Aug 17, 2018

Tuviendeleze vipaji ili viitangaze nchi kimataifa



KILA mtu aliyezaliwa na mwanamke anacho kitu cha pekee alichojaaliwa kuwa nacho. Kitu hiki si umbile lake, elimu yake, umaarufu wake, usomi wake, cheo chake katika jamii, au utajiri wake wa vitu na fedha; la hasha, bali ni kipaji chake.

Kipaji ni uwezo wa kiasili ulio ndani ya mtu katika maumbile, nafsi na roho yake. Kipaji kinatoka ndani yake. Ni tunu au zawadi toka kwa Mungu ambayo hakuna anayeweza kutunyang’anya au kutuibia mpaka tutakapokufa.

Fedha na magari vyaweza kuibiwa, nyumba inaweza kuanguka, kubomoka, kubomolewa au hata kuungua, lakini vipaji hubakia kuwa nasi daima.

Kipaji ni karama. Ni zawadi anayokirimiwa mtu kutoka kwa Mungu. Kipaji hiki hukua katika ufanisi na matumizi ikiwa kitakuzwa na kuendelezwa na kimenuiwa kutumika kwa niaba ya vingine, si kwa ajili ya ubinafsi bali kwa faida ya wengine na si yake wenyewe.

Tunapomuomboleza King Majuto tusisahau somo alilotuachia

Wachekeshaji mahiri nchini ambao kwa sasa ni marehemu, King Majuto na Sharo Milionea

WIKI iliyopita tasnia ya vichekesho na wapenda burudani tulipata pigo kwa msiba uliogusa na kuwashtua watu wengi sana, wafuatiliaji na wasio wafuatiliaji wa sanaa ya vichekesho, kutokana na kifo cha King Majuto.

King Majuto ambaye jina lake halisi aliitwa Amri Athuman alikuwa msanii mkongwe na maarufu nchini Tanzania na Afrika Mashariki, na gwiji wa vichekesho ambaye umahiri wake ulikuwa wa aina yake.

Majuto alifariki dunia wakati akipokea matibabu kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam, majira ya saa 2 usiku wa Jumatano Agosti 8, 2018 akiwa amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi.

Baada tu ya kifo chake watu maarufu ndani na nje ya Tanzania walituma salamu za rambirambi kwa familia yake kupitia mitandao ya kijamii, miongoni mwao akiwa Rais wa Tanzania, John Magufuli.

Tumeitupa misingi ya michezo kwa binadamu



MICHEZO si tu kwamba ina faida kubwa sana kwa mwanadamu na nchi, pia ni chombo cha kuwasilisha tunu msingi katika kuboresha ubinadamu na katika ujenzi wa jamii ya amani na ya kindugu.

Kwa kauli hiyo yatari tunapata wazo kuu juu ya michezo kwa ujumla ya kwamba michezo imekuwa na lengo kuu msingi tangu zamani za kale la kujenga undugu na amani.

Kama mchezo ni chombo cha kuwasilisha tunu ya binadamu mwenyewe, kujieleza mwenyewe, kukubalika mwenyewe na kujikubali, inamaana kwamba nchi yoyote haiwezi kutambulikana na utaifa wake bila kuwa na utamaduni wao, na mojawapo ya viungo vya utamaduni huo vinavyounganisha katika dunia hii ni michezo.

Aretha Franklin: Malkia wa Soul aliyeishi maisha ya ‘mateso ya kimyakimya’



MUZIKI ni chombo ambacho kimewavutia wanadamu. Katika kutumia nyimbo, waimbaji wameweza kuhifadhi historia na utamaduni wa jamii zao.

Muziki umekuwa ukitumika kama njia mojawapo ya kujifundisha utamaduni na aghalabu hutumiwa katika kumwelezea mtu, mazingira yake na jinsi anavyoweza kuyatumia na kuyatunza vilivyo.

Kama chombo ambacho hutumiwa kuelezea historia ya jamii, muziki hutumiwa kupasha ujumbe maalumu kwa wanajamii hasa kutoka kizazi kimoja hadi kingine na hutumiwa hasa kuelezea historia, imani, itikadi na kaida zajamii.

Nyimbo kama zao la mazingira ya jamii, zinaweza kufananishwa na mtoto ambaye hufinyangwa na mambo mengi katika historia ya jamii yake.
Hata hivyo, muziki ni zaidi ya taaluma kama zilivyo taaluma zingine za sheria, uhandisi, udaktari, usimamizi wa fedha, biashara na kadhalika. muziki ni kipawa ambacho mtu hutunukiwa na Mungu.

Aug 12, 2018

King Majuto atabaki kuwa nembo ya tasnia ya ucheshi nchini



WASANII wakongwe na mahiri nchini wa sanaa ya maigizo, hususan wa vichekesho wanazidi kupukutika, na kuwaacha wasanii wachanga wakiwa katika mkanganyiko.

