali, na mwalimu, Tony Robbins anabainisha kuwa, “Hatupo katika kizazi cha taarifa na maarifa. Tupo katika kizazi cha burudani na starehe.”

Sep 1, 2018

Sanaa hustawisha fikra



SANAA ni hazina muhimu sana inayohifadhi kazi ya uumbaji, ina lugha pana ambayo hakuna lugha yoyote nyingine yenye upana kama huo.

Hii si lugha ya sayansi, wala lugha ya kawaida, wala lugha ya mawaidha yenye upana kama wa lugha ya sanaa. Inapaswa ipewe umuhimu na pafanyike juhudi za kuhakikisha muundo wa kujivunia wa sanaa unatumiwa.

Bila ya kuwepo sanaa, matamshi ya kawaida hayawezi kupata nafasi yake katika akili ya mtu yeyote yule. Sanaa ni ala na nyenzo nzuri sana ya kufikisha na kupanua fikra sahihi.

Aug 17, 2018

Tuviendeleze vipaji ili viitangaze nchi kimataifa



KILA mtu aliyezaliwa na mwanamke anacho kitu cha pekee alichojaaliwa kuwa nacho. Kitu hiki si umbile lake, elimu yake, umaarufu wake, usomi wake, cheo chake katika jamii, au utajiri wake wa vitu na fedha; la hasha, bali ni kipaji chake.

Kipaji ni uwezo wa kiasili ulio ndani ya mtu katika maumbile, nafsi na roho yake. Kipaji kinatoka ndani yake. Ni tunu au zawadi toka kwa Mungu ambayo hakuna anayeweza kutunyang’anya au kutuibia mpaka tutakapokufa.

Fedha na magari vyaweza kuibiwa, nyumba inaweza kuanguka, kubomoka, kubomolewa au hata kuungua, lakini vipaji hubakia kuwa nasi daima.

Kipaji ni karama. Ni zawadi anayokirimiwa mtu kutoka kwa Mungu. Kipaji hiki hukua katika ufanisi na matumizi ikiwa kitakuzwa na kuendelezwa na kimenuiwa kutumika kwa niaba ya vingine, si kwa ajili ya ubinafsi bali kwa faida ya wengine na si yake wenyewe.

Tunapomuomboleza King Majuto tusisahau somo alilotuachia

Wachekeshaji mahiri nchini ambao kwa sasa ni marehemu, King Majuto na Sharo Milionea

WIKI iliyopita tasnia ya vichekesho na wapenda burudani tulipata pigo kwa msiba uliogusa na kuwashtua watu wengi sana, wafuatiliaji na wasio wafuatiliaji wa sanaa ya vichekesho, kutokana na kifo cha King Majuto.

King Majuto ambaye jina lake halisi aliitwa Amri Athuman alikuwa msanii mkongwe na maarufu nchini Tanzania na Afrika Mashariki, na gwiji wa vichekesho ambaye umahiri wake ulikuwa wa aina yake.

Majuto alifariki dunia wakati akipokea matibabu kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam, majira ya saa 2 usiku wa Jumatano Agosti 8, 2018 akiwa amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi.

Baada tu ya kifo chake watu maarufu ndani na nje ya Tanzania walituma salamu za rambirambi kwa familia yake kupitia mitandao ya kijamii, miongoni mwao akiwa Rais wa Tanzania, John Magufuli.

Tumeitupa misingi ya michezo kwa binadamu



MICHEZO si tu kwamba ina faida kubwa sana kwa mwanadamu na nchi, pia ni chombo cha kuwasilisha tunu msingi katika kuboresha ubinadamu na katika ujenzi wa jamii ya amani na ya kindugu.

Kwa kauli hiyo yatari tunapata wazo kuu juu ya michezo kwa ujumla ya kwamba michezo imekuwa na lengo kuu msingi tangu zamani za kale la kujenga undugu na amani.

Kama mchezo ni chombo cha kuwasilisha tunu ya binadamu mwenyewe, kujieleza mwenyewe, kukubalika mwenyewe na kujikubali, inamaana kwamba nchi yoyote haiwezi kutambulikana na utaifa wake bila kuwa na utamaduni wao, na mojawapo ya viungo vya utamaduni huo vinavyounganisha katika dunia hii ni michezo.

Aretha Franklin: Malkia wa Soul aliyeishi maisha ya ‘mateso ya kimyakimya’



MUZIKI ni chombo ambacho kimewavutia wanadamu. Katika kutumia nyimbo, waimbaji wameweza kuhifadhi historia na utamaduni wa jamii zao.

Muziki umekuwa ukitumika kama njia mojawapo ya kujifundisha utamaduni na aghalabu hutumiwa katika kumwelezea mtu, mazingira yake na jinsi anavyoweza kuyatumia na kuyatunza vilivyo.

Kama chombo ambacho hutumiwa kuelezea historia ya jamii, muziki hutumiwa kupasha ujumbe maalumu kwa wanajamii hasa kutoka kizazi kimoja hadi kingine na hutumiwa hasa kuelezea historia, imani, itikadi na kaida zajamii.

Nyimbo kama zao la mazingira ya jamii, zinaweza kufananishwa na mtoto ambaye hufinyangwa na mambo mengi katika historia ya jamii yake.
Hata hivyo, muziki ni zaidi ya taaluma kama zilivyo taaluma zingine za sheria, uhandisi, udaktari, usimamizi wa fedha, biashara na kadhalika. muziki ni kipawa ambacho mtu hutunukiwa na Mungu.