· Ni
wakati sasa mfikirie kuwa na dira
Wafanyuakazi wa Mamlaka ya Mapato (TRA) walipotembelea wauzaji wa filamu za Tanzania kuhakiki kazi zenye stempu za TRA |
Mmoja wa wasanii wa filamu Tanzania, Vicent Kigosi, maarufu kama Ray |
KWA Tanzania hakuna msanii
yeyote anayeweza kusimama na kujisifu kwamba anakula halali kulingana na wingi
wa jasho lake. Kila mmoja anatambua kuwa kuna mfumo kandamizi unaonyonya jasho
la wasanii. Na ili kuendelea kuwanyonya, sasa wameaminishwa (na wale
waliolishika soko) kuwa soko la kazi zao limekufa.
Wameaminishwa
hivyo kwa kuwa soko la kazi zao linadhibitiwa na wafanyabiashara wachache,
wasiozingatia taaluma na wasioongozwa na weledi. Ki ukweli kwa sasa soko
halieleweki kabisa! Hali hii imesababisha watu kushindwa kutofautisha iwapo
wanachokiona ni filamu, maigizo au mkanda wa harusi wenye “taito” za majina ya
wasanii na wafanyabiashara wenye asili ya Kiasia!