Nawakumbuka wasanii ambao walikuwa mahiri sana katika sanaa ya maigizo na vichekesho enzi za uhai wao na sasa hatupo nao ni pamoja na Ibrahim Raha (Mzee Jongo), Fundi Said (Mzee Kipara), Rajab Kibwana Hatia (Mzee Pwagu) na Ali Said Keto (Pwaguzi).

Wengine ni Hamis Tajiri (Janja au Meneja Mikupuo) Tunu Mrisho (Mama Haambiliki), Branco Minyugu, Bartholomew Milulu (Masawe), Said Ngamba (Mzee Small), Said Maulid Banda (Max) na wengine.

Wasanii hawa waliifanya sanaa ya maigizo, hususan ucheshi (comedy) kujizolea umaarufu mkubwa nchini na hivyo kuwafanya vijana wengi nchini kuingia kwenye sanaa ya vichekesho.

Tuitumie fursa ya burudani kukuza uchumi na kuongeza ajira

Diamond Platnumz akitumbuiza


“HATUPO katika kizazi cha taarifa na maarifa. Tupo katika kizazi cha BURUDANI na STAREHE.” Tony Robbins.

Tony Robbins ni mwandishi wa Marekani, mjasiriamali, mwalimu na anajulikana kwa matangazo yake kwenye runinga, semina na vitabu, ikiwa ni pamoja na ‘Unlimited Power’ na ‘Awaken the Giant Within’.

Burudani ni biashara inayokua kwa kasi sana barani Afrika zaidi ya kawaida. Sekta ya burudani imejaa fursa nyingi sana kupita kawaida. Yeyote atakayeamua kuichunguza sekta hii kwa makini atashangaa fursa zilizojaa.

Kila siku mamilioni ya watu duniani wanahangaika kutafuta sehemu za kustarehe, vitu vya kujistarehesha na kujiburudisha, michezo na matamasha ya kufurahisha.

Tujitafakari upya kwenye Bongo Fleva

Wanamuziki Profesa Jay (kushoto) na MwanaFA


MUZIKI kama chombo ambacho hutumiwa kuelezea historia ya jamii, hupasha ujumbe maalumu kwa wanajamii, hasa kutoka kizazi kimoja hadi kingine na hutumiwa kuelezea historia, imani, itikadi na kaida za jamii.

Kwa kawaida nyimbo ni zao la mazingira ya jamii. Zinaweza kufananishwa na mtoto ambaye hufinyangwa na mambo mengi katika historia ya jamii yake.

Hii inamaanisha kwamba muziki hauibuki katika ombwe tupu na hauwezi vilevile kujiundia mazingira yake yenyewe. Mabadiliko na maendeleo ya muziki yamekuwa yakifuatana na historia ya watu wenyewe.

Umuhimu wa muziki unadhihirika katika matumizi ya nyimbo katika wakati maalumu kama njia mojawapo ya kuanzisha mabadiliko katika tabia za jamii au mtu binafsi.

Hatuwezi kuitenganisha sekta ya sanaa na utalii


TANZANIA ni moja ya sehemu bora kabisa duniani ambazo msanii atafurahia kutengeneza filamu yake au kupigia picha za video kwa muziki wake, historia, utamaduni na wanyamapori.

Kuna hali ya hewa nzuri na watu wakarimu ambao wako tayari kumkaribisha mgeni katika mtazamo wa Kitanzania.

Imekuwa inashangaza kuona wasanii wetu wanakwenda kufanya video zao Afrika Kusini na Kenya, wakati Tanzania inashika nafasi ya pili duniani, nyuma ya Brazil, kwa kuwa na vivutio vingi vya utalii huku nchi ya Afrika ya Kusini ikishika nafasi ya 14.

Tupaze sauti dunia ijue kuhusu michoro ya Tingatinga


SANAA ya ufundi ambayo inajumuisha uchoraji, upakaji rangi picha, ufinyanzi, uchongaji na utengenezaji wa mapambo mbalimbali ya asili ni utamaduni ambao, kwa mujibu wa machapisho mbalimbali, ilianza nchini Tanzania.

Sanaa ya uchoraji ilianzia nchini Tanzania takribani miaka 5,000 iliyopita na uthibitisho halisi ni michoro iliyopo katika mapango ya Kondoa Irangi.

Kwa miongo kadhaa, Tanzania imejulikana kwa umahiri wa uchoraji wa picha licha ya kuwa Watanzania wenyewe wametajwa kujiona kuwa siyo walengwa husika wa sanaa hii.
Sanaa ya uchoraji ni lugha ambayo ina ulingo mpana na kila msanii ana lugha yake na wapo wasanii ambao wanafanana katika mfumo wa sanaa wanayofanya na wengine hawafanani kabisa.