Dec 31, 2017

Mwaka 2017 umekwisha, dira ya wasanii ni ipi?

Wasanii mbalimbali wakifuatilia mjadala kwenye ukumbi wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA)

Msanii akipiga tarumbeta

HEBU fikiria, unaamka asubuhi na mapema, unajiandaa na kubeba begi lako kisha unaelekea kituo cha basi, unalikuta gari na kupanda, lakini hujui unaelekea wapi!

Au mpo katika kituo cha mabasi, mara basi linakuja, kila mmoja analikimbilia na kupanda, tena mnafikia hatua ya kugombea siti, na safari inapoanza ndipo mnagundua kuwa gari haliendi kule mnakokwenda. Mnataharuki na kuanza kumpigia kelele dereva kumtaka asimamishe gari!

Dereva anawashangaa na analiegesha gari pembeni, kisha anawauliza kwani ninyi mnaelekea wapi? Hapo ndipo mnapojigundua kuwa kila mmoja anaelekea sehemu tofauti kabisa na linakokwenda gari